Tanzania na changamoto ya Ajira

Tanzania na changamoto ya Ajira

Alloyce PR

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2020
Posts
590
Reaction score
706
“Changamoto ya ajira nchini Tanzania haiko kwenye ukosefu wa kazi, bali kwenye mfumo wa unyonyaji unaoendelea, hususan katika sekta binafsi. Watu wanatumia muda wao mwingi, maarifa yao ya hali ya juu, na nguvu zao kuzalisha thamani kubwa kwa waajiri, lakini malipo wanayopata ni duni, yasiyolingana na juhudi zao. Wengine hulipwa kwa kuchelewa, wengine hawalipwi kabisa/wanadhulumiwa. Hili si tatizo la ajira, bali ni udhalilishaji wa nguvu kazi. Na hapo ndipo penye kiini cha changamoto. Na hiyo ndiyo chanzo kikubwa cha kukuza ukatili wa kijamii, kiuchumi na kisaikolojia.”-Alloyce, P.R.
 
Tuko vizuriii
1000043588.jpg
 
Sijawahi kusikia wanasiasa na viongozi.wanazungumzia wages kwenye report au hotuba zao.
 
“Changamoto ya ajira nchini Tanzania haiko kwenye ukosefu wa kazi, bali kwenye mfumo wa unyonyaji unaoendelea, hususan katika sekta binafsi
Anasema hatuwezi kuandamana hapa mtandaoni

16 June 2025

''MTU ALIYEKUWA na MAKAZI BORA HAWEZI KUANDAMANA'' - MKURUGENZI MTENDAJI NHC AFUNGUKA...

View: https://m.youtube.com/watch?v=1g3Au2S8JUI

Shirika la Nyumba la Taifa NHC limeelezea jinsi lilivyokwamuliwa na Utawala wa mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuliwezesha kukamilisha miradi yake ya makazi bora na ya kisasa.

Akizungumza na wahariri Dar leo, Mkurugenzi Mtendaji wa NHC Hamad Abdallah amesema miongoni mwa miradi ambayo ilikwama kama vile mradi wa Golden Premier Regence ambao ulikwama kwa miaka nane sasa miradi huo umefufuliwa kwa jitihada za Rais Samia na tayari mkandarasi sasa anaendelea na kazi....

Milango ya kwenye nyumba hizi za NHC tumenunua kutoka China, maana milango bora ya mbao haipo hapa Tanzania, milango hiyo ya kutoka China ni imara hakuna haja ya kuweka mageti milangoni..

Tumeona wale wanao andamana Kenya wengi wanatokea mitaa ya masikini ya mabanda kule Kibera Nairobi...anasema mkurugenzi wa NHC Hamad Abdallah
 
Anasema hatuwezi kuandamana hapa mtandaoni

16 June 2025

''MTU ALIYEKUWA na MAKAZI BORA HAWEZI KUANDAMANA'' - MKURUGENZI MTENDAJI NHC AFUNGUKA...

View: https://m.youtube.com/watch?v=1g3Au2S8JUI

Shirika la Nyumba la Taifa NHC limeelezea jinsi lilivyokwamuliwa na Utawala wa mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuliwezesha kukamilisha miradi yake ya makazi bora na ya kisasa.

Akizungumza na wahariri Dar leo, Mkurugenzi Mtendaji wa NHC Hamad Abdallah amesema miongoni mwa miradi ambayo ilikwama kama vile mradi wa Golden Premier Regence ambao ulikwama kwa miaka nane sasa miradi huo umefufuliwa kwa jitihada za Rais Samia na tayari mkandarasi sasa anaendelea na kazi....

Asante sana kwa taarifa mkuu. 🙏🙏
 
Back
Top Bottom