Wawakilishi wa serikali ya uingereza katika eneo lililokuja kuitwa Tanganyika baadae, wakashauri majina yafuatayo ndiyo yatumike kutambulisha eneo husika:
1. New Maryland - serikali ya uingereza ikalikataa.
2. Smutsland - likakataliwa.
3. Victoria - likakataliwa.
4. Ebumea - likakataliwa.
5. Windsorland - nalo likakataliwa.
Iwapo umma wa wazanzibari bila ya ushawishi wowote kutoka nje, na kwa sababu zao wenyewe, wataona kuwa muungao una hasara kwa uhai wao, sitowapiga mabomu kuwalazimisha. Muungano utakuwa hauna tena sababu ya kuendelea iwapo washiriki wake wataamua kuukana
Bara lenye ukubwa wake kamili, moja na lisilohgawika, ndilo nataka liwepo. Hii haina maana huku ni kuwa na serrikali moja kwa bara lote,katika hali ya kuwa na serikali kuu yenye mamlaka yote. Kinachotakiwa ni kuwa na serikali moja inayounganisha nyingi na kuwa na mamlaka katika maeneo fulani fulani. Zaidi ya hapo kunaweza kuwepo na serikali nyenginezo, hizi zikiwa na mamlaka yaliyo hafifu kidogo, na mamlaka hayo yakiwa yanatokana zaidi na katiba za ndani na sio kutoka serikali kuu. Hii ni sawa na kusema kuwa Africa mpya inaweza kuwa ni dola ya shirikisho, ambayo nguvu zake zitagawiwa baina ya serikali za mataifa washiriki kwa mujibu wa matakwa ya waanzilishi na vizazi vijavyo.
Mkataba wa Muungano Baina Ya Jamhuri Ya Tanganyika na Jamhuri Ya Watu Wa Zanzibar.
Jamhuri Ya Muungano Wa Tanganyika Na Zanzibar
Sherria ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, 1964, Na. 22 ya 1964.
Kila siku kuna swali halijibiwi. Ni nini legal foundation ya muungano huu unaopigiwa debe wa serikali 2?
Legal foundation ya serikali 3 ni article of union ya mwaka 1964.
Mambo yafuatayo ndiyo yatakayokuwa chini ya Bunge na serikali ya jamhuri ya muungano:
1. Katiba na serikali ya jamhuri ya muungano.
2.Mambo ya nchi za nje.
3.Ulinzi
4.Polisi
5.Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya hatari
6.Uraia
7.Uhamiaji
8.Mikopo na biashara ya nchi za je
9.Utumishi katika jamhuri ya muungano.
10. Kodi ya mapato inayolipwa na watu binafsi, ushuru wa forodha a ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini na kusimamiwa na idara ya forodha.
11.Bandari, mambo yanayohusu usafiri wa anga, posta na simu.
Bara lenyeukubwa wake kamili, moja na lisilohgawika, ndilo nataka liwepo. Hii haina maana huku ni kuwa na serrikali moja kwa bara lote,katika hali ya kuwa na serikali kuu yenye mamlaka yote. Kinachotakiwa ni kuwa na serikali moja inayounganisha nyingi na kuwa na mamlaka katika maeneo fulani fulani. Zaidi ya hapo kunaweza kuwepo na serikali nyenginezo, hizi zikiwa na mamlaka yaliyo hafifu kidogo, na mamlaka hayo yakiwa yanatokana zaidi na katiba za ndani na sio kutoka serikali kuu. Hii ni sawa na kusema kuwa Africa mpya inaweza kuwa ni dola ya shirikisho, ambayo nguvu zake zitagawiwa baina ya serikali za mataifa washiriki kwa mujibu wa matakwa ya waanzilishi na vizazi vijavyo.
Sisi viongozi wa nchi za afrika mashariki tunajifunga kisiasa kuwa na shirikisho la afrika mashariki. Mkutano wetu wa leo unaongozwa na hamu ya kuunganisha bara la afrika na sio ubinafsi wa maslahi ya maeneo yetu. Leo ni siku ya vitendo katika kuelekea katika maadili tunayoyaamini na umoja na uhuru ambao sote tumeupatia mateso na kujitolea mhaga kwa ajili hiyo.
Ingawaje Zanzibar haikuwasilishwa katika mkutano huu inatulazimu tuseme wazi kuwa nayo inakaribishwa kujiunga na mkutano huu wenye kulenga shirikisho. Mara tu baada ya zanzibar kumaliza taratibu zake za uchaguzi serikali yake itashirikishwa katika kamati ya kufuatilia jambo hilo au kamati nyingine ile itakayoanzishwa katika kufikia hilo shirikisho.
Nina wasiwasi kuwa Profesa alikuwa akiitizama Katiba ya 1977 katika mtazamo wa kishirikisho ambapo ungeweza kuwa na serikali tatu tofauti. Nina uhakika waliotunga katiba ya jamhuri ya muungano(1977) hawakuwa na mawazo hayo vichwani mwao.
Kuna ndani ya mipaka ya eneo la kila jimbo, serikali mbili ambazo zinafungwa katika utendaji wao, lakini kila moja ikiwa huru kutoka nyingine na zenye sauti ya mwisho katika mamlaka ilizo hodhi. Kila moja ina idara zake, sheria zake pekee, na kila moja ikiwa na mahakama zake yenyewe za kukazia sheria hizo. Hakuna serikali inayoweza kuingia katika eneo la mamlaka ya nyingine wala kuamuru uingiliaji wa watendaji wake wa sheria katika matendo ya mwingine.
Inaendelea kutoka bandiko #3
Suala lingine muhimu pia nia kwamba, licha ya Tanzania kuwepo kama taifa kwa miaka 50, taifa hili has never been consistent sio tu na matakwa ya wananchi bali pia juu ya nini taifa hili linataka kuwafanyia wananchi. Kwa mfano:
*Mwaka 1961-1966 - Tanzania was a "party state". Lengo kuu katika kipindi hiki lilikuwa to create and sustain a new order kufuatia uhuru. Viongozi wetu wakiongozwa na Nyerere hawakuwa na uzoefu na masuala ya madaraka, hivyo it became prudent to secure their own position at the helm of the state.
Mwaka 1967-1985- Tanzania ikageuka kuwa "developmental state". Lengo kuu katika kipindi hiki likawa kwamba kuleketea wananchi matunda ya uhuru kwani viongozi muda sio mrefu wakabaini kwamba walihitajika kuonyesha uwezo wa kuendeleza nchi zao kiuchumi, na matokeo yake yawe katika maendeleo ya kijamii - maji elimu afya n.k.
Mwaka 1986 - hadi leo (2014), our state has shifted from that of being developmental to "CONTRACTING STATE". Tofauti na kipindi cha nyuma, serikali ikapoteza umiliki wa dira yake ya taifa na sera kwa ujumla na kuzihamishia kwa mataifa makubwa kupitia mashirika ya kimataifa ya fedha - IMF na World Bank. Since then, serikali imekuwa ikiimbia ubeti wa uliberali na kuchezeshwa na wakubwa hawa wa nje. In the process, the state has been contracting in terms of kuwahudumia wananchi tofauti na ilivyokuwa huko nyuma. Wananchi hawakuandaliwa kuingia kwenye soko huria na serikali ikaamua kuwaingiza kwenye mfumo huo kiholela. Serikali kupitia chama baadae ikalifuta azimio la arusha kimya kimya mwaka 1992, na tangia wakati huo, wananchi walio wengi wamekuwa wanaishi maisha ya kuokoteza okoteza. Wataganyika ambao ndio wengi katika muungano huu ambao sasa umebakia kuwa ni ushirikiano baada ya ule ulioasisiwa na Nyerere na Karume kuvunjwa na Katiba ya Zanzibar (2010), badala ya viongozi kuwaokoa watanganyika na kusema sasa basi, imetosha, na nyie mnahitaji Tanganyika yenu ambayo mtakuwa na fursa ya kujipangia mambo yepi yawe yenu na yepi yawe ya pamoja, viongozi hawa wameamua mchana kweupe kuwadhulumu wananchi wa Tanganyika haki yao, haki waliyojichagulia kupitia tume ya katiba - autonomy, self determination, hence fostering of democracy.
CCM inasahau kwamba wananchi hawajakataa muungano bali wamekataa mfumo wa muungano ambao, kwanza haujawaletea neema yoyote wananchi wa pande zote mbili zaidi ya madaraka kwa kada ya watu fulani, lakini muhimu zaidi, muungano unaotetewa na ccm leo ni wa "nchi mbili, serikali mbili". Huo sio muungano aliotuachia Nyerere, ndio maana tutaupinga kwa kila namna.
CCM inasahau kwamba wananchi hulinda yale tu wanayoshirikishwa kuyatengeneza, na katika hili, suala la mfumo wa muungano linalopiganiwa na ccm will not be the creation of the peole bali CCM. Kwahiyo watakaoulinda muungano huu tena kwa gharama za wananchi (kodi) na pengine kwa gharama zitakazoathiri maisha ya wananchi iwapo mabomu yatatumika kuulinda mfumo wa aina hii, hao watakuwa ni CCM, na watabeba lawama zote.
Mwalimu Nyerere kupitia gazeti la Observer la uingereza, toleo la tarehe 20 Aprili alinena hivi:
Miaka 46 baada ya maneno haya ya Mwalimu, leo umma unatishiwa mabomu na vifaru. Na sio kwamba kwasababu hawautaki muungano, bali kwa sababu (1) Mfumo wa serikali mbili umeleta hasara kuliko faida kwa miaka 50 (2) Muungano wa Mwalimu na Karume haupo tena, umevunjwa na zanzibar 2010. Kwahiyo wananchi wanataka mapungufu yafanyiwe kazi ili kuboresha na kudumisha muungano kwani serikali mbili zinazidi kuudhoofisha, na serikali moja ni jambo lisilowezekana. Halikuwezekana miaka 50 iliyopita ambapo Mwalimu mwenyewe alipinga, sembuse leo wakati the union question has always remained to be the Zanzibar Question?
Kwa vile suala la Tanganyika lilikataa kukaa chii ya zulia baada ya sakata la jumbe 1984, tukio jingine muhimu la kihistoria katika harakati za kuizindua Tangayika lilikuwa 1993 kupitia sakata la G55. Katika hili pia, Mwalimu alitetea mfumo uliopo kwa hoja, lakini muhimu zaidi, akiwa anapinga kukiukwa kwa katiba ya muungano uliotambua Tanzania kama nchi moja. Leo utetezi wa muungano katika mazingira ya nchi mbili serikali mbili unajengwa kwa misingi gani ya hoja?
Tutambue kwamba kutokana na mapungufu yaliyopo pamoja na uchakachuaji wa historia yetu watanganyika, sio tu kwamba tunaweza anza upya kwa manufaa ya vizazi vyetu vikavyo, bali tuna haja ya kuanza upya na kulipatia taifa letu la Tanganyika Dira na Self Determination. Hivyo ndivyo majirani wetu wataweza tuamini katika muktadha wa shirikisho la Afrika Mashariki ambalo Mwalimu katika kikao cha OAU, Julai 1964 jijini Cairo alisema (yameukuliwa pia kwenye kitabu cha Mwalimu cha "Uhuru na Umoja", 1966, Ukurasa 300-304:
CCM, huu ndio wosia wa Mwalimu katika nyakati za leo. Msikilizeni kama mna ia ya kuokoa muungano wetu. CCM imeachia Zanzibar ivunje katiba ya muungano kupitia katiba ya zanzibar ya 2010. Katika hili, Mwalimu kupitia hotuba zake ambazo zimejaa "youtube" anasema kwamba:
"Iwapo watangayika watavunja muungano kwa hoja ya sisi watanganyika na wao wazanzibari, wataganyika hawatabaki salama.
Lakini iwapo wazanzibari watavunja muungano kwa hoja za sisi wazanzibari, na wao watangayika, wao hawatabaki salama bali watanganyika watabak salama"
Wazanzibari wamevuja muungano tayari kwani tofauti na katiba ya JMT (2010), Tanzania ni nchi mbili. Lakini walichofanya zanziba ni hatua muhimu kwao kuelekea mamlaka kamili na ya kweli ndani ya muungano kwani hayawezi patikana bila ya kuzinduliwa kwa Taganyika. CCM ina fursa ya kuokoa muungano na pia wazanzibari kwa kuizindua Tanganyika, vinginevyo bila ya kuizindua Tanganyika, wazanzibari hatimaye watauvunja muungano kwa hoja ya sisi wazanzibari, na wao watanganyika. Na katika hili, Mwalimu alituhakikishia kwamba watanganyika tutabaki salama. Swali linalofuatia ni je, lengo la ccm ni kuizuia Tanganyika ili zanzibar hatimaye ivunje kabisa muungano kisha sisi watanganyik tuishie kushuhudia ndugu na majirani zetu wakimalizana sababu tu sisi tutakuwa salama kama Tanganyika? Sidhani kama hii ndio njia ambayo CCM ndio inapendelea Tanganyika irudi, kama itarudi. Tukifika huko, ccm ijue tu ingeweza epusha maafa yote.
Wananchi wenzangu, TANGANYIKA ndio ASILI YAKO, Usidanganyike na muungano wa Kisiasa fraught with Legal Manipulation and Political Expediency. Tukiendelea kuendekeza haya, ni hatua ya kutojali well being ya vizazi vyetu vijavyo.
Nguruvi3, tunaomba somo lako kuhusu hoja ya Waziri Mku Pinda na Tanganyika.
Itaendelea kwa utaratibu ulioanishwa bandiko #1 .
TANZANIA KWANZA, TANGANYIKA KABLA.
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
UTAMBULISHO WA ZNZ
Pinda anataka znz ipate utambulisho. Akiwa mwanasheria kitaaluma ameshindwa kutambua mkataba wa muungano ulikuwa baina ya nchi ngapi na nini kilitokea akiwa ofisi ya rais kwa matukio tuliyoyaorodhesha hapo juu.
Katiba ya 2010 ambayo iliiyoondoa znz katika JMT kimantiki imeipa znz uwezo wa kutambulika kama nchi kwa jina, bendera, wimbo wa taifa, Rais, BLW, vikosi vya ulinzi na usalama.
Hayo yametokea machoni mwa Pinda akiwa waziri mkuu, mshauri mkuu wa pili wa Rais wa JMT.
Pinda hakumbuki yeye kama waziri mkuu hana uwezo wa kuzungumza na masheha katika shehia yoyote kule znz kwa capacity ya waziri mkuu.
Uwaziri mkuu wake unaishia bara kwasababu ZNZ ina uongozi kamili na yeye hana lake hata kwa bahati mbaya. Ni kutokana na hilo hana utambulisho znz na ni kitu cha ajabu anapodai znz ipewe utambulisho.
Znz inao utambulisho,kilichokosekana ni mshirika wa znz katika JMT ambaye ni Tanganyika.
Katika mazingira ya kwaida Pinda alipaswa kulia kuliko kuitafutia znz utambulisho.
Angeangua kilio kwasababu ile nchi aliyozaliwa Tanganyika imetoweka katika mazingira tatanishi.
Pinda hana kumbu kumbu za uwepo wa Tanganyika kama alivyosema.
Katika hali isiyo ya kawaida, mapendekezo ya Pinda kule Dodoma kama waziri mkuu lazima yaende baraza la wawakilishi znz kupewa baraka zote.
Endapo Pinda anapendekeza ujenzi wa vyoo vya shule basi kama waziri mkuu lazima apate ridhaa ya BLW znz kama ilivyo katika katiba ya znz iliyofanyiwa marekebisho 2010.
Ni kwa muktadha huo, Pinda anaitambua znz zaidi kuliko sisi wa mitaani kwasababu hawezi kutekeleza majukumu yake hadi pale Pandu Kificho na wenzake 50 wanaoitwa BLW watakapokubali.
Kinachomsumbua mzee Kayanza ni usahaulifu wa historia pengine kutokana na majukumu mengi ya kazi au tatizo la kibinadamu la kumbu kumbu hafifu.
WATANGAYIKA KUNYIMWA ARDHI
Hili Pinda analiona dogo sana lakini kwa wananchi wa nchi moja ni kubwa.
Nguvu ya soko huamuliwa na soko lenyewe.
Itakuwa ni kituko mtu kwenda kununua ardhi ya sh milioni 50 kwa ekari moja kuliko kununua mashamba Tanganyika.Hata hivyo katika misingi ya utaifa znz haipaswi kuweka vikwazo hivyo.
Hii maana yake ipo siku Kilimanjaro nao watasema hivyo na Pinda takubaliana nao.
Sheria ya ardhi iimemlenga Mtanganyika kwasababu Mkenya na mtaliano au Mwarabu hawaguswi na sheria hiyo.Ni ubaguzi huu ndio unapelekea Watanganyika kujiuliza kama sisi ni taifa.
Ubaguzi wa ardhi ni sehemu tu ya ubaguzi unaoendelea visiwani ukiwalenga Watanganyika na si raia wa eneo lingine.
Katika nchi moja znz haitambui leseni ya Tanzania bara,na kazi ni kwa kibali achilia mbali ukazi.
Kama waziri mkuu Pinda alipaswa kuliangalia hili tatizo kwa upana wake zaidi hasa katika ubaguzi na wala si kwa mtazamo hafifu finyu na potofu alioutoa.
TANGAZO LA SERIKALI Na. 246 lililochapwa 1/5/1966.
SHERIA ZA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR, 1964.
AMRI
Kwa mujibu wa vifungu 3(b) na 8 Vya Sheria Zilizotajwa
AMRI YA UTARATIBU WA KIPINDI CHA MPITO, 1964.
1. Amri hii itajulikana kama amri ya utaratibu wa kipindi cha mpito 1964, na itaanza kutumika siku ya muungano.
2. Amri hii itasomwa kama sehemu ya katiba ya muda.
....
....
....
9. Mali na Mikataba:
Mali zote na haki juu ya mali za jamhuri ya Tanganyika na mali zote na haki juu ya mali za jamhuri ya watu wa zanziba zilizokuwa zinamilikiwa au kutumiwa au zilizomilikiwa au kutumiwa kimsingi kuhusiana na mambo ya muungano, zitakuwa kuanzia siku ya muungano chini ya jamhuri ya muungano.
Barubaru,
Nadhani hoja ya msingi ya Nguruvi3 ni kwamba - Waziri Mkuu anajulikana kikatiba kama waziri mkuu wa jamhuri ya muungano, lakini in practice hana mamlaka yoyote kwenye upande wa pili wa muungano, hivyo hana moral authority ya kutetea jambo ambalo hana mamlaka nayo.
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Karume, however had no time for legal arrangements. He continued to exercise power in complete disregard on union matters. Karume declared that they would not be elections in Zanzibar for the next 50 Years. Nyerere was exasperated but he could do little without pushing Karume out of the union. Meanwhile, his legal craftsmen amended the constitution to postpone the constitutional commission and the constituent assembly indefinitely. The union was governed by the interim constitution of 1965 for the next 12 years.
Hatukutaka tudhaniwe hata kwa makosa kwamba tulianzisha ubeberu mpya, kwahiyo mimi nilipanga mfumo wa serikali mbili.
Ni vizui kuelezea shabaha ilikuwa kuziunganisha nchi za Afrika mashariki ziwe nchi moja; wakati Zanzibar na Tanganyika zinaungana, Kenya, Uganda na Tanganyika zilikuwa katika mazungumzo ya kutafuta uwezekano wa kuungana.
Kama jambo hilo lingetokea, mfumo wa nchi mpya ambayo ingezaliwa ungekuwa ni wa shirikisho, ama shiikisho la nchi tatu zenye serikali nne, au shirikisho la nchi nne zenye serikali tano.
Nani anaweza kusema katika mazingira ya sasa kunaweza kuundwa afrika moja? Kama hakuna, hofu ya kuundwa serikali ya Tanganyika ipo wapi?
Kama jambo hilo lingetokea, mfumo wa nchi mpya ambayo ingezaliwa ungekuwa ni wa shirikisho, ama shirikisho la nchi tatu zenye serikali nne, au shirikisho la nchi nne zenye serikali tano.