Tanzania kutangaza hali ya hatari!?

Habari wanajamvi.

Katika pitapita zangu nimekutana na hili tangazo kutoka Jeshi la Ulinzi na Usalama Tanzania (TPDF) na limeniacha na maswali kadhaa. Naombeni mwenye fikira kama zangu aungane name au mwenye fikira tofauti atupe mwanga wa ni nini kinahusiana na tangazo hili.
1. Je yewezekana jeshi la polisi limeshindwa kazi?
2. Je, nchi inaweza kuingia katika hali ya hatari wakati wowote kuanzia sasa?
3. Je, yawezekana utawala wa demokrasia Tanzania umeshindwa?
4. Au tutegemea nini kama nchi!!

Kwa heshima na taadhima nawasilisha
attachment.php
JW walishaona hali inazidi kuwa tete!! EL mwaka huu atawatoa jasho CCM pamoja na serikali yao.
na mimi naona kama kuna ujumbe uliokusudiwa bali tangazo la saba saba limetumika tu.
Najuaribu kuiangalia hiyo rangi nyekundu iliyotumika kama alert kwa msomaji.
Lakini ni kwa nini kama kweli wana nia nzuri wasiingilie masuala yanayoisumbua nchi kama ufisadi!? Au ndio wameanza na wale maofisa wa SUMA JKT waliopelekwa mahakamani juzi juzi!?
 
Tanzania bila shaka tuna majeshi matano kwa sasa(kama sipo sahihi unaweza nisahihisha).

Jeshi la Wananchi - lipo ili kulinda mipaka ya nchi na usalama wa Taifa kwa ujumla n.k.
Jeshi la Polisi - kulinda raia ndani ya mipaka ya nchi n.k.

Inapotokea vurugu kubwa ambayo inaweza kuhatarisha amani ya nchi au usalama wa Amri Jeshi mkuu, moja kwa moja JWTZ wanaingia kazini pasipo mjadala wowote na hicho ndio kinachomaanishwa katika hilo tangazo lao.

Hizi kweli ndizo kazi za hayo majeshi uliyotaja hapa.

Lakini suala la mgomo na vurugu ni vitu viwili tofauti. Hapa wamemaanisha migomo kama ya Madakitari, Walimu, Ma-House Girl / Boys,

Sasa hizi si kazi zao kuna Jeshi la Polisi linapaswa kuwajibika endapo kama hali itatishia Usalama wa Nchi ndipo JWTZ wanaingilia kati kwani wao hapo ndio wanaoruhusiwa kutumia Silaha ya Moto. Lakini tumeshuhudia Polisi wakitumia Silaha za moto sehemu ambapo walitakiwa kutumia virungu.

JESHI LA POLISI ni DHAIFU KAMA .............



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Loading ....... mada zingine zakupotosha tangazo linahusu 77 sasa linahusiana vipi na hali ya hatari great thinker ?
 
Back
Top Bottom