Tanzania kupata mkopo wa USD 250Million kutoka mabenki ya ndani na nnje ya Nchi

godbiy

Member
Nov 9, 2010
14
16
Hivi punde imethibitishwa kuwa Serikali ya JK itapokea mkopo wa kiasi cha USD 250Million kutoka kwa mabenki ya ndani na nnje ya nchi.

Stanbic ndiyo inaonekana kuwa "Lead Arranger" wa mkopo huu,ingawa mabenki mengine ya ndani hayajatajwa bado.
Maswali ambayo inabidi tujiulize ni kama yafuatayo
a)Kwa nini serikali iamue kukopa kutoka mfumo tofauti na ule wa kawaida wa ukopaji.i.e Kupitia T-bills,IMF,world bank etc
b)Je hatua hii haiwezi kusababisha 'Liqudity crisis" kwa soko la fedha la ndani ya nchi.kiuchumi, baadhi ya mabenki ndani ya nchi yanaweza kushindwa kuwapa mikopo wafanyabiashara wa ndani kutokana na kiasi kikubwa kuwa kimechukuliwa na serikali na hivyo "interest rates' zaweza kupanda kwani soko la fedha litakuwa linapiganiwa na wakopaji wa kawaida na serikali.

Mwenye habari zaidi kuhusu huu mkopo tunaomba atujuze hasa hasa ni benki zipi ambazo zitatoa hizi fedha,ni miaka mingapi na mengineyo
 
serikali iliwahi kukopa toka stanbic kama sikosei mwaka jana mwanzoni!!ila tumemsikia mkulo mwenyewe akikiri kuwa hii ni bongo,hivyo kuna watu serikalini wanamzidi ujanja wanazitafuna pesa za mikopo!!
 
Back
Top Bottom