Tanzania kuipa Comoro Msaada wa Ndege

kwa mara ya kwanza nimesikia maiti ikiombwa t
damu
 
Ha ha haa..... Nilivyosoma "heading" nilifikiri ni msaada wa ndege kama "quelea quelea" labda walihitajika kutibu janga flani hivi linalohusiana na mazingira/mabadiliko ya tabia nchi.
 
TZ bana! Eti waziri wa uchukuzi sikui nani nani yule.. ameshatoa agizo kwa tcaa iangalie jinsi ya kusaiodia!!! My foot...

Na Comorro bana yaani wakaona nchi ya kuwasaidia ni TZ... Ama kweli acheni vipofu wavutane wenyewe...
 
Wakati Ethiopia wana 787 dream liner 4 na 52 mchanganyiko wa air bus na boeing za kutosha,,sisi tunakuna Nazi tuu, Ndege zinataka usimamizi wa hali ya juu sana,nadhani hata tungekua na Ndege zipo baadhi ya Nchi zingepigwa ban kwa sababu ya UNGA maana wangeficha hadi ktk engine kama watanzania tuu ndio wanameza iyo ingekua rahisi tuu.
 
He he hii lazima ucheke Tanzania kwa kipindi kile isinge weza kumshauri yeyote juu ya masuala ya ndege
 
Ni miujiza lakini kweli kipofu kumuomba msaada kiwete!
 
Achana na kuwasaidia ndege; hata wangeomba tuanzishe safari za ndege kwenda kwao uwezo huo hatuna...!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…