Tanzania Katika Miaka Mitano Ijayo: Inatisha

Tanzania Katika Miaka Mitano Ijayo: Inatisha

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,820
Reaction score
24,472
Nina wasiwasi sana na hali ya Tanzania kiuchumi na kisiasa katika kipindi cha miaka mitano ijayo kwa sababu kadhaa:

(1) wafadhili hawatahudumia bajeti ya serikali kama ilivyozoeleka kwa sababu ya utawala mbovu, na ukweli kuwa EU wameshajua kuwa serikali iliyopo madarakani imeingia kimabavu. EU wakisitisha misaada yao tu, basi tutasahau na misaada ya USA, Australia na Japan. Huenda tukabakiwa ni misaada kutoka China na Canada tu. Sina uhakika kama China iliwahi kutoa msaada wa kulipia bajeti ya serikali. Msaada wa Kanada kwenye bajeti ya serikali huwa ni mdogo sana. Serikali inaweza kulazimika kufanya mambo kadhaa: kupunguza wafanya kazi wake, na hivyo kuongeza unemployment rate, kuchapisha hela nyingi za madafu, na hivyo kuongeza inflation, au kujisahau na kutelekeza majukumu yake huku nchi ikibaki haina usimamizi.

(2) Kikwete atakuwa bize sana kujijenga yeye na familia yake kwa vile uraisi wake ni swala la familia yake. Kwa sasa hivi kikwete hahitaji kura zetu tena, na hata akivurunda vipi, hilo yeye halimhusu tena. Kwa mazingira hayo, rushwa itashamiri sana kipindi hiki, na hivyo madhara yote ya rushwa yatang'aa sana na kufanya maisha yawe magumu zaidi.

(3) Ndani ya CCM kutakuwa na msigishano mkubwa sana baina ya watu wanaotaka kumrithi Kikwete pale Magogoni: watu kama Lowassa, Nchimbi, Mwandosya, Membe, Magufuli, Sita, Mwakyembe, na wengineo watakwaruzana sana kupitia bunge na kulifanya bunge lisiendeshe majukumu yake ipasavyo hasa ukizingatia kuwa halina uongozi thabiti.

(4) Kutokana na hayo yote, kutakuwa na malalamiko sana kutoka kwa wananchi wa kawaida ambayo yatatiwa chumvi zaidi na wagombeaji wa CCM ili kila upande ujipatie wafuasi wengi. Malalamiko hayo ya wananchi yataendana na maandamano na migomo ya mara kwa mara ambayo itaweza kuleta vurugu nchini na kusababisha watu wengi sana wapoteze maisha hasa kwa vile polisi wetu wanapenda sana kukamua trigger huku wakielekeza mitutu yao kwa raia.

(5)Kutaibuka mtengano wa wazi baina aya makundi mbalimbali ya jamii, ambayo yatapandikizwa na wanasiasa wa CCM kuwania uraisi wa mwaka 2015.


Yote hayo hapo juu yanatisha sana ila tujiandae kukabiliana nayo.
 
Hiyo miaka 5 mbali, yatunisia na egypt ndo solution. Bila hivyo, tutafika huko kweli tena kwa aibu zote.
 
Bajeti ya kutegemea ufadhili kwa nguvu sasa inatuadhiri ile mbaya!
 
Lakini JK alidai wakati wa kampeni kuwa wafadhili wameahidi misaada zaidi tukimchagua.:A S 20:

Labda ataongeza safari za nje kutafuta misaada zaidi! Cha ajabu sehemu nyingi ameshakwenda maradufu mpaka sasa anaona aibu kurudia tena.
Kwa hiyo nchii bila misaada ya wafadhili na the so called wenza kati maendeleo itadhalilika?!
 
Nina wasiwasi sana na hali ya Tanzania kiuchumi na kisiasa katika kipindi cha miaka mitano ijayo kwa sababu kadhaa:

(1) wafadhili hawatahudumia bajeti ya serikali kama ilivyozoeleka kwa sababu ya utawala mbovu, na ukweli kuwa EU wameshajua kuwa serikali iliyopo madarakani imeingia kimabavu. EU wakisitisha misaada yao tu, basi tutasahau na misaada ya USA, Australia na Japan. Huenda tukabakiwa ni misaada kutoka China na Canada tu. Sina uhakika kama China iliwahi kutoa msaada wa kulipia bajeti ya serikali. Msaada wa Kanada kwenye bajeti ya serikali huwa ni mdogo sana. Serikali inaweza kulazimika kufanya mambo kadhaa: kupunguza wafanya kazi wake, na hivyo kuongeza unemployment rate, kuchapisha hela nyingi za madafu, na hivyo kuongeza inflation, au kujisahau na kutelekeza majukumu yake huku nchi ikibaki haina usimamizi.

(2) Kikwete atakuwa bize sana kujijenga yeye na familia yake kwa vile uraisi wake ni swala la familia yake. Kwa sasa hivi kikwete hahitaji kura zetu tena, na hata akivurunda vipi, hilo yeye halimhusu tena. Kwa mazingira hayo, rushwa itashamiri sana kipindi hiki, na hivyo madhara yote ya rushwa yatang'aa sana na kufanya maisha yawe magumu zaidi.

(3) Ndani ya CCM kutakuwa na msigishano mkubwa sana baina ya watu wanaotaka kumrithi Kikwete pale Magogoni: watu kama Lowassa, Nchimbi, Mwandosya, Membe, Magufuli, Sita, Mwakyembe, na wengineo watakwaruzana sana kupitia bunge na kulifanya bunge lisiendeshe majukumu yake ipasavyo hasa ukizingatia kuwa halina uongozi thabiti.

(4) Kutokana na hayo yote, kutakuwa na malalamiko sana kutoka kwa wananchi wa kawaida ambayo yatatiwa chumvi zaidi na wagombeaji wa CCM ili kila upande ujipatie wafuasi wengi. Malalamiko hayo ya wananchi yataendana na maandamano na migomo ya mara kwa mara ambayo itaweza kuleta vurugu nchini na kusababisha watu wengi sana wapoteze maisha hasa kwa vile polisi wetu wanapenda sana kukamua trigger huku wakielekeza mitutu yao kwa raia.

(5)Kutaibuka mtengano wa wazi baina aya makundi mbalimbali ya jamii, ambayo yatapandikizwa na wanasiasa wa CCM kuwania uraisi wa mwaka 2015.


Yote hayo hapo juu yanatisha sana ila tujiandae kukabiliana nayo.

Kichuguu,
Sasa hivi kumezuka fisi ambaye anangojea mkono uanguke audake. Serikali ya CCM hawana njia yoyote ile kumkwepa huyu fisi. Lazima tuliwe safari hii. Kuna safari nyingi mno za mawaziri zimefuliza kwenda China, na huko kote waaambiwa kuwa pesa zipo, lakini kitu kimoja tu! Si mna dhahabu, gesi, Copper,etc etc basi tupeni hizo resources na sisi tutawajengea mnachotaka.

Hapo ndipo kichwa kinawauma serikali ya CCM, je wafanyeje? infact China can enroll CCM in its lifetime, but headche is how to tell the people that they exchanged this country resources with such investments? Hawa CCM ni Mafisadi, lakini vile vile wana kale ka-uzalendo kwa nchi yao kama mtutu yeyote----conflict-- of interest?
ATC privatization negotiation kwa wachina ndipo hapo ilipoanguka, maana walidai wapewe resources kama gaurantee ya hiyo investment. Yaani wapewe shirika, market na vilevile resources!!
 
Back
Top Bottom