Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 17,820
- 24,472
Nina wasiwasi sana na hali ya Tanzania kiuchumi na kisiasa katika kipindi cha miaka mitano ijayo kwa sababu kadhaa:
(1) wafadhili hawatahudumia bajeti ya serikali kama ilivyozoeleka kwa sababu ya utawala mbovu, na ukweli kuwa EU wameshajua kuwa serikali iliyopo madarakani imeingia kimabavu. EU wakisitisha misaada yao tu, basi tutasahau na misaada ya USA, Australia na Japan. Huenda tukabakiwa ni misaada kutoka China na Canada tu. Sina uhakika kama China iliwahi kutoa msaada wa kulipia bajeti ya serikali. Msaada wa Kanada kwenye bajeti ya serikali huwa ni mdogo sana. Serikali inaweza kulazimika kufanya mambo kadhaa: kupunguza wafanya kazi wake, na hivyo kuongeza unemployment rate, kuchapisha hela nyingi za madafu, na hivyo kuongeza inflation, au kujisahau na kutelekeza majukumu yake huku nchi ikibaki haina usimamizi.
(2) Kikwete atakuwa bize sana kujijenga yeye na familia yake kwa vile uraisi wake ni swala la familia yake. Kwa sasa hivi kikwete hahitaji kura zetu tena, na hata akivurunda vipi, hilo yeye halimhusu tena. Kwa mazingira hayo, rushwa itashamiri sana kipindi hiki, na hivyo madhara yote ya rushwa yatang'aa sana na kufanya maisha yawe magumu zaidi.
(3) Ndani ya CCM kutakuwa na msigishano mkubwa sana baina ya watu wanaotaka kumrithi Kikwete pale Magogoni: watu kama Lowassa, Nchimbi, Mwandosya, Membe, Magufuli, Sita, Mwakyembe, na wengineo watakwaruzana sana kupitia bunge na kulifanya bunge lisiendeshe majukumu yake ipasavyo hasa ukizingatia kuwa halina uongozi thabiti.
(4) Kutokana na hayo yote, kutakuwa na malalamiko sana kutoka kwa wananchi wa kawaida ambayo yatatiwa chumvi zaidi na wagombeaji wa CCM ili kila upande ujipatie wafuasi wengi. Malalamiko hayo ya wananchi yataendana na maandamano na migomo ya mara kwa mara ambayo itaweza kuleta vurugu nchini na kusababisha watu wengi sana wapoteze maisha hasa kwa vile polisi wetu wanapenda sana kukamua trigger huku wakielekeza mitutu yao kwa raia.
(5)Kutaibuka mtengano wa wazi baina aya makundi mbalimbali ya jamii, ambayo yatapandikizwa na wanasiasa wa CCM kuwania uraisi wa mwaka 2015.
Yote hayo hapo juu yanatisha sana ila tujiandae kukabiliana nayo.
(1) wafadhili hawatahudumia bajeti ya serikali kama ilivyozoeleka kwa sababu ya utawala mbovu, na ukweli kuwa EU wameshajua kuwa serikali iliyopo madarakani imeingia kimabavu. EU wakisitisha misaada yao tu, basi tutasahau na misaada ya USA, Australia na Japan. Huenda tukabakiwa ni misaada kutoka China na Canada tu. Sina uhakika kama China iliwahi kutoa msaada wa kulipia bajeti ya serikali. Msaada wa Kanada kwenye bajeti ya serikali huwa ni mdogo sana. Serikali inaweza kulazimika kufanya mambo kadhaa: kupunguza wafanya kazi wake, na hivyo kuongeza unemployment rate, kuchapisha hela nyingi za madafu, na hivyo kuongeza inflation, au kujisahau na kutelekeza majukumu yake huku nchi ikibaki haina usimamizi.
(2) Kikwete atakuwa bize sana kujijenga yeye na familia yake kwa vile uraisi wake ni swala la familia yake. Kwa sasa hivi kikwete hahitaji kura zetu tena, na hata akivurunda vipi, hilo yeye halimhusu tena. Kwa mazingira hayo, rushwa itashamiri sana kipindi hiki, na hivyo madhara yote ya rushwa yatang'aa sana na kufanya maisha yawe magumu zaidi.
(3) Ndani ya CCM kutakuwa na msigishano mkubwa sana baina ya watu wanaotaka kumrithi Kikwete pale Magogoni: watu kama Lowassa, Nchimbi, Mwandosya, Membe, Magufuli, Sita, Mwakyembe, na wengineo watakwaruzana sana kupitia bunge na kulifanya bunge lisiendeshe majukumu yake ipasavyo hasa ukizingatia kuwa halina uongozi thabiti.
(4) Kutokana na hayo yote, kutakuwa na malalamiko sana kutoka kwa wananchi wa kawaida ambayo yatatiwa chumvi zaidi na wagombeaji wa CCM ili kila upande ujipatie wafuasi wengi. Malalamiko hayo ya wananchi yataendana na maandamano na migomo ya mara kwa mara ambayo itaweza kuleta vurugu nchini na kusababisha watu wengi sana wapoteze maisha hasa kwa vile polisi wetu wanapenda sana kukamua trigger huku wakielekeza mitutu yao kwa raia.
(5)Kutaibuka mtengano wa wazi baina aya makundi mbalimbali ya jamii, ambayo yatapandikizwa na wanasiasa wa CCM kuwania uraisi wa mwaka 2015.
Yote hayo hapo juu yanatisha sana ila tujiandae kukabiliana nayo.