Tanzania Internet Service Providers: Packages

Status
Not open for further replies.
mmmhh, i must agree, i never knew conns could go that cheap couse i never cared.
anyway i just decided to get myself a zain's line and see what happens on its internet connection, *** i've been having voda on my bb8800 but the speed is not too good due to more emails and more updates i get from my cell ***

After that i'll probably start paying more attention on my home and office connections.

cheers
 
Nitainunua this week, tuonane basi mkuu mbona kimya sana wewe?

Halafu kama ni $42 kwa 2GB basi hao ndio watakuwa Cheapest ISP in Tanzania kwa sasa mkuu....

Hehehe poa mkuu vp leo?
Kama ukipata chance nishtue nitakuja hata kitaa.
 
I have just rated this thread as EXCELLENT!! You can do the same.


Kuna Zantel:
Hawa nimekuwa nao kwa muda sasa na mimi ni Postpaid Customer wao, hawa nao nalipia bundle ya 10GB kwa mwezi. Nimekuwa nikitumia service yao kwa zaidi ya miezi 6 sasa na naweza kusema pamoja na kuwa nilishakumbana na matatizo nao lakini mara zote wametoa ushirikiano wa karibu. Hawa download speed yao ni nzuri na kuna wakati inafikia 250kb/s. Kwa bundle hii ya 10GB, nanunua 1MB kwa Tshs 26/= na inakuwa ina VAT ndani yake. Haya matangazo wanayoweka barabarani na kudai wana UNLIMITED Internet service ni lugha ya kibiashara ambayo inamaanisha 2BG kwa 90,000/= wakiwa wamewa-target normal users. Kwa mtu kama mimi ambaye per month najikuta nina zaidi ya 20GB siwezi kukubaliwa kuwa na hiyo ya Tshs 90,000/= per month. Hawa ukikumbana na tatizo na service zao naweza hata kukusaidia endapo utakosa msaada wa haraka kwani modem zao nimezitumia karibia zote na kuna device ambayo ukiichukua kwao hata kama una PC 20 ofisini kwako bado unaweza kutumia modem moja kwa PC zote.
TCRA wafanye kazi yao na kuacha kuzembea hali wananchi wanaongopewa kwenye mabango. Kama matangazo yao yanaongopa, waondoe hayo mabango barabarani. Na ikiwezekana wapatiwe faini pia.
 
Aisee tunangojea feedback ya CTV tujitume....what the feedback max?


Mara ya mwicho nilipotumia CTV ilikuwa wanapitisha waya kutoka kwao hadi kwenye computer yako, so inabidi uwe maeneo ya mjini. Speed slow, lakini ndo hivyo cheap. Hii ilikuwa miaka 2-3 iliyopita.
 
Mara ya mwicho nilipotumia CTV ilikuwa wanapitisha waya kutoka kwao hadi kwenye computer yako, so inabidi uwe maeneo ya mjini. Speed slow, lakini ndo hivyo cheap. Hii ilikuwa miaka 2-3 iliyopita.

Mkuu bado ipo huduma zao sio mbaya sana ni $42 kwa mwezi unapewa 2GB.
 
...heshima yenu wakuu wa jukwaa hili.

kati ya ISP wa Tanzania, (sijui TTCL, ZAIN, ZANTEL, VODA) kampuni gani inahuduma (nzuri zaidi) za mobile broadband? na vipi bei na upatikanaji wake bila kukwazika na urasimu wa kibongo bongo?.

au, mnanishauri kuchukua USB modems/internet dongles za kampuni gani hapa UK ambazo zitafanya kazi vizuri na hao ISP wa Tanzania?

Shukran.
 
mpaka sasa bado speed ni ya kuchechemea.....tuliaambiwa naa gharaama zzitashuka kwa more than 70%......labda waya zina relax kwanza coco beach.....
 
Mbu,

Labda wakwambie wengine. Mi kwa sasa sijui

...dah, ama kweli jana nilizidiwa na usingizi hii thread sikuiona tangu mwanzo wake. Shukran sana kwa darasa Max.

Kwa darasa ulilotoa, na muda ninaotegemea kukaa Tz, nitachukua bundle hiyo bundle ya ZANTEL. fingers crossed kusiwe na longolongo nyingi, nakereka sana na urasimu wa Kibongo, pesa unayo mkononi watu bado wanakuringia haki yako.

Shukran kwa wote mliotoa darasa kwenye thread hii.
 
Mkuu Max. hili darasa murua sana, asante sana. Hivi hizi simu wanazouza TCCL Huawei, unazionaje kwa matumizi ya binafsi ya nyumbani na uwapo safari within the country, maana wakati nikiwa TZ huwa natumia moja na kwa kweli wakati mwingine inafanya kazi vizuri sana na wakati inakuwa very slow, haswa maeneo fulani fulani inaelekea antenna zao siyo nzuri nje kidogo tu ya "city center"?.
Is there a better alternative? or means to improve the service? Maana kama ulivyosema huduma kwa wateja ni mbaya sana inaweza kukuchukua nusu siku kuwaelewesha tu kuwa una shida gani licha ya tatizo kutatuliwa.
Halafu niwapo nyumbani is there any means or possibility ya kuiwekea ss wireless point?
 
Internet Bundle za Vodacom
10MB=2,000/- 200.00Tsh/MB
20MB=3,700/- 185.00Tsh/MB
100MB=15,000/- 150.00Tsh/MB
250MB=25,000/- 100.00Tsh/MB
500MB=40,000/- 80.00Tsh/MB
1GB = 70,000/- 70.00Tsh/MB
2GB =95,000/- 47.50Tsh/MB
4GB = 190,000/- 47.50Tsh/MB
5GB =200,000/- 40.00Tsh/MB
10GB =360,000/- 36.00Tsh/MB
20GB =450,000/- 22.50Tsh/MB
50GB =1000,000/- 20.00Tsh/MB
Ukifuatilia kwa rates hizi za Vodacom utagundua kuwa kadri unavyochukua bundles kubwa zaidi ndipo na matumizi yake yanakuwa cheap kwa mfano anayechukua 50GB kwa sh. 1000,000/= ni sawa na sh. 20 tu kwa kila MB. Na hizi ni kwa miezi mitatu (3)

Mimi binafsi juzijuzi hapa nimeweka IGB kwa sh.70,000 kwa hiyo nakamuliwa 70sh/MB.

Halafu hawa Vodacom kuna modem yao inakuwa na speed kali sana na wakati mwingine inakuwa low speed. Lakini hata hivyo kama na-download file kubwa kuna wakati speed yake inafika 150Kbs/sec na wakati mwingine inakuwa ndogo sana hadi 5Kbs/sec. Lakini bado nawakubali japokuwa gharama zao bado zinaonekana kuwa kubwa.
 
Nothing UNLIMITED! Ni lugha za kibiashara mkuu.

Halafu kama una kampuni unajua unataka kuwa hustle free unaweza kununua 20GB ya TTCL kwa Tshs 450,000/= kwa mwezi na speed nakuhakikishia ni ya kueleweka. Tatizo ni kama nilivyosema awali, usi-deal na TTCL moja kwa moja, kama unaweza kupata mtaalam ambaye ni mwaminifu akakusaidia ku-deal nao basi inakurahisishia mambo na kukusahaulisha kero za internet.
Huyo dealer anachofanya yeye nini ambacho mimi mteja itaniwia vigumu kufanya? Tuchukulie nina Internet cafe yenye PC 6.
 
Ukifuatilia kwa rates hizi za Vodacom utagundua kuwa kadri unavyochukua bundles kubwa zaidi ndipo na matumizi yake yanakuwa cheap kwa mfano anayechukua 50GB kwa sh. 1000,000/= ni sawa na sh. 20 tu kwa kila MB. Na hizi ni kwa miezi mitatu (3)

Mimi binafsi juzijuzi hapa nimeweka IGB kwa sh.70,000 kwa hiyo nakamuliwa 70sh/MB.

Halafu hawa Vodacom kuna modem yao inakuwa na speed kali sana na wakati mwingine inakuwa low speed. Lakini hata hivyo kama na-download file kubwa kuna wakati speed yake inafika 150Kbs/sec na wakati mwingine inakuwa ndogo sana hadi 5Kbs/sec. Lakini bado nawakubali japokuwa gharama zao bado zinaonekana kuwa kubwa.
Yep! Gharama yao ni kubwa. Utaona wamejaribu kumechisha bei pamoja na volume usage ifanane na ya TTCL. Mtego upo kwenye speed; na hata ukiangalia kwenye advert yao, haikutajii speed (They don't want you to know).
TTCL wametaja speed. Imeelezwa kwamba wao pekee ndiyo wameconnect kwenye mkonga (fiber).

Wengine hawataridhika na hiyo speed ya Voda. Usisahau pia kwamba ukivuka hiyo limit iliyowekwa na Voda (mfano 1GB), gharama ya kila megabyte utakayo download inabadilika kutoka 70 kuwa 100/MB kwa kila MB utakayozidisha.
 
Hao wote wanotangaza UNLIMITED SPEED ni wango wakubwa kwani wao wakifanya uwe Unlimited utaweza Pull bandwidth yote ukasababisha wenzako internet kuwa Slow

Hizo Modem nadhani huwa wanaweka dedicated bandwidth kutokana na gharama unayolipia

Halafu huwa wengine wanatumia Device called Bandwidth Manager ambayo wana limit kwa gharama uliyo towa pia ndani yake kuna PIPE wanayokuweka so ikiwa 100% Max inaanza kuwa slow connection

Tuangalie na VSAT LINK inakuwaje pamoja inakuwa ni gharama kununua vifaa

Then nikweli huu usemi the bigger bandwidth you buy the faster speed you get
 
Wakuu hapa nimeondoka na mengi mema!
Kama kuna la zaidi tuzidi kupeana wanaJF.
 
Nimekuwa nikitumia TTCL broadband kwenye internet cafe yenye PC 12, huwa nanunua 20 GB kwa 450,000 na inanisuit vizuri. Sasa nataka kufungua branch nyingine sehemu ambayo TTCL hawana cable network yaani nyaya zao za landline hazijafika. Mkuu Melo unanishauri nitumie kampuni gani? Zantel itaweza kunisaidia? i'll appreciate ur help!!
 
Nimekubali
Lakini si nimesikia kuwa ule mkonga wa mawasiliano uliozinduliwa na Mzee,DK,Mh,JK tuliambia kuwa unaanzia afrika mashariki hadi ulaya na kuwa utapunguza tatizo la kusuasua kwa interenet na kupunguza gharama,hii ni kweli au siasa tu.
 
Nimekuwa nikitumia TTCL broadband kwenye internet cafe yenye PC 12, huwa nanunua 20 GB kwa 450,000 na inanisuit vizuri. Sasa nataka kufungua branch nyingine sehemu ambayo TTCL hawana cable network yaani nyaya zao za landline hazijafika. Mkuu Melo unanishauri nitumie kampuni gani? Zantel itaweza kunisaidia? i'll appreciate ur help!!
Kama bado upo Dar na nakumbuka tuliwahi kukutana then tunaweza kuwasiliana via email nami nikakuunganisha na mtu wa ndani Zantel akakupa device flani hivi ukaunganisha kwenye Router yako ili kuweza kuunganisha pc zaidi ya 1 (hata 12 inafanya kazi).

Aidha, hapa kwangu nina Wireless na nimejaribu 30m from home bado inakuwa detected. Device ni nzuri na inafanya kazi, wao hawajaitangaza nami walinipa ili niijaribu na kuwapa feedback. Inafanya kazi vizuri sana. Hutakuwa na haja ya kufunga nyaya kibao kwenye cafe yako, sanasana ni kufanya wireless connection ofisini kwako na ndani ya 3hrs service inakuwa ishaanza.

Gharama wameshusha... I have to contact them ili nikwambie bei ikoje kwa 20GB, that's my package na haifiki hata Tshs 450,000/=

Uzuri wa device ile ni kuwa hata hizi modem za VodaCom na SimbaNet inafanya kazi nazo...

Ahsante mkuu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom