Tanzania inauhitaji ushiriki wake AFCON kuliko hizi siasa za miaka ya sasa

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,488
13,610
Asitokee mtu akamdanganya mtanzania kwa namna yoyote ile, ushiriki wetu wa michuano ya mataifa huru Afrika ni muhimu kuliko siasa za kisasa za vyama vingi. Kuonekana kwetu katika michuano hii ya soka ambayo hukutanisha timu bora za mataifa ya afrika ni muhimu sasa pengine kuliko katika kipindi chochote nyuma.

Tulionekana mara ya mwisho tukishiriki AFCON mwaka 1980, miaka 39 iliyopita. Sio jana wala sio juzi, enzi hizo magari unayahesabu jijini Dar. Unatoka na basi la Yarabi Salama pale kisutu kituo cha mabasi cha zamani saa moja kasoro jioni unafika Tanga kituo cha mabasi saa moja kamili asubuhi inayofuata. Unatuma barua kwenda Kigoma au Rukwa inafuka baada ya wiki mbili.

Marais kuanzia wa awamu ya tatu mpaka hii ya tano wamejitahidi sana kuitangaza Tanzania kiuchumi lakini uchumi pekee pasipo nchi kuwa na uwezo wa kujitangaza yenyewe kupitia michezo ni jambo gumu kufanikiwa.

Kuna watu wanasema hawawezi kuiunga mkono Taifa Stars ikicheza dhidi ya Uganda Cranes eti kwa sababu waliopewa kazi ya kuamsha hamasa ni watu wenye dhambi kadhaa. Wanachosahau ni kuwa Tanzania ni kubwa na yenye thamani kuliko hawa wanajamii wa kisasa ambao mwaka 1980 wakati kina Tino na Ngulungu wanapambana kule Lagos walikuwa aidha ni wadogo sana au hawajazaliwa.

Tanzania inahitaji sana wimbo wake wa Taifa upigwe mbele ya hadhira nzima ya wapenda soka wa Afrika, litakuwa ni jambo ambalo litautangaza utalii, litainua upya kiburi cha kitaifa kwamba nasisi tunaweza kile kinachoweza kufanywa na muafrika mwingine yoyote. Kizazi cha sasa chenye wenye nguvu ya kuzalisha kitakuwa kimepata heshima mpya.

Hapo sijaongelea soko la wachezaji, la hawa wadogo zake Mbwana Samatta na Simon Msuva. Sijaongelea soko la makocha wazalendo. Sijaongelea changamoto watakazozipata Simba na Yanga katika kuendana na dunia ya kisasa isiyomsubiri mtu asimame na kujikung'uta, yenyewe ikienda mbio muda wote.

Yapo mengi mno na muhimu tutakayoyapata ikiwa tutafanikiwa kushiriki AFCON kule Misri.
 
Wewe mtanzania unaota ndoto za kushiriki AFCON wakati unaomba dua mbili mbili eti mimi nishinde na yule afungwe, mnasahau kuwa yule naye ana haki ya kuomba ushindi kwa Mungu na aliutumia vyema mwanzo wake! Kwanza kuomba dua mbili mbili kwa Mungu ni sawa na uchawi. Pambaneni na hali zenu bwana. Ujana wenu nilikuwa wapi leo siku ya mwisho mnajaza behewa la dua kwenda kwa Mungu?
 
Watanzania wanapenda stars ifuzu afcon na walianza nayo tangu mashindano yanaanza tatizo ni hawa wanasiasa waliovamia huku mwishoni hao ndo kero ya tulio wengi, hawakuonekana tangu mwanzo sasa wanataka ionekane bila wao stars isingefika ilipo
Tatizo, hao ni mfumo mzima wa uendeshaji soka nchini ni wa ki magumashi, na ki zimamoto, wewe mwishoni kabisa ndio mnakuja na slogan, bila maandalizi mazuri!! Juzi kuna timu ya Arusha imejitoa ligi daraja la kwanza kisa wanapokutana na timu za majeshi, zikifungwa mtapigwa ile mbaya na ni marufuku kwa mechi ku recodiwa hata kama una kibali!! Na mkipeleka malalamiko kwenye bodi ya ligi wanayapuuza!! Tatizo sio kushiriki Afcon /kombe la dunia, saudi arabia /iran si kila mala wanashiriki kombe la dunia wanaenda wanachukua sita!! Hao ni wazee wa kudandia treni kwa mbele!! Kutafuta political mileage tu,
 
Tatizo, hao ni mfumo mzima wa uendeshaji soka nchini ni wa ki magumashi, na ki zimamoto, wewe mwishoni kabisa ndio mnakuja na slogan, bila maandalizi mazuri!! Juzi kuna timu ya Arusha imejitoa ligi daraja la kwanza kisa wanapokutana na timu za majeshi, zikifungwa mtapigwa ile mbaya na ni marufuku kwa mechi ku recodiwa hata kama una kibali!! Na mkipeleka malalamiko kwenye bodi ya ligi wanayapuuza!! Tatizo sio kushiriki Afcon /kombe la dunia, saudi arabia /iran si kila mala wanashiriki kombe la dunia wanaenda wanachukua sita!! Hao ni wazee wa kudandia treni kwa mbele!! Kutafuta political mileage tu,
Nimemkataza mtoto wangu asiende kesho.bashite anataka tusahau madhambi take ya kuteka na kuua watanzania wasiomkubali jiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu tubariki sisi waganda tuifunge Tanzania ya makonda
Asitokee mtu akamdanganya mtanzania kwa namna yoyote ile, ushiriki wetu wa michuano ya mataifa huru Afrika ni muhimu kuliko siasa za kisasa za vyama vingi. Kuonekana kwetu katika michuano hii ya soka ambayo hukutanisha timu bora za mataifa ya afrika ni muhimu sasa pengine kuliko katika kipindi chochote nyuma.

Tulionekana mara ya mwisho tukishiriki AFCON mwaka 1980, miaka 39 iliyopita. Sio jana wala sio juzi, enzi hizo magari unayahesabu jijini Dar. Unatoka na basi la Yarabi Salama pale kisutu kituo cha mabasi cha zamani saa moja kasoro jioni unafika Tanga kituo cha mabasi saa moja kamili asubuhi inayofuata. Unatuma barua kwenda Kigoma au Rukwa inafuka baada ya wiki mbili.

Marais kuanzia wa awamu ya tatu mpaka hii ya tano wamejitahidi sana kuitangaza Tanzania kiuchumi lakini uchumi pekee pasipo nchi kuwa na uwezo wa kujitangaza yenyewe kupitia michezo ni jambo gumu kufanikiwa.

Kuna watu wanasema hawawezi kuiunga mkono Taifa Stars ikicheza dhidi ya Uganda Cranes eti kwa sababu waliopewa kazi ya kuamsha hamasa ni watu wenye dhambi kadhaa. Wanachosahau ni kuwa Tanzania ni kubwa na yenye thamani kuliko hawa wanajamii wa kisasa ambao mwaka 1980 wakati kina Tino na Ngulungu wanapambana kule Lagos walikuwa aidha ni wadogo sana au hawajazaliwa.

Tanzania inahitaji sana wimbo wake wa Taifa upigwe mbele ya hadhira nzima ya wapenda soka wa Afrika, litakuwa ni jambo ambalo litautangaza utalii, litainua upya kiburi cha kitaifa kwamba nasisi tunaweza kile kinachoweza kufanywa na muafrika mwingine yoyote. Kizazi cha sasa chenye wenye nguvu ya kuzalisha kitakuwa kimepata heshima mpya.

Hapo sijaongelea soko la wachezaji, la hawa wadogo zake Mbwana Samatta na Simon Msuva. Sijaongelea soko la makocha wazalendo. Sijaongelea changamoto watakazozipata Simba na Yanga katika kuendana na dunia ya kisasa isiyomsubiri mtu asimame na kujikung'uta, yenyewe ikienda mbio muda wote.

Yapo mengi mno na muhimu tutakayoyapata ikiwa tutafanikiwa kushiriki AFCON kule Misri.

In God we trust
 
Nimemkataza mtoto wangu asiende kesho.bashite anataka tusahau madhambi take ya kuteka na kuua watanzania wasiomkubali jiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo Bashite kazaliwa 1982 taifa stars ilikwend Lagos 1980, alikuwa hajazaliwa. Sisi wengine tulikuwa tunajua nini kinaendelea duniani, tuliziona na kuzitumia stempu zenye picha ya Jellah Mtagwa, kutuambia tusiende mpirani kwa sababu tu ya huyo bwana mdogo ni kulikosea heshima taifa zima.
 
Philipo ni dhahiri bashite na jiwe ni maadui wa umoja wetu wa kitaifa, ni kipi linamfanya huyo bashite awe na kimbelembele wakati anajua hakubaliki? Ili wajue hatuko nao, tunaomba Tanzania ifungwe mabao ya kutosha.
 
Huyo Bashite kazaliwa 1982 taifa stars ilikwend Lagos 1980, alikuwa hajazaliwa. Sisi wengine tulikuwa tunajua nini kinaendelea duniani, tuliziona na kuzitumia stempu zenye picha ya Jellah Mtagwa, kutuambia tusiende mpirani kwa sababu tu ya huyo bwana mdogo ni kulikosea heshima taifa zima.
Ndiyo mjue madhara ya siasa za kibaguzi na kikandamizaji. Leo watu wanaotuhumiwa kwa mambo ya hovyo kwenye jamii eti ndiyo wanataka kuongoza watu kuonesha uzalendo.
 
Back
Top Bottom