voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,545
- 11,943
Tanzania inaendelea kubakia nyuma wakati mataifa mengi ya kiafrika yakipiga mwendo kwenye Demokrasia ya kweli.
Tanzania hakuna Demokrasia ya kweli isipokuwa kuna kiini macho cha Demokrasia au mazingaombwe ya Demokrasia.
Ni Tanzania tu ambako Rais wa nchi ni lazima awe Dokta, yaani mtu anapokuwa Rais wa Tanzania anapewa cheo cha ziada cha Udokta, wakati Rais wa nchi ni mkubwa kwa hadhi Kuliko vyeo vyote, maana yake Baada ya Mungu kwa hadhi anayefuata ni Rais wa nchi.
Lakini kwa Tanzania ni lazima waanze na Dokta, yaani kumwita tu mh Rais wanaona haitoshi.
Senegal Tayari wamepata tena Rais kutoka upinzani huku sisi tukiendelea kuikumbatia CCM, Chama kilichojichokea kabisa na kimekosa Dira ya kuongoza nchi.
CCM ni chama cha watu aina mbili Tu, kundi la kwanza ni watu wanaofaidika na Chama,na kundi la pili ambalo ndo kubwa zaidi ni la mambumbumbu wa kutupwa,ambao akila na kushiba,hata ukimwambia kuwa hii hewa inaletwa na CCM yeye anakubali tu.
Ni Tanzania tu, ambako Rais anapewa kila aina ya sifa na wapambe ili kujikomba.
Ni bora wangefuta kabisa vyama vya upinzani ili wabakie na li CCM Lao Kuliko kuwafanya watu wote hawana akili kabisa.
Yaani inashangaza sana, Tanzania yenye kila kitu kizuri, kuanzia ardhi, Raslimali zote lakini watu wake ni maskini wa kutupwa halafu Chama cha CCM kilichofeli kuongoza nchi eti bado kinawaambia wananchi wakipe ridhaa Tena.
Aisee Tanzania unachefua sana wewe nchi
Karibu Senegal !
Nimekatiza kusoma bandiko lako pale tu ulipoanza kuonyesha kuwa hujui jambo muhimu kuhusu Senegal [emoji1211].
Huyo Rais aliyeondoka madarakani alikuwa ni kiongozi wa upinzani aliyeshinda uchaguzi mkuu wa Senegal mwaka 2019.
Na aliingia madarakani kwa mbwembwe na ahadi za kutimiza utawala wa kidemokrasia tofauti na mtangulizi wake yule Mzee Wade.
Miaka mitano baadae naye amekuwa mtawala .....
Sasa anaingia kijana mwingine kutoka coalition ya Sonko aliyezuiwa kwa hila na serikali ya Mark Sally kugombea.
Na hiyo ndiyo hasa iliyowabeba hawa vijana maana wananchi walishuhudia mateso waliyoyapitia!
Kwa hiyo wamepata "POLITICAL SYMPATHY"
Nyinyi wapinzani wa Tanzania kazi yenu ni "kugombania" Tonge na sio kuwapigania wananchi. Ndio sababu hata wapinzani kwa wapinzani hampendani wala kuaminiana.
Halafu vijana wa kitanzania wengi wapenda short cuts za maisha.wale wa west Africa ni wapambanaji na wakienda shule wanaenda kweli.
Niambie ni mpinzani gani msomi wa Tanzania ambae amewahi kwenda kuongeza elimu ili kujisimika vizuri kwenye mazingira ya kufanya kazi na siasa kwa pamoja?