Tanzania ina hospital na vituo vingapi mahususi kushughulikia afya ya akili?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,607
46,245
Ukifuatilia kwa makini utagundua kuna ndugu, jamaa, marafiki, wafanyakazi, majirani na wengine wengi wanaotuzunguka kwa maneno wanayosema, vitu wanavyoamini au baadhi ya vitendo wana matatizo ya akili na hivyo kuhitaji huduma za afya ya akili kupitia wanasaikolojia na madokta wa afya ya akili "psychiatrists". Hata wewe binafsi unaweza kujikuta katika hali ya matatizo ya aina hiyo.

Kila mara huwa nasikia Mirembe ikitajwa kila inapozungumzwa matatizo ya akili.
Ningetaka kujua kwa wanaofahamu kama kuna Hospitali nyingine zaidi ya Mirembe za serikali au binafsi zinazotoa huduma za afya ya akili.

Pia serikali ina sera au muongozo wowote unahohusu kushugulikia wagonjwa au wenye matatizo akili?
 
Hospitali ya Mirembe ni Ya taifa kwa magonjwa ya afya ya akili.. ndiyo maana inaonekana maarufu.

Ni sawa na Kibong"oto kilimanjaro.. ni hospital ya taifa ya TB.


lakini huduma hiyo inapatikana kwa uzuri.. na ubingwa karibu hospital zote za mikoa.. na hospital zote za kanda
 
Mkuu, ni kweli. Hii hoja ni muhimu.
Hasa humu JF wamejaa tele, kwao matusi ni ya kufikia.

Tusubiri majibu ya Waungwana
 
Back
Top Bottom