Tanzania Daima's Obsession

Tanzania Daima's Obsession

Anaye sign ni Rais, na Rais bado hajasign sasa hapo lawama kuelekezwa kwake si upotoshwaji wa kesi nzima?

mkada Are you sure Rais Kikwete bado hajasaini sheria ya tozo la simu?
Kama bado hajasaini inakuwaje serikali ilishatangaza kutumika kwa sheria hii kuanzia Julai Mosi?
Kwanini tayari watanzania wameshaanza kula maumivu kwa sheria hii?
 
Last edited by a moderator:
mkada Are you sure Rais Kikwete bado hajasaini sheria ya tozo la simu?
Kama bado hajasaini inakuwaje serikali ilishatangaza kutumika kwa sheria hii kuanzia Julai Mosi?
Kwanini tayari watanzania wameshaanza kula maumivu kwa sheria hii?

Haelewi huyo
 
Last edited by a moderator:
Inavyoonekana mkada bado ni mchanga sana kuhusu siasa na mfumo wa uendeshaji wa nchi yetu, hususani Bunge na serikali.

*Kwa kifupi sana. Mfumo wa uendeshaji wa serikali yetu chini ya CCM Unaanzia kwenye Chama ambapo kwa sasa Kikwete ndio mwenyekiti wake, kisha jambo linaletwa ndani ya Baraza la mawaziri na hapo Kikwete ndio mwenyekiti wake, kisha linaletwa bungeni kupitia waziri husika na hapo Waziri mkuu, mawaziri wote na wabunge wote wa CCM wanatakiwa kuliunga mkono kwa hali na mali na mwisho wa siku Rais anatia saini kuwa sheria rasmi.

Tukirudi kwenye hili suala la tozo la simu, Serikali kupitia kwa waziri wa Fedha Willium Mgimwa ilileta bungeni likapitishwa na wabunge wa CCM KWA ASILIMIA 100 na mwisho likatiwa saini na Rais Kikwete kuwa sheria rasmi ili kuweza kutumika.
 
Last edited by a moderator:
Let's be realistic. Tanzania Daima is far much better kuliko Uhuru na Mzalendo. Sisemi wako perfect kama Mwanahalisi lakini atleast wanatekeleza kazi yao ya kuikosoa serikali na kuelimisha jamii ni kitendo cha kizalendo. Hawawezi wakaandika kila kitu unachopenda wewe, watanzania inatubidi tukubali kukosolewa hili Taifa ni letu sote sio la chama fulani au la dini fulani au kabila fulani.
 
Bunge lililopitisha ni Mibunge ya ccm kwa kura za ndiyoooooooo!!!!

Sasa hapo unaongea upumbavu gani wewe?
Chanzo ni ccm na ccm hii kodi itawagharimu

Uko sahihi Freedom Of Flag, asilimia kubwa ya wabunge wa upinzani waliikataa budget ya serikali na wa CCM wote waliokuwemo ndani ya ukumbi wakati huu walisema "ndiyo" maana yake ni kuwa walikubaliana na kila kitu. Ni mwanachama hai wa CCM lakini kwa kifupi viongozi wetu wengi ni majanga.
 
Last edited by a moderator:
Gazeti Tanzania Daima ni gazeti huru,haijalishi ni ccm au chadm habari zote zinaandikwa bila upendeleo...kamwe msibadilike km huyo mwenzenu..wamebakia kuandika "habari kwa ufupi,sijui kanda ya kati...nk
 
Ukisoma Taarifa ya gazeti la leo la Tanzania Daima la kichwa cha habari Simu kuing’oa CCM, ni wazi utajua kuwa sasa hili gazeti liko obsessed na chuki na hasira zinazopelekea kutuchanganya sisi wasomaji wake.Ni dhahiri kuwa tozo la kodi la kila mwezi lilipitishwa na bunge,,na hii ina maana lawama zote lazima ziende kwa Bunge na Spika akiwemo...lakini hili la Tanzania Daima la kuandika kuwa
kilichofanyika kilipata baraka za viongozi wa chama hicho, akiwamo Rais Jakaya Kikwete, nafikiri ni kuleta confusion ambayo ni very unnecessary.
Tanzania Daima wanachojaribu kufanya hapa ni kuconnect dots ambazo ziko too remote kwani tuna jua kuwa Bunge lina uongozi wake unaojitegemea, Rais hakuwa bungeni na pia hajaridhia maamuzi ya bunge ya tozo la kodi kuwa sheria.Sasa Rais hapo anaingiaje?Bunge si mhimili unaojitegemea, sasa kwa nn makosa ya bunge yawe makosa ya Rais.
This is unprofessional guys,,,inakuwa shida sana kulisoma hili gazeti kwa sasa bila kuchanganya na akili zako.Mbona Mwananchi wanaandika habari Objectively na bado linapendwa tu.Tanzania Daima you need to stop barking at the wrong trees for issues which are very serious. Tanzaia Daima wanataka kututufifisha kumjua the real enemy,,na hii itasababisha kushindwa kwa hii vita.The president should be involved in appeal but not in the war. Shida ni Bunge na sio Rais. Professionalism is not taking things personal.

in complete darkness we are all the same,it is our knowledge and wisdom that separates us,dont let your eyes deceive it.
 
Inavyoonekana mkada bado ni mchanga sana kuhusu siasa na mfumo wa uendeshaji wa nchi yetu, hususani Bunge na serikali.

*Kwa kifupi sana. Mfumo wa uendeshaji wa serikali yetu chini ya CCM Unaanzia kwenye Chama ambapo kwa sasa Kikwete ndio mwenyekiti wake, kisha jambo linaletwa ndani ya Baraza la mawaziri na hapo Kikwete ndio mwenyekiti wake, kisha linaletwa bungeni kupitia waziri husika na hapo Waziri mkuu, mawaziri wote na wabunge wote wa CCM wanatakiwa kuliunga mkono kwa hali na mali na mwisho wa siku Rais anatia saini kuwa sheria rasmi.

Tukirudi kwenye hili suala la tozo la simu, Serikali kupitia kwa waziri wa Fedha Willium Mgimwa ilileta bungeni likapitishwa na wabunge wa CCM KWA ASILIMIA 100 na mwisho likatiwa saini na Rais Kikwete kuwa sheria rasmi ili kuweza kutumika.

Umetiririka vizuri hadi nimekumbuka kwamba 2015 haiko mbali, hizi kodi tutakoma!!! Waziri wa Fedha anasema pesa hizo zinakusanywa kwaajili ya ''umeme na maji'' vijijini!!!
 
Last edited by a moderator:
Ukisoma Taarifa ya gazeti la leo la Tanzania Daima la kichwa cha habari Simu kuing¡¯oa CCM, ni wazi utajua kuwa sasa hili gazeti liko obsessed na chuki na hasira zinazopelekea kutuchanganya sisi wasomaji wake.Ni dhahiri kuwa tozo la kodi la kila mwezi lilipitishwa na bunge,,na hii ina maana lawama zote lazima ziende kwa Bunge na Spika akiwemo...lakini hili la Tanzania Daima la kuandika kuwa
kilichofanyika kilipata baraka za viongozi wa chama hicho, akiwamo Rais Jakaya Kikwete, nafikiri ni kuleta confusion ambayo ni very unnecessary.
Tanzania Daima wanachojaribu kufanya hapa ni kuconnect dots ambazo ziko too remote kwani tuna jua kuwa Bunge lina uongozi wake unaojitegemea, Rais hakuwa bungeni na pia hajaridhia maamuzi ya bunge ya tozo la kodi kuwa sheria.Sasa Rais hapo anaingiaje?Bunge si mhimili unaojitegemea, sasa kwa nn makosa ya bunge yawe makosa ya Rais.
This is unprofessional guys,,,inakuwa shida sana kulisoma hili gazeti kwa sasa bila kuchanganya na akili zako.Mbona Mwananchi wanaandika habari Objectively na bado linapendwa tu.Tanzania Daima you need to stop barking at the wrong trees for issues which are very serious. Tanzaia Daima wanataka kututufifisha kumjua the real enemy,,na hii itasababisha kushindwa kwa hii vita.The president should be involved in appeal but not in the war. Shida ni Bunge na sio Rais. Professionalism is not taking things personal.

Siliungi mkono gazeti hili lakini
Sikubaliani na wewe kuhusu bunge la Tz.
Bunge la Tz ni muhimili unaojitegemea kinadharia tu ili hali uhalisia wake ni sehemu ya serikali. Hebu tazama spika na wenyeviti wake wanavyoliendesha bunge, ni wazi kabisa kuwa wanaliendesha kwa kufuata maelekezo toka serikalini, hawako huru kabisa. FACT.
 
Chadema wanafiki bungeni wanaanzisha hoja na kuipitisha wakiwa nje ya bunge wanaipinga huo ni unyoka.
 
Gazeti Tanzania Daima ni gazeti huru,haijalishi ni ccm au chadm habari zote zinaandikwa bila upendeleo...kamwe msibadilike km huyo mwenzenu..wamebakia kuandika "habari kwa ufupi,sijui kanda ya kati...nk
Mkuu hapo siyo kweli tanzania daima ni gazeti la chadema kwa sababu mmiliki wa gazeti hili ni mbowe sasa unategemea nini hapo.
 
Kwa mda mrefu sasa tanzania daima limejikita kwenye udini huku likiweka mbele ukristo na kubeza udini kitu ambacho ni kibaya zaidi.
 
Anaye sign ni Rais, na Rais bado hajasign sasa hapo lawama kuelekezwa kwake si upotoshwaji wa kesi nzima?

kabla ya kwenda bungeni lilijadiliwa na baraza la mawaziri, na mwenyekiti ni rais hapo unasemaje?
 
unatuona sisi wajinga sana eeh? hivi nani haoni ushabiki wa kipumbavu unaofanywa na wabunge wapumbavu wa ccm kupitisha mambo ya kipumbavu kwa maagizo ya serikali ya kipumbavu ya ccm?
Mbona ckusikia hata mbunge mmoja wa upinzani akipinga hii kodi kwenye kujadili ule mswaada wa fedha uliokuja na haya mapendekezo tatizo hapa sio wabunge wa ccm wabunge wote ni tatizo wao wanatumia bunge kama ni platform ya kujenga vyama nyao


Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom