Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Balozi Emily Burns ambaye pia ametumia kikao hicho kwa ajili ya kujitambulisha,amesema nchi ya Canada ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika kuwaendeleza wachimbaji wadogo nchini kwa kuwajengeza uwezo katika uchimbaji wa matumizi sahihi ya Teknolojia utakaozingatia utunzaji wa mazingira na kuwajengea ujuzi ili kuongeza tija kwenye uzalishaji madini.
Balozi Burns ametumia pia fursa hiyo kuupongeza uongozi wa Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa mageuzi makubwa yanayofanyika kwenye sekta ya madini hadi kupelekea kuongezeka kwa mchango wa sekta ya madini kwenye pato la Taifa kufikia asilimia 10.1 kwa mwaka 2024.
Waziri Anthony Mavunde ameishukuru serikali ya Canada kwa dhamira yake ya kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza sekta ya madini huku msisitizo mkubwa akiuweka katika ushirikiano wa Utafiti wa Kina wa upatikanaji wa madini nchini ili kusaidia upatikanaji wa taarifa sahihi za uwingi wa madini nchini.
Waziri Mavunde pia ameonesha umuhimu wa uwezeshaji wa Wakina mama na Vijana kupitia Programu ya Mining for a brighter Tomorrow(MBT) yenye lengo la kuyawezesha makundi hayo mawili katika ushiriki wake katika uchumi kupitia sekta ya madini.