Tangazo la maelezo ya ajira - MSD

SHOOyaKIBABE

JF-Expert Member
Feb 10, 2014
2,181
1,707
Screenshot_2017-03-30-20-41-55.png


TAARIFA KWA UMMA UTAPELI KUHUSU KUITWA KWENYE USAILI

Hivi karibuni Bohari ya Dawa (MSD) ilitangaza nafasi za kazi mbalimbali,ambapo imekamilisha kupokea maombi tangu tarehe 14/3/2017. Kwa sasa MSD ipo katika Hatua za kukamilisha uchambuzi wa sifa za waombaji kulingana na nafasi walizoomba. Waombaji wote watakaokidhi vigezo wataitwa kwa ajili ya usaili na hata wale ambao hawataitwa kwa ajili ya usaili watajulishwa kwa utaratibu ambao Ofisi itauweka. Kumezuka matapeli wanaowapigia wananchi simu za kuitwa kwenye usaili. Wananchi wote mnaombwa kupuuza simu mnazopigiwa na watu hao wanaodai kuwa ni wa Bohari ya Dawa, zikidai kuwaita kwenye usaili na kuombwa kutuma shilingi 70,000/= au fedha yoyote. Watu hao ni matapeli na hawahusiki na Ofisi ya Bohari ya Dawa (MSD). Endapo unahisi kuna mtu anakupa taarifa hizo tafadhali piga simu na omba kuongea na Ofisi ya Rasilimali Watu au tuma Barua pepe kwa anuani:
maoni.dg@msd.go.tz ,

Kwa ufafanuzi zaidi, wasiliana moja kwa moja na MSD kwa kupiga simu ya mezani namba +255 22 2860890 - 7

Imetolewa na
Etty Kusiluka
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Bohari ya Dawa (MSD)
22/03/2017

“ Tumedhamiria Kuokoa Maisha Yako ”
 
View attachment 488948

TAARIFA KWA UMMA UTAPELI KUHUSU KUITWA KWENYE USAILI

Hivi karibuni Bohari ya Dawa (MSD) ilitangaza nafasi za kazi mbalimbali,ambapo imekamilisha kupokea maombi tangu tarehe 14/3/2017. Kwa sasa MSD ipo katika Hatua za kukamilisha uchambuzi wa sifa za waombaji kulingana na nafasi walizoomba. Waombaji wote watakaokidhi vigezo wataitwa kwa ajili ya usaili na hata wale ambao hawataitwa kwa ajili ya usaili watajulishwa kwa utaratibu ambao Ofisi itauweka. Kumezuka matapeli wanaowapigia wananchi simu za kuitwa kwenye usaili. Wananchi wote mnaombwa kupuuza simu mnazopigiwa na watu hao wanaodai kuwa ni wa Bohari ya Dawa, zikidai kuwaita kwenye usaili na kuombwa kutuma shilingi 70,000/= au fedha yoyote. Watu hao ni matapeli na hawahusiki na Ofisi ya Bohari ya Dawa (MSD). Endapo unahisi kuna mtu anakupa taarifa hizo tafadhali piga simu na omba kuongea na Ofisi ya Rasilimali Watu au tuma Barua pepe kwa anuani:
maoni.dg@msd.go.tz ,

Kwa ufafanuzi zaidi, wasiliana moja kwa moja na MSD kwa kupiga simu ya mezani namba +255 22 2860890 - 7

Imetolewa na
Etty Kusiluka
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Bohari ya Dawa (MSD)
22/03/2017

“ Tumedhamiria Kuokoa Maisha Yako ”
Hiyo ni michezo ya ndani humo humo namba zngu wemezitoa wapi mpka na nafasi niliomba wanaijuaje kama sio mnazungukana humo ndani?
 
Tayari wapo wateule. Wanakuzubaisha ili ukipigiwa simu upuuze, wapate kuwaajiri watoto wao kirahisi
 
Wanaita lin huo usail kinacho wachelewesha ni iki tu kutupgia cm matapel wametoa wap no ?
 
huo ujumbe unasemaje ebu uweke humu tuone kama ni official
Wakuu sina haja ya kuzingua mtu humu sikujui hunijui, nikuzingue ili iweje, hujalazimishwa kuamini, mie nawaambia kitu halisi
Wamenitumia Ujumbe unasema "Ndugu (JINA LANGU) MSD inakukaribisha kwenye usahili kwa nafasi uliyoomba ya Software Developer itakayofanyika siku ya jumamosi tarehe 29/4/2017 saa 4.30 asubuhi chuo cha IFM, Dar es salaam. Tafadhali fika na kitambulisho chako. MSD haitahusika na gharama za usafiri. Kwa maelezo zaidi piga 255 222860890/7
 
Wakuu sina haja ya kuzingua mtu humu sikujui hunijui, nikuzingue ili iweje, hujalazimishwa kuamini, mie nawaambia kitu halisi
Wamenitumia Ujumbe unasema "Ndugu (JINA LANGU) MSD inakukaribisha kwenye usahili kwa nafasi uliyoomba ya Software Developer itakayofanyika siku ya jumamosi tarehe 29/4/2017 saa 4.30 asubuhi chuo cha IFM, Dar es salaam. Tafadhali fika na kitambulisho chako. MSD haitahusika na gharama za usafiri. Kwa maelezo zaidi piga 255 222860890/7
Hana tofauti na yule alisemaga kuwa lapf wamepgia sim kufnya usaili trh 23 March kumbe full uongo
 
Hana tofauti na yule alisemaga kuwa lapf wamepgia sim kufnya usaili trh 23 March kumbe full uongo
Kupiga simu na kutumiwa ujumbe ni vitu viwili tofauti mkuu. Ila kama huamini basi, mie nimetoa taarifa kama watu walivyokuwa wanaulizia, Hiyo ndo taarifa niliyopewa, nidanganye ili isaidie nini; Sina haja ya kusema uongo kwa ajili yangu mwenyewe, huo ndo ukweli, Hulazimishwi kukubaliana na Taarifa niliyoitoa, ukiona inafaa sawa ukion uongo pia mie sina kitu cha kupoteza.
 
Back
Top Bottom