Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Tarehe 21 na 22 ya mwezi huu,sisi wanachama wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) tulikuwa na mkutano wa siku mbili.Mkutano husika ulifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC). Vikao husika vilifanyika katika Ukumbi wa Simba.
Katika mkutano huo, hasa sku ya kwanza, mada mbalimbali ziliwasilishwa na kujadiliwa. Mada zilizowasilishwa zililenga hasa Mchakato unaoendelea hapa nchini wa kuandika Katiba mpya ya nchi yetu. Watoa mada na wachangia mada walikuwa machachari na waliojiandaa vya kutosha. Wataalamu wa Sheria kama akina Prof. Hamudi Ismail Majamba na Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi walichagiza mada hizo.
Jioni ya tarehe 21, TLS ikaadhimia kuwa na tamko la pamoja juu ya Mchakato wa Katiba mpya Tanzania kwakuwa ilionekana mchakato huo kuanza kwenda mrama. TLS,kama chama cha Wanasheria, kikataka kuweka mambo sawa katika kukemea,kuelekeza na kusahihisha mchakato husika. Timu ya manguli wa sheria ikaundwa kuandaa maadhimio. Ikawajumuisha Mawakili Wasomi kama Prof. H.I. Majamba, Alute Mughway, Beatus Malima na Peter Kibatala.
Maadhimio yakaandaliwa na kusomwa tarehe 22/2/2014. Maadhimio husika yalijikita katika,pamoja na mambo mengine, kusema kuwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba lazima wazingatie maoni ya wananchi katika kuchakata Katiba mpya. Hii ni kusema,Bunge Maalum la Katiba halina mamlaka ya kuacha kabisa Rasimu ya Pili ya Tme ya Jaji Warioba na kuongelea litakayo. Lazima Rasimu iwe ndiyo msingi wa majadiliano kwakuwa ndiyo iliyobeba maoni ya watanzania.
Lakini,tangu maadhimio hayo, kumekuwa na ukimya. Maadhimio hayasikiki wala kutambulika. Hata sina taarifa ya kufanyika kwa Mkutano wa Waandishi wa Habari kutoa Maadhimio hayo. Maadhimio yale ya Arusha yaliishia wapi?
Katika mkutano huo, hasa sku ya kwanza, mada mbalimbali ziliwasilishwa na kujadiliwa. Mada zilizowasilishwa zililenga hasa Mchakato unaoendelea hapa nchini wa kuandika Katiba mpya ya nchi yetu. Watoa mada na wachangia mada walikuwa machachari na waliojiandaa vya kutosha. Wataalamu wa Sheria kama akina Prof. Hamudi Ismail Majamba na Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi walichagiza mada hizo.
Jioni ya tarehe 21, TLS ikaadhimia kuwa na tamko la pamoja juu ya Mchakato wa Katiba mpya Tanzania kwakuwa ilionekana mchakato huo kuanza kwenda mrama. TLS,kama chama cha Wanasheria, kikataka kuweka mambo sawa katika kukemea,kuelekeza na kusahihisha mchakato husika. Timu ya manguli wa sheria ikaundwa kuandaa maadhimio. Ikawajumuisha Mawakili Wasomi kama Prof. H.I. Majamba, Alute Mughway, Beatus Malima na Peter Kibatala.
Maadhimio yakaandaliwa na kusomwa tarehe 22/2/2014. Maadhimio husika yalijikita katika,pamoja na mambo mengine, kusema kuwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba lazima wazingatie maoni ya wananchi katika kuchakata Katiba mpya. Hii ni kusema,Bunge Maalum la Katiba halina mamlaka ya kuacha kabisa Rasimu ya Pili ya Tme ya Jaji Warioba na kuongelea litakayo. Lazima Rasimu iwe ndiyo msingi wa majadiliano kwakuwa ndiyo iliyobeba maoni ya watanzania.
Lakini,tangu maadhimio hayo, kumekuwa na ukimya. Maadhimio hayasikiki wala kutambulika. Hata sina taarifa ya kufanyika kwa Mkutano wa Waandishi wa Habari kutoa Maadhimio hayo. Maadhimio yale ya Arusha yaliishia wapi?