Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamisi Mwinjuma maarufu MwanaFA amezindua mradi wa maji katika Kijiji cha Kwatango wenye thamani ya shilingi milioni 679.
Akizindua mradi huo kwenye uwanja wa Kijiji cha Kwatango kilichopo kata ya Kwemingoji wilayani Muheza, MwanaFA alisema mradi huo ni matunda yaliyofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika miradi mingi ya maji nchini ikiwemo wilaya ya Muheza.
Alisema mradi huo ni kati ya miradi 17 iliyopo wilayani Muheza ambayo inashughulikiwa na Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) na inagharimu kiasi cha shilingi bilioni 8.4. fedha zote zilizotolewa kwa ajili ya miradi ya maji wilayani Muheza ni shilingi bilioni 11.890.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Alisema wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan wakati wa ziara yake mkoani Tanga alizindua mradi wa Maji wa miji 28 katika mkoa wa Tanga ambao utaweza kugharimu kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 100 na kati ya fedha hizo Muheza imetengewa shilingi bilioni 40.
Alisema kabla ya mwaka 2020 wilaya ya Muheza ilikuwa ikipata maji kwa wastani wa asilimia 41 na Sasa katika miaka minne hii wananchi wa Muheza wanapata maji kwa wastani wa asilimia 71.
"Mradi wetu wa Maji wa miji 28 katika wilaya yetu ya Muheza ukikamilika tutakuwa tunapata maji kwa wastani wa juu ya asilimia 95 na utahudumia wananchi wapatao 400,000 katika kata 17 zilizopo wilayani hapa," alisema.
Alisema serikali ya awamu ya sita imekuja kumtua mama ndoo kichwani kutokana na kwamba hapo awali ndoa nyingi zilikuwa zikivunjika kutokana na tatizo la uhaba wa Maji lakini Sasa wananchi wanapata maji karibu.
Akizindua mradi huo kwenye uwanja wa Kijiji cha Kwatango kilichopo kata ya Kwemingoji wilayani Muheza, MwanaFA alisema mradi huo ni matunda yaliyofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika miradi mingi ya maji nchini ikiwemo wilaya ya Muheza.
Alisema mradi huo ni kati ya miradi 17 iliyopo wilayani Muheza ambayo inashughulikiwa na Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) na inagharimu kiasi cha shilingi bilioni 8.4. fedha zote zilizotolewa kwa ajili ya miradi ya maji wilayani Muheza ni shilingi bilioni 11.890.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Alisema wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan wakati wa ziara yake mkoani Tanga alizindua mradi wa Maji wa miji 28 katika mkoa wa Tanga ambao utaweza kugharimu kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 100 na kati ya fedha hizo Muheza imetengewa shilingi bilioni 40.
Alisema kabla ya mwaka 2020 wilaya ya Muheza ilikuwa ikipata maji kwa wastani wa asilimia 41 na Sasa katika miaka minne hii wananchi wa Muheza wanapata maji kwa wastani wa asilimia 71.
"Mradi wetu wa Maji wa miji 28 katika wilaya yetu ya Muheza ukikamilika tutakuwa tunapata maji kwa wastani wa juu ya asilimia 95 na utahudumia wananchi wapatao 400,000 katika kata 17 zilizopo wilayani hapa," alisema.
Alisema serikali ya awamu ya sita imekuja kumtua mama ndoo kichwani kutokana na kwamba hapo awali ndoa nyingi zilikuwa zikivunjika kutokana na tatizo la uhaba wa Maji lakini Sasa wananchi wanapata maji karibu.