Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,450
- 5,277
Mwalimu Enock Peter (32) wa Shule ya Msingi Potwe wilayani Muheza mkoani Tanga, amedaiwa kujinyonga kwa kutumia shuka nyumbani kwake, wakati Kesi yake dhidi ya anayedaiwa kuwa Mpenzi wake ikiwa Mahakamani.
Leo Jumatano Julai 16, 2025, Mratibu Elimu Kata ya Pongwe, Rajabu Msuya amesema alifika shuleni kwa mwalimu huyo kwaajili ya kufanya kikao ambapo alimu wote walikuwepo kasoro mwalimu Enock.
“Nilimtuma mwanafunzi aende nyumbani kwake akamuite, lakini aliporudi akasema amegonga lakini hakuitikiwa. Baadaye mwalimu mwingine alienda naye, wakagonga bila kuitikiwa, akaamua kuchungulia dirishani ndipo akamuona mwenzetu amejinyonga,” amesimulia Msuya.
Amesema baada ya kubaini hayo, walitoa taarifa polisi na askari walifika na kuingia ndani na kukuta amejinyonga kwa kutumia shuka aliyoifunga kwenye mbao za juu ya paa la nyumba ya shule aliyokuwa akiishi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi amesema uchunguzi wa awali unaonesha chanzo cha kifo hicho ni wivu wa mapenzi.
Soma Pia: Geita: Mwalimu ajinyonga kisa migogoro ya kifamilia
“Katika uchunguzi wetu tumebaini marehemu alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mpenzi wake (jina limehifadhiwa). Waliwahi kugombana na alichana vyeti vya mwenza wake na kesi ilikuwa inaendelea mahakamani. Wakati kesi ikiendelea, ndiyo mwalimu huyo ameamua kujinyonga,” amesema.
Amesema Enock alishawahi kukamatwa na kufunguliwa kesi mahakamani akituhumiwa kwa uharibifu wa mali za mwenza wake na aliachiwa kwa dhamana huku kesi ikiendelea.
Shuhuda wa tukio hilo, Abdulrazaq Kikungo amedai siku mbili kabla ya kujinyonga, Enock aligombana na mwenza wake baada ya kudai kumkuta na ujumbe wa mapenzi kwenye simu. Alimtishia kumuua kwa kisu, jambo lililomfanya mwenza huyo kukimbia.
“Baada ya mpenzi wake kutoroka, Enock alichukua kisu na kukatakata baadhi ya vyombo, kuvunja kabati na kuchana vyeti vya chuo vya mwenza wake. Alishtakiwa polisi na alikamatwa, akaamriwa kulipa gharama za vyeti.”
Amesema wakati mvutano huo ukiendelea na kesi ikiwa mahakamani, jana ndipo waligundua mwalimu huyo amejinyonga, wakihisi chanzo ni wivu wa mapenzi.
“Baada ya ugomvi huo, Enock alikuwa hatoki nje. Mchana alikuwa anakaa ndani pekee yake, usiku kidogo ndio anaenda dukani kununua mikate au viazi."
Leo Jumatano Julai 16, 2025, Mratibu Elimu Kata ya Pongwe, Rajabu Msuya amesema alifika shuleni kwa mwalimu huyo kwaajili ya kufanya kikao ambapo alimu wote walikuwepo kasoro mwalimu Enock.
“Nilimtuma mwanafunzi aende nyumbani kwake akamuite, lakini aliporudi akasema amegonga lakini hakuitikiwa. Baadaye mwalimu mwingine alienda naye, wakagonga bila kuitikiwa, akaamua kuchungulia dirishani ndipo akamuona mwenzetu amejinyonga,” amesimulia Msuya.
Amesema baada ya kubaini hayo, walitoa taarifa polisi na askari walifika na kuingia ndani na kukuta amejinyonga kwa kutumia shuka aliyoifunga kwenye mbao za juu ya paa la nyumba ya shule aliyokuwa akiishi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi amesema uchunguzi wa awali unaonesha chanzo cha kifo hicho ni wivu wa mapenzi.
Soma Pia: Geita: Mwalimu ajinyonga kisa migogoro ya kifamilia
“Katika uchunguzi wetu tumebaini marehemu alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mpenzi wake (jina limehifadhiwa). Waliwahi kugombana na alichana vyeti vya mwenza wake na kesi ilikuwa inaendelea mahakamani. Wakati kesi ikiendelea, ndiyo mwalimu huyo ameamua kujinyonga,” amesema.
Amesema Enock alishawahi kukamatwa na kufunguliwa kesi mahakamani akituhumiwa kwa uharibifu wa mali za mwenza wake na aliachiwa kwa dhamana huku kesi ikiendelea.
Shuhuda wa tukio hilo, Abdulrazaq Kikungo amedai siku mbili kabla ya kujinyonga, Enock aligombana na mwenza wake baada ya kudai kumkuta na ujumbe wa mapenzi kwenye simu. Alimtishia kumuua kwa kisu, jambo lililomfanya mwenza huyo kukimbia.
“Baada ya mpenzi wake kutoroka, Enock alichukua kisu na kukatakata baadhi ya vyombo, kuvunja kabati na kuchana vyeti vya chuo vya mwenza wake. Alishtakiwa polisi na alikamatwa, akaamriwa kulipa gharama za vyeti.”
Amesema wakati mvutano huo ukiendelea na kesi ikiwa mahakamani, jana ndipo waligundua mwalimu huyo amejinyonga, wakihisi chanzo ni wivu wa mapenzi.
“Baada ya ugomvi huo, Enock alikuwa hatoki nje. Mchana alikuwa anakaa ndani pekee yake, usiku kidogo ndio anaenda dukani kununua mikate au viazi."