Tanga mjini na stori za kufikirika

Tanga mjini na stori za kufikirika

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
372,655
Reaction score
863,525
kwamba;
1.kuna sehemu inaitwa mwembebasha, ukijipumzisha hapo mchana, lazima utapitiwa na usingizi na ukiamka umelowa makalioni

2; kuna warembo wa kiarabu lakini miguu kwato za ng'ombe

3; vifuu havipigwi teke, ukifanya hivyo kitakuuliza unanipigia nini?

4; kuna gesti chumba no 8 ukilala hapo lazima popobawa akupitie

5; usibebe hovyo wachumba wengine majini, unabeba mnaenda kulala gesti, ukiamka asubuhi uko ufukweni uchi au juu ya mti!!! kuna stori nyingi sana za kweli na za uongo ukifika huko sikiliza zote halafu amua mwenyewe
 
Hiyo namba moja sidhani kama ni ya kufikirika mkuu, hiyo kitu ipo niliwahi kupata ushuhida kwa utingo wa lori ambaye alikiri kukutana na jambo hilo
 
Kuna mti mkavu. asee haupindi huo ulivosimama ndio ivoivo.
 
Hamna vitu ivyo huku.ni story za vijiweni tu na kama zilikuwepo ni zamani sna.sasa tanga unabeba demu yeyoye.yaan pako poa.interraction na outsiders elite imekua kubwa.uswahil unapungua
 
Hiyo namba moja sidhani kama ni ya kufikirika mkuu, hiyo kitu ipo niliwahi kupata ushuhida kwa utingo wa lori ambaye alikiri kukutana na jambo hilo

Lakini ule mwembe uko bwembera sio tanga.
 
Hiyo namba moja sidhani kama ni ya kufikirika mkuu, hiyo kitu ipo niliwahi kupata ushuhida kwa utingo wa lori ambaye alikiri kukutana na jambo hilo

Mtambuzi, submission is not evidence, huyo driver alitoa submission, hakukupa ushahidi
 
Hiyo namba moja sidhani kama ni ya kufikirika mkuu, hiyo kitu ipo niliwahi kupata ushuhida kwa utingo wa lori ambaye alikiri kukutana na jambo hilo

ni kweli kaka naona kuna ukweli kwakuwa Tanga kuna maeneo ma5 tofauti yana hili jina
 
Lakini ule mwembe uko bwembera sio tanga.

yote ni Tanga kuna Muheza kama unaelekea Kicheba, kuna Misozwe mbele ya kicheba, Majani Mapana na njia ya kuelekea Mombasa karibu na Chumvini
 
Hiyo teknolojia ya mwembebasha ingetakiwa kuwekwa bungeni, mbunge akilala tu....akiamka lazma aombe muongozo 🙂 hahaha.

komba-auchapa-3.jpg


SIX.jpg

Mrema+chapa+Usingizi+3+%282%29.jpg


wasira+akifuatilia.jpg


MHE AKILALAMIKA KWENYE VYOMBO VYA HABARI JUU YA VITI VIPYA VYA BUNGE VYENYE TEKNOLOJIA YA TANGA ... :smile-big:

7.jpg


hii ni mtazamo tu jamani...
 
Back
Top Bottom