Tores
JF-Expert Member
- Nov 7, 2010
- 551
- 475
Kwa taarifa zinavyoripoti kwenye gazeti la Mwananchi, inaelekea baada ya mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kutaka ripoti ya matumizi ya kiasi fulani cha fedha toka TANESCO na TANESCO kushindwa kumpelekea ripoti ya matumizi ya fedha hizo, basi inasadikiwa kuwa shirika hilo la umeme Tanzania, TANESCO, limeilipa Kampuni ya kufua umeme ya DOWANS dola za Marekani 1.2 milioni ikiwa ni gharama ya kusafirisha mitambo ya kampuni hiyo kuja nchini kwa ndege, badala ya dola 120,000 tu.
Matumizi hayo ya ziada yanayokadiriwa kufikia shilingi za Kitanzania bilioni 1.4 yaliingizwa katika akaunti ya DOWANS kimakosa.
Matumizi mengine ya fedha yaliyohitaji ripoti wachilia hayo ya Bilioni 1 na ushee, ni mchanganuo wa matumizi ya dola za Marekani 4,865,000 sawa na shilingi za Kitanzania Bilioni 6.8!
Matumizi hayo ya ziada yanayokadiriwa kufikia shilingi za Kitanzania bilioni 1.4 yaliingizwa katika akaunti ya DOWANS kimakosa.
Matumizi mengine ya fedha yaliyohitaji ripoti wachilia hayo ya Bilioni 1 na ushee, ni mchanganuo wa matumizi ya dola za Marekani 4,865,000 sawa na shilingi za Kitanzania Bilioni 6.8!