TANESCO, Tangazeni ratiba ya mgao wa umeme

Lukolo

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
5,143
3,196
Kwa sasa karibu mikoa yote ya Tanzania inakabiliwa na katizo la umeme la kila siku. Vijiji vya pembezoni mwa Dar Es Salaam kama vila Pugu Majohe, vinakosa umeme kila siku kuanzia saa kumi jioni au wakati mwingine kuanzia saa moja na nusu jioni hadi saa sita za usiku. Wakati mwingine wakazi wa majohe wanakosa umeme usiku kucha. lakini hali ya ukataji wa umeme imeripotiwa pia huko Njombe, Mbeya, Arusha, Moshi, Mwanza na maeneo mengine mengi.

Pamoja na hali hii kukithiri na kuwa kero kwa watumiaji wa umeme, TANESCO haijatoa tamko lolote kuhusiana na mgao huu unaoendelea na wala haijawa tayari kutoa ratiba ya mgao huo. Binafsi napendekeza kwamba kwa maslahi ya wananchi, ni vema TANESCO wakatangaza ratiba ya mgao wa umeme ili wote tujue na tujiandae pale muda wa umeme kukatika unapofika. Utaratibu huu wa sasa wa ukataji umeme, unatuumiza sana watanzania wa hali ya chini, ambao maisha yetu yanategemea uuzaji wa ice cream na mabarafu.
 
Hii ni "PLAN" ili mkuu wa kaya apate la kusema, si mwaona IPTL wamezima mitambo yao shida tunayoipata?




"RAISI KAZI YAKE NI KUCHEKA CHEKA TUU!!"
 
Ninaungana na wazo la kubinafsisha shirika la TANESCO. Wenzetu Uganda wamefanya hivyo, na tangu shirika lao libinafsishwe, umeme haukatiki. Hapa kwetu serikali ya CCM inaogopa kulibinafsisha shirika hili kwa kuwa ndiyo kisima cha fedha zao za kampeni. Iwapo litabinafsishwa watashindwa kwa kuchota hela. If you can recall Richmond, IPTL ya wakati huo, na leo tena ESCROW. Hizi ni kashfa ambazo zimekuwa zikihusisha mabilioni ya fedha ambazo zinachotwa kutoka TANESCO kwa manufaa ya CCM. Kuna kila sababu ya watanzania kulipigia kelele suala hili na kuilazimisha serikali ibinafsishe huduma hii. Kama serikali imekuwa tayari kubinafsisha huduma mhimu kama za benk ambazo zinahusu fedha ya nchi, wanashindwaje kubinafsisha huduma ya umeme??
 
lipo tatizo la macashier wazee hasa mwanza hawawezi kutumia mashine za kuhesabu pesa wanahesabu kwa mikono ukiwa na laki mbili atahesabu saa nzima.
 
Back
Top Bottom