Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Tanesco inaelekea wanataka kutuhadaa -- wanajaribu sasa kuonyesaha kuwa kwa kiasi kikubwa matatizo yao ya kifedha yanatokana na madeni waliyolimbikiza wateja hali kadhalikawezi wa umeme.
Hilo sikatai lakini ni ukweli usiopingika kwamba matatizo yao makubwa yanatokana na ufisadi dhidi ya shirika hilo uliokuwa ukifanywa, na unaoendelea kufanywa na maafisa wa shirika hilo wakishirikiana na vigogo wa serikali.
Kikubwa hapa ni ule mtindo wa kuyapa makampuni binafsi kuweka mitambo, kufua umeme na kuiuzia Tanesco kwa mikataba kandamizi sana hadi kufikia kwamba Tanesco sasa hivi inayalipa makampuni hayo zaidi ya Sh bilioni 42 kwa mwezi.
Hebu fikiria iwapo badala yake, serikali ingekuwa imeiwezesha Tanesco kwa kuipatia mitambo hiyo, isingekuwa inalipa fedha hizo.
Mtindo huu, kwa kisingizio cha kupata umeme wa dharura ni 'brainchild' ya Jk tangu akiwa waziri wa nishati wakati wa awamu ya Msee Ruksa pale walipoleta IPTL iliyoanza kuinyonga Tanesco, na kuna kesi mahakamani kati ya IPTL na Tanesco/serikali hadi leo haijaisha.
Miaka 10 ya Mkapa hakukuwekwa kampuni yoyote ya kufua umeme wa aina hii, lakini alipoingia JK tu, makampuni hayo yakaanza kuja kama nyuki -- kuanzia Richmond, hadi sasa yako zaidi ya 10 yanayoinyonya Tanesco ile mbaya.
Eti sasa Tanesco inataka/inajaribu kuonyesha kwamba matatizo yao ya kifedha ni kutokana na madeni na wezi wa umeme.
Mimi naona hiyo ni janja tu, wanataka kuficha ufisadi mkubwa unaofanyika, kila mwezi viongozi wa serikali wananufaika na mabilioni kutoka makampuni hayo yanayoiuzia Tanesco umeme.
Nawasilisha hoja.
Hilo sikatai lakini ni ukweli usiopingika kwamba matatizo yao makubwa yanatokana na ufisadi dhidi ya shirika hilo uliokuwa ukifanywa, na unaoendelea kufanywa na maafisa wa shirika hilo wakishirikiana na vigogo wa serikali.
Kikubwa hapa ni ule mtindo wa kuyapa makampuni binafsi kuweka mitambo, kufua umeme na kuiuzia Tanesco kwa mikataba kandamizi sana hadi kufikia kwamba Tanesco sasa hivi inayalipa makampuni hayo zaidi ya Sh bilioni 42 kwa mwezi.
Hebu fikiria iwapo badala yake, serikali ingekuwa imeiwezesha Tanesco kwa kuipatia mitambo hiyo, isingekuwa inalipa fedha hizo.
Mtindo huu, kwa kisingizio cha kupata umeme wa dharura ni 'brainchild' ya Jk tangu akiwa waziri wa nishati wakati wa awamu ya Msee Ruksa pale walipoleta IPTL iliyoanza kuinyonga Tanesco, na kuna kesi mahakamani kati ya IPTL na Tanesco/serikali hadi leo haijaisha.
Miaka 10 ya Mkapa hakukuwekwa kampuni yoyote ya kufua umeme wa aina hii, lakini alipoingia JK tu, makampuni hayo yakaanza kuja kama nyuki -- kuanzia Richmond, hadi sasa yako zaidi ya 10 yanayoinyonya Tanesco ile mbaya.
Eti sasa Tanesco inataka/inajaribu kuonyesha kwamba matatizo yao ya kifedha ni kutokana na madeni na wezi wa umeme.
Mimi naona hiyo ni janja tu, wanataka kuficha ufisadi mkubwa unaofanyika, kila mwezi viongozi wa serikali wananufaika na mabilioni kutoka makampuni hayo yanayoiuzia Tanesco umeme.
Nawasilisha hoja.