Tanesco Morogoro wahujumu uchumi

IQup

JF-Expert Member
Jul 3, 2018
933
1,310
kuna taasisi mbili za ajabu sana mkoa wa morogoro na ninawasiwasi na mishahara wanayolipwa sijui ni kwasababu ipi
1. TANESCO. Tanesco ni kinara wa kukata umeme kila ifikapo mda wa saa kumi na mbili jioni mfululizo, kuanzia mda huo hadi saa sita usiku yaani ni kukata umeme na kurudisha hilo zoezi linajirudia mara kwa mara alafu ni kila siku. Saizi inaanza wiki ya pili sasa tangu waanze huo ujinga wao. Wamekuwa wakituharibia sana vitu vya thamani vinavyotumia umeme....imekuwa kero sana kila giza linapoanza kuingia hukata kata umeme mara kwa mara utadhani kwenye mitambo kuna wanafunzi wa field ambao wanajaribu kubonyeza kila kitu kuona nini kinatokea. Sasa wanatutia hasara....popote mlipo hiyo biashara kama inawalipa tangazeni kama kuanzia mida hiyo umeme sio wa uhakika hadi asubuhi kunapokucha


2. JESHI LA POLICE; linatumia nguvu kubwa sana kufukuzana na vijana barabarani...lakini hawawasaidii sana badala yake ni kama inajengwa uadui. Watoto hawana elimu wamenunuliwa boda wajikwamue kimaisha ..wewe trafic uliyesoma unavaa sare za kawaida na kuwafatilia vijana hadi nyumbani wanakoishi na kuwakamata huo ni utoto. Kumekuwa na wimbi la askari usalama kutokuvaa sare za kazi, inapotokea boda hajavaa kofia akapita mbele yake hao askari hujibeba na boda boda yao na kuanza kumfuata kwa nyuma taratibu...kijana anaposimama afanye kazi zake hapohapo wanamkamata...aisee waelimisheni kwanza acheni hizo roho...hao watu wakirudi mtaani wanaumiza wananchi ndio wanageuka waporaji, wabakaji nk

Jeshi unaanzisha semina za kuwafundisha madereva wote, unatumia wiki nzima, mnajilipa posho, mmekodi ukumbi wa bei kubwa..mnazunguka kutafuta vijana wa kuwafundisha....kumbe ni kamradi kenu mmeandaa vyeti vya bodaboda (elfu 50 sijui) na wale wa magari (100,000+_ kwa gharama mbili tofauti...sasa mnasaidia nini au mnafanya biashara kama wafanyabiashara wengine mitaani??. si mngewashauri waende veta mwezi mmoja wapata vyeti na leseni baadae.....

Hili la hawa jamaa bado linatia mashaka sana; pia mbona ujambazi wa kupora fedha watu unatokea karibu na kituo cha police tena mda wa saa kumi na mbili kweupe...mnashindwa kuwapata majambazi wanaotumia pikipiki kwelii kabisa?, kazi yenu ni ipi? msikie wananchi wameua mwizi nanyi muende mkabebe maiti? ndio kazi yenu kuu hiyo? (wanapora maduka ya jumla matatu na wanafanikiwa kutoweka hadi leo siku ya tatu kimyaa kwelii?)
Jeshi lijipambanue, usalama wa raia bado upo hatiani sana. Hata hao wafanyabiashara saizi wanafanya biashara roho zao zipo juu juu sana...mchana wanawaza kuvamiwa na usiku wanawaza kuvunjiwa.

Nilichokiona kwenu jeshi la police; mkipata taarifa huwa mnatoka kwa kujivuta alafu mnakimbiza gari baadae mnaanza kurudi kama kinyonga mnatumbua macho mkiwa mmekaa kwenye mabomba. Aisee wasaidieni wananchi kupata amani katika shughuri zao
 
kuna taasisi mbili za ajabu sana mkoa wa morogoro na ninawasiwasi na mishahara wanayolipwa sijui ni kwasababu ipi
1. TANESCO. Tanesco ni kinara wa kukata umeme kila ifikapo mda wa saa kumi na mbili jioni mfululizo, kuanzia mda huo hadi saa sita usiku yaani ni kukata umeme na kurudisha hilo zoezi linajirudia mara kwa mara alafu ni kila siku. Saizi inaanza wiki ya pili sasa tangu waanze huo ujinga wao. Wamekuwa wakituharibia sana vitu vya thamani vinavyotumia umeme....imekuwa kero sana kila giza linapoanza kuingia hukata kata umeme mara kwa mara utadhani kwenye mitambo kuna wanafunzi wa field ambao wanajaribu kubonyeza kila kitu kuona nini kinatokea. Sasa wanatutia hasara....popote mlipo hiyo biashara kama inawalipa tangazeni kama kuanzia mida hiyo umeme sio wa uhakika hadi asubuhi kunapokucha


2. JESHI LA POLICE; linatumia nguvu kubwa sana kufukuzana na vijana barabarani...lakini hawawasaidii sana badala yake ni kama inajengwa uadui. Watoto hawana elimu wamenunuliwa boda wajikwamue kimaisha ..wewe trafic uliyesoma unavaa sare za kawaida na kuwafatilia vijana hadi nyumbani wanakoishi na kuwakamata huo ni utoto. Kumekuwa na wimbi la askari usalama kutokuvaa sare za kazi, inapotokea boda hajavaa kofia akapita mbele yake hao askari hujibeba na boda boda yao na kuanza kumfuata kwa nyuma taratibu...kijana anaposimama afanye kazi zake hapohapo wanamkamata...aisee waelimisheni kwanza acheni hizo roho...hao watu wakirudi mtaani wanaumiza wananchi ndio wanageuka waporaji, wabakaji nk

Jeshi unaanzisha semina za kuwafundisha madereva wote, unatumia wiki nzima, mnajilipa posho, mmekodi ukumbi wa bei kubwa..mnazunguka kutafuta vijana wa kuwafundisha....kumbe ni kamradi kenu mmeandaa vyeti vya bodaboda (elfu 50 sijui) na wale wa magari (100,000+_ kwa gharama mbili tofauti...sasa mnasaidia nini au mnafanya biashara kama wafanyabiashara wengine mitaani??. si mngewashauri waende veta mwezi mmoja wapata vyeti na leseni baadae.....

Hili la hawa jamaa bado linatia mashaka sana; pia mbona ujambazi wa kupora fedha watu unatokea karibu na kituo cha police tena mda wa saa kumi na mbili kweupe...mnashindwa kuwapata majambazi wanaotumia pikipiki kwelii kabisa?, kazi yenu ni ipi? msikie wananchi wameua mwizi nanyi muende mkabebe maiti? ndio kazi yenu kuu hiyo? (wanapora maduka ya jumla matatu na wanafanikiwa kutoweka hadi leo siku ya tatu kimyaa kwelii?)
Jeshi lijipambanue, usalama wa raia bado upo hatiani sana. Hata hao wafanyabiashara saizi wanafanya biashara roho zao zipo juu juu sana...mchana wanawaza kuvamiwa na usiku wanawaza kuvunjiwa.

Nilichokiona kwenu jeshi la police; mkipata taarifa huwa mnatoka kwa kujivuta alafu mnakimbiza gari baadae mnaanza kurudi kama kinyonga mnatumbua macho mkiwa mmekaa kwenye mabomba. Aisee wasaidieni wananchi kupata amani katika shughuri zao
wamekamata pikipiki 700 hazifanyikazi hawaoni kwa kuziweka polisi wanakosesha mapato mengi kama zingejaza mafuta kiasi gani cha kodi tumepoteza kama turnover
 
wamekamata pikipiki 700 hazifanyikazi hawaoni kwa kuziweka polisi wanakosesha mapato mengi kama zingejaza mafuta kiasi gani cha kodi tumepoteza kama turnover
yaani hawa akili zao sijui zikoje aisee, waendesha boda boda wenyewe ukiwaangalia sura zao wengi wanaonekana kabisa kwamba ukimtoa huko na usipompatia kazi nyingine atakuwa kibaka huko aendako. Yaani hawawazi, wanakenua meno kufurahia kukamata...., watu wanatuumiza mitaani wanakabwa roba wanapokonywa vipochi akina dada....

sasa badala ya kutengeneza mazingira mazuri wengi wakimbilie kwenye boda boda ili mitaani angalau kuwe shwari, sasa wao ndio wanavuruga kabisa...sijui akili zao zikoje??
 
Jeshi la police morogoro chini ya RPC wao anaitwa Mtafungwa washapoteza dira wanaishia kuonea wananchi hasa Boda Boda wana kula rushwa ovyo ovyo
 
Jeshi la police morogoro chini ya RPC wao anaitwa Mtafungwa washapoteza dira wanaishia kuonea wananchi hasa Boda Boda wana kula rushwa ovyo ovyo
Mkuu wewe unaita rushwa,lakini unasahau zile figure zinatangazwa kila mwezi kuwa makusanyo yatokananyo na makosa ya barabarani yamepanda,na mtukufu anafurahi sana na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayofanya hao askari barabarani!?
Unadhani hayo makusanyo yanayoongezeka yanatika wapi kama sio matokeo ya hiyo mikimbizano na hao bodaboda pia?

Askari barabarani wana jukumu la kuelimisha raia juu ya utii wa sheria (za barabarani)bila shuruti, nilidhani wangepongezwa kama kungekuwa na mapato kidogo yatokanayo na makosa ya barabarani kwa sababu ingekuwa na maana kwamba raia wanaelimishwa vizuri juu ya kufuata sheria barabarani,na wangepaswa kukemewa pale mapato yanayotokana na makosa ya barabarani yanapoongezeka,kwani tafsiri yake ni kwamba wananchi walio wengi hawana uelewa na sheria hizo.

Maajabu ya hapa kwetu ni kwamba,tunafurahia na kualikwa kwenye lile jumba takatifu kwa ongezeko la mapato yatokanayo na makosa ya barabarani, lakini tunasikitika na kushangaa ajali zilivyoshika kasi ya kupunguza watanzania wenzetu kwa vifo!
 
Jeshi unaanzisha semina za kuwafundisha madereva wote, unatumia wiki nzima, mnajilipa posho, mmekodi ukumbi wa bei kubwa..mnazunguka kutafuta vijana wa kuwafundisha....kumbe ni kamradi kenu mmeandaa vyeti vya bodaboda (elfu 50 sijui) na wale wa magari (100,000+_ kwa gharama mbili tofauti...sasa mnasaidia nini au mnafanya biashara kama wafanyabiashara wengine mitaani??. si mngewashauri waende veta mwezi mmoja wapata vyeti na leseni baadae


Wameacha kazi ya usalama wa raia wanafanya biashara!? Hilo ni janga jingine sasa! Hivi hapo mjini si kuna chuo cha VETA cha udereva wa magari?
 
Huyo W. Mutafungwa alikuwa Tabora na ni shida sana, ni mzoefu kwenye hizo habari za kupokea make pale Tabora ni sehemu ambako vitendo hivyo ndo maisha ya kada yake. Kwahiyo Morogoro mkae mkao wa kutoa sana make mmempata master.

Tanesco Morogoro ni sawa na Tanesco Bukoba, wanakata umeme hadi unajiuliza hivi walienda kusomea kukata umeme tu? kwa siku wanaweza kukata zaidi ya mara kumi na wasiombe hata radhi na siku za wkend tulishazoeshwa hakuna umeme hata iweje ...kwa staili hii najiuliza hivyo viwanda vinakujaje na uchumi kukua
 
Wameacha kazi ya usalama wa raia wanafanya biashara!? Hilo ni janga jingine sasa! Hivi hapo mjini si kuna chuo cha VETA cha udereva wa magari?
Chuo cha VETA kipo tena mjini karibu tu hapa, cha ajabu wanachokifanya sasahivi ni aibu.....yaani wanapita na magari kwa mara nyingine tena kutangaza kwamba mafunzo yataanza tena tarehe 30 mwezi huu kwa ambao hawajahudhuria ili wapatiwe vyeti ......ni huzuni kwakweli
 
Mkuu wewe unaita rushwa,lakini unasahau zile figure zinatangazwa kila mwezi kuwa makusanyo yatokananyo na makosa ya barabarani yamepanda,na mtukufu anafurahi sana na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanayofanya hao askari barabarani!?
Unadhani hayo makusanyo yanayoongezeka yanatika wapi kama sio matokeo ya hiyo mikimbizano na hao bodaboda pia?

Askari barabarani wana jukumu la kuelimisha raia juu ya utii wa sheria (za barabarani)bila shuruti, nilidhani wangepongezwa kama kungekuwa na mapato kidogo yatokanayo na makosa ya barabarani kwa sababu ingekuwa na maana kwamba raia wanaelimishwa vizuri juu ya kufuata sheria barabarani,na wangepaswa kukemewa pale mapato yanayotokana na makosa ya barabarani yanapoongezeka,kwani tafsiri yake ni kwamba wananchi walio wengi hawana uelewa na sheria hizo.

Maajabu ya hapa kwetu ni kwamba,tunafurahia na kualikwa kwenye lile jumba takatifu kwa ongezeko la mapato yatokanayo na makosa ya barabarani, lakini tunasikitika na kushangaa ajali zilivyoshika kasi ya kupunguza watanzania wenzetu kwa vifo!

Mkuu umenena timamu kabisa. Bandiko lako lilistahili kuwafikia wote wanaohusika tokea juu hadi chini.

Ya kuwa hamkujua? Siku moja itabidi kuyajibu haya kwa ufasaha wake.

Malipo yote ni hapa hapa duniani.
 
Back
Top Bottom