TANESCO board split on MD Rashidi's fate

Mimi namuona Rashid kama fisadi tu. Huyu si ndiye aliyehamishiwa $600,000 na Chenge kwa kusaidia dili la rada? SFO walipombana akababaika. Aachie ngazi Tanesco huku akisubiri kesi yake. Tusipende sana kuwafagilia watu wanaopora utajiri wetu. Zitto anamtetea huyu fisadi kwa sababu zilizo wazi. (Refer utetezi wa ununuzi wa mitambo chakavu ya Dowans). Rashidi aliwekwa pale na Rostam baada ya kumtumia kule Vodacom. Aliwekwa Tanesco mahsusi kwa ajili ya ku-facilitate wizi wa kutisha wa kundi la mafisadi papa kupitia mikataba feki. Kwa kuwa wanaona hawajamaliza kazi ya kutuibia kwa njia ya mikataba mingi feki ya nishati ndio maana wanataka aendelee pale.

Rhetorics
 
Zitto ndugu yangu sawa inawezekana anafaa ila tutaishije na doa la RADAR? Mbona tumeshindwa kuishi na doa la RICHMOND tukamvua Uwaziri Mkuu mtu ambaye wadau wanakiri ni mtendaji wa hali ya juu? Unataka kusema LILA na FILA sasa VINATANGAMANA?

Ufisadi wa RADAR kwa mujibu wa makaratasi ya SFO unajadiliwa JF? Au ndio hukumu tayari?
Akamatwe akajibu mashitaka yake huko. Swali litakuja nani amkamate, wananchi tuna nguvu za kusukuma DPP kufungua mashtaka dhidi ya watuhumiwa. Mwishowe itakuwa yale yale ya kila mtu fisadi (unaona hata Sopshia Simba anaona eti michango ya harusi ya ya Jeetu Patel ni ufisadi wa Anna Kilango ili mradi tu kila mtu avikwe shuka ya ufisadi). CEO wa TANESCO sio mwanasiasa, ni mtendaji na hivyo hakuna kilichoitwa ajali ya kisiasa.......!!!!!!!
Tunapogeuza ufisadi ni mijadala ndio tunapoenda mrama. Mpaka sasa ni tuhuma na mahakama ikimtia hatiani hutaniona ninajenga hoja hizi. Lakini kama kuna ufisadi, au tuhuma za ufisadi akafanya TANESCO toka amekuwa CEO pale ziwekwe hapa na sio kutumia visingizio vya SFO kumhukumu mtu katika court za vijiweni.

Kuna vested interest nyingi katika Mashirika na kuna watu wanaona ni zamu yao kula. Ni suala la kuchagua nani iwe zamu yake maana siku hizi media ni silaha za wazi na kila kundi lina media zake. Katika TANESCO kuna zaidi ya tunachosoma katika This Day na Kulikoni au gazeti lingine loote. Kuna watu wanajaribu kuwatake wengine for granted. Wanaweza kufanikiwa lakini maana siku hizi Tanzania ni 'either with us or with Fisadis'
 
The best person (mzawa) kuliongoza shirika kama Tanesco angekuwa Idrisa. Ni mtu ambaye hababishiwi na wanasiasa. Track record yake hata akiwa BOT ilikuwa nzuri. Mlishawahi kusikia matumizi mabaya ya account ya EPA au scandal yeyote wakati wa tenure yake pale BOT.Doa pekee labada ni hizo payment zilizofanyika kwenye account yake kupitia kwa Andy Chenge. La kustaabisha ni kuwa hamna/hakuna mtu aliyemfuata kumuuliza his side of story (kama anayo hiyo obligation).
Hatoi posho au magari kwa wa wabunge/wanasiasa .
Critics wake should come out with suggestions na siyo kulaumu tu. Kama mnaona hafai basi angalau msuggest nani anaweza kuchukua nafasi hiyo.
Wizi wote unaotokea huwa ni siri mpaka bomu linapolipuka, wakati wa Rashid akiwa gavana wizi wa epa ulikuwepo na hata kuna mwanahalisi alishatoa moja ya wizi wa EPA enzi za Rashid akiwa gavana na fungu hili lilipitia Akiba Benki na nakala yake ilikuwepo kwenye mwanahalisi, So Rashidi si safi hata kidogo ni fisadi
 
Rhetorics

Rigidity..! Hebu tupunguze.

Tunasema mzuri, hajawahi kutokea, n.k.
Nadhani ni kiwango cha ufahamu tu. Kama hujawahi kuona mambo yakienda vizuri zaidi ya hapo, huwezi kuona ubaya. Lakini kwangu mimi nimeona mashirika yeaendayo vizuri duniani na CEO wazuri, wengine ni wa-TZ

Rashid can’t be a subset of them. Tatizo ni hizo support zisizokuwa na objectivity. Zimejaa siasa. Tulisoma naye, tunamfahamu, alitoa allowance nzuri, n.k, n.k
 
Pre-emptive strategy...........!

Umpende usimpende Rashidi, ni one of the best CEOs of our Parastatals.

Lets not lose sight here as to what is at stake... ITS INTERGRITY.
Dr Rashid experieced,learned or otherwise has not proven his worth.
When you have carry on baggages like the RADAR scandal and the Serious Fraud Office(SFO)is hounding you, is not exactly one thing to be proud of.
Dr Rashid has not proven to be a character of the caliber of Mr Arnold Kilewo,Mr Mbowe(formely of TIB), Mr Nsekela etc.

Ill intentions in management can kill ones reputation, as is the case with Dr Rashid
 
Wizi wote unaotokea huwa ni siri mpaka bomu linapolipuka, wakati wa Rashid akiwa gavana wizi wa epa ulikuwepo na hata kuna mwanahalisi alishatoa moja ya wizi wa EPA enzi za Rashid akiwa gavana na fungu hili lilipitia Akiba Benki na nakala yake ilikuwepo kwenye mwanahalisi, So Rashidi si safi hata kidogo ni fisadi

hebu thibitisha na habari za mwanahalisi zithibitshe kwa kutueleza namba ya toleo la gazeti. Habari zilizopo mpaka sasa ni zilizotolewa na Raiamwema kwa vithibitisho kwa EPA kuanza mwaka 2000. Ni kweli kulikuwa na debt conversion schemes etc. Thibitisha ufisadi uliotokea huko na tutakubaliana nawe badala ya kutoa sweeping statements.

Halafu tutaenda nyuma kuanzia kwa Mzee Mtei mpaka kina Nyirabu, Rutihinda nk ili kuona hizi schemes zilikuwaje. Pia tutaangalia wakati Benki Kuu inaungua ilikuwa ni nini nk. Yaani tuanze toka wakati wa Mwalimu akiwa Rais na hatua alizochukua, kwa mfano kwa kuungua Benki Kuu. Tusiwe na memory ndogo kwa ajili ya kumhukumu mtu.

On RADAR - nimesema hili ni suala la mahakamani na tushinikize wanaotajwa wapelekwe mahakamani na mahakama ndio pekee zenye mamlka ya kusafisha mtu au kuhukumu. Ingawa najua zitakuja hoja za uhuru wa mahakama nk - maana hata mimi suala la Zombe liliniacha hoi licha ya kuheshimu uhuru wa mahakama.
 
Rigidity..! Hebu tupunguze.

Tunasema mzuri, hajawahi kutokea, n.k.
Nadhani ni kiwango cha ufahamu tu. Kama hujawahi kuona mambo yakienda vizuri zaidi ya hapo, huwezi kuona ubaya. Lakini kwangu mimi nimeona mashirika yeaendayo vizuri duniani na CEO wazuri, wengine ni wa-TZ

Rashid can’t be a subset of them. Tatizo ni hizo support zisizokuwa na objectivity. Zimejaa siasa. Tulisoma naye, tunamfahamu, alitoa allowance nzuri, n.k, n.k

nipo flexible katika hili. Nipe facts tu na nitakubaliana nawe.

Sijasema hajawahi kutokea
 
Lets not lose sight here as to what is at stake... ITS INTERGRITY.
Dr Rashid experieced,learned or otherwise has not proven his worth.
When you have carry on baggages like the RADAR scandal and the Serious Fraud Office(SFO)is hounding you, is not exactly one thing to be proud of.
Dr Rashid has not proven to be a character of the caliber of Mr Arnold Kilewo,Mr Mbowe(formely of TIB), Mr Nsekela etc.

Ill intentions in management can kill ones reputation, as is the case with Dr Rashid

Integrity nakubaliana na wewe 100%! Mahakama basi ifanye kazi maana tusiwe mahakimu ingawa kuna court of public opinion.

Sina comment on kina Kilewo maana ni watu ninaowaheshimu sana ingawa nao wana mawaa yao. Tulikodisha KIA kwa kampuni ya kiingereza kwa tozo la dola 1000 kwa mwaka na kampuni hiyo mdau wake ni Mzee Kilewo. Unakumbuka lawama kwa Nsekela on ukabila nk. Ndio maana huwa sipendi kuhukumu watu kwa jumla jumla
 
Integrity nakubaliana na wewe 100%! Mahakama basi ifanye kazi maana tusiwe mahakimu ingawa kuna court of public opinion.

Sina comment on kina Kilewo maana ni watu ninaowaheshimu sana ingawa nao wana mawaa yao. Tulikodisha KIA kwa kampuni ya kiingereza kwa tozo la dola 1000 kwa mwaka na kampuni hiyo mdau wake ni Mzee Kilewo. Unakumbuka lawama kwa Nsekela on ukabila nk. Ndio maana huwa sipendi kuhukumu watu kwa jumla jumla

Sawa sawa Mkuu Zitto, lakini allegations za Dr Rashid zinagusa moja kwa moja kwenye maamuzi yake ambayo ni fraudulent in nature.
Hivyo basi reputation ya mtu kuongoza kitengo chochote cha kibiashara inakuwa na walakin, na anporudishwa mahala hapo against public opinion eyebrows tend to be raised.
Hivyo basi inabidi wasi wasi huo uondolewe na mahakama KABLA ya mtu huyo kupewa madaraka mengine kama hayo.
Hao nilio wataja hawakuwa DIRECTLY implicated katika allegations ulizozitoa , bali ni third party.
 
Tunapogeuza ufisadi ni mijadala ndio tunapoenda mrama. Mpaka sasa ni tuhuma na mahakama ikimtia hatiani hutaniona ninajenga hoja hizi. Lakini kama kuna ufisadi, au tuhuma za ufisadi akafanya TANESCO toka amekuwa CEO pale ziwekwe hapa na sio kutumia visingizio vya SFO kumhukumu mtu katika court za vijiweni.QUOTE][/COLOR]

Hivi Mh Zitto kwenye ile list yenu of shame mliyoitoa pale Mwembe Yanga wale watu walikuwa wameshahukumiwa na mahakama gani? Kama ni mahakama za kisiasa kawa nini watu wengine wakitumia njia hiyo kumhukumu Dr Idris unaona wanakosea? Halafu katika ripoti ya EPA ya auditors ambayo iko JF wakaguzi wanasema kwamba waliona barua ya Ruth Mollel kwa Gavana wa Benki ya mwaka 1997 (wakati huo akiwa Idris) ikitaka kujua status ya EPA ambayo haikujibiwa. Kitu kingine ni CIS ambayo pia inafanana na EPA ambayo ilitokea Dr Idris akiwa gavana na hiyo utakuwa unafahamu maana zaidi kuliko mimi maana nadhani kuna kamati iliundwa kuchunguza. Pia Idris alivyoondoka BoT alikwenda Akiba ambako hakukaa akaenda Vodacom ambako alishushwa cheo kutoka CEO mpaka Marketing Manager, wewe unatuambia kuwa the guy is the best CEO.

Inawezekana unatumia vigezo vingine na sisi, lakini kipimo cha utendaji siyo faidia tu ndugu Zitto, na inabidi uwe makini sana kwani faida inaweza kutengenezwa kwa kupunguza matumizi ambayo pengine yangekuwa muhimu katika utoaji huduma. Hivyo basi kipimo kingine zaidi ya vipimo vya fedha ungeangalia kama kiwango cha huduma na ubora wa huduma.

Ukiangalia utaoji huduma ya umeme hali imekuwa ile na bila ubora kuongezeka. Na kibaya tunapata mgao hata msimu wa mvua tofauti na zamani ambapo tulipata wakati wa kiangazi tu. Muheshimiwa Zitto unaweza kuwa unamwona jamaa ni mzuri na hata ukiongea naye unamwelewa lakini ni kwamba ukiangalia utoaji huduma jamaa hajaweza kufanya kile kitu ambacho ungetaka watu tuamini utetezi wako.
 
Kwa jinsi ninavyofahamu, Dr. Rashid angekuwa one of the best CEO kama ambavyo mnasema basi tungeona performance yake pale Tanesco. Uwezo wa mtu unapimwa na performance yake! Kama mnataka kumtetea kwa kusema eti anaingiliwa na bodi ya wakurugenzi, waziri husika, katibu mkuu na baadhi ya wakurugenzi wizara ya nishati na madini basi angejiuzuru mapema na huo ndio weledi duniani kote!!

Professionalism means meticulous adherence to undeviating courtesy, honesty, and responsibility in one's dealings, plus a level of excellence that goes over and above the commercial considerations and legal requirements. Professionalism is not about your job title or self-proclaimed worth. It is not about self-perception at all. Professionalism is about personal ethics, quality work and a quality attitude.

Na kama kuna mazingira ya watu kukushurutisha ufanye jambo ambalo ni kinyume na wewe unavyoamini, you resign!!

Hata kama Rais atakuomba urudi unampa masharti ya kurudi, akishindwa kukutekelezea you quit!!!

He is just another failure, period!!!!


This is very well said Mkuu, Asante sana na hili ndiyo tatizo kubwa la viongozi wetu. Na ndiyo maana wanaonekana waganga njaa!
Wengi wamo kwenye viti vyao ilimradi liende No satisfaction, completely zero achievements, wanapokea watoto wa wakubwa na kuwapa kazi hata kama hawana sifa. Ni wakati gani watoto wa vigogo walikuwa recruited sana pale BOT?? A mess they are struggling to clean now! Tusitetee marafiki kwenye kujadili maswala ya kitaifa, wacha uhusiano wako na mtu unapojadili mambo yaliyo muhimu na yanayomgusa kila mtu kwenye Taifa zima. Kama watu hawana uvumilivu wa ku-serve the public as an honest civil servant, with integrity should resign and join the private sector.
Warwanda wameshatuacha, wakenya wameshatuacha, sasa tunangoja wakongo sasa hivi watarudi hali ya utulivu nao pia watatuacha tunapiga bla, blaaa isiyojenga nchi yetu.
 
Lets not lose sight here as to what is at stake... ITS INTERGRITY.
Dr Rashid experieced,learned or otherwise has not proven his worth.
When you have carry on baggages like the RADAR scandal and the Serious Fraud Office(SFO)is hounding you, is not exactly one thing to be proud of.
Dr Rashid has not proven to be a character of the caliber of Mr Arnold Kilewo,Mr Mbowe(formely of TIB), Mr Nsekela etc.

Ill intentions in management can kill ones reputation, as is the case with Dr Rashid


Mjomba hayo majina una uhakika na unavyo visema?
Fanya utafiti utajua huko Jersey kuna account ngapi.....
 
Ufisadi wa RADAR kwa mujibu wa makaratasi ya SFO unajadiliwa JF? Au ndio hukumu tayari?
Akamatwe akajibu mashitaka yake huko. Swali litakuja nani amkamate, wananchi tuna nguvu za kusukuma DPP kufungua mashtaka dhidi ya watuhumiwa. Mwishowe itakuwa yale yale ya kila mtu fisadi (unaona hata Sopshia Simba anaona eti michango ya harusi ya ya Jeetu Patel ni ufisadi wa Anna Kilango ili mradi tu kila mtu avikwe shuka ya ufisadi). CEO wa TANESCO sio mwanasiasa, ni mtendaji na hivyo hakuna kilichoitwa ajali ya kisiasa.......!!!!!!!
Tunapogeuza ufisadi ni mijadala ndio tunapoenda mrama. Mpaka sasa ni tuhuma na mahakama ikimtia hatiani hutaniona ninajenga hoja hizi. Lakini kama kuna ufisadi, au tuhuma za ufisadi akafanya TANESCO toka amekuwa CEO pale ziwekwe hapa na sio kutumia visingizio vya SFO kumhukumu mtu katika court za vijiweni.

Kuna vested interest nyingi katika Mashirika na kuna watu wanaona ni zamu yao kula. Ni suala la kuchagua nani iwe zamu yake maana siku hizi media ni silaha za wazi na kila kundi lina media zake. Katika TANESCO kuna zaidi ya tunachosoma katika This Day na Kulikoni au gazeti lingine loote. Kuna watu wanajaribu kuwatake wengine for granted. Wanaweza kufanikiwa lakini maana siku hizi Tanzania ni 'either with us or with Fisadis'

Can this 'not guilty until proved in a court of law' conclusion of yours be extended to Chenge who, as the then Minister responsible for Construction, 'constructed' that road in your Kigoma North Constituency?
 
Integrity nakubaliana na wewe 100%! Mahakama basi ifanye kazi maana tusiwe mahakimu ingawa kuna court of public opinion.

Sina comment on kina Kilewo maana ni watu ninaowaheshimu sana ingawa nao wana mawaa yao. Tulikodisha KIA kwa kampuni ya kiingereza kwa tozo la dola 1000 kwa mwaka na kampuni hiyo mdau wake ni Mzee Kilewo. Unakumbuka lawama kwa Nsekela on ukabila nk. Ndio maana huwa sipendi kuhukumu watu kwa jumla jumla


Muheshimiwa, naona kama unateleza kidogo maana hawa wengine umewavalisha kofia haraka ila Dk unamkingia kifua.

Ukweli ni kwamba Dk ni msomi anayekubalika pia ni mchapakazi anayejua afanyalo ila tatizo linabaki pale pale...Accountability.

Je tumpe pass kwa sababu mahakama haijamuhukumu?......
 
Mimi nilifanya kazi kwa karibu sana na Dr Rashid. lakini all in all itazameni NMB alivyoibeba na hata kuifanya pesa hata BOT kuifanya atleast pesa ya Tanzania kuwa stable ( pitia miaka mitatu kabla kuwa Gavana na miaka mitatu baada ya kuondoka ugavana).

Sasa hivi ni mwenyekiti wa Nafikiri bank ya Azania. Ni mtu anayeaminika sana katika fani ya Finance.

Kila Bin'Adam ana upungufu wake lakini sifa zake lazima tumpe.

Labda sijui siku hizi huko Tanzania. lakini zamani Shirika kama hilo la Umma, Dg ni kama kibarua tu kuna wengi sana wanamkono wao ndani ya shirika na hata DG anapokea maelekezo tu na yeye anabaki kuwa mtekelezaji.
Kuna Waziri, katibu Mkuu, akurugenzo wengi tu wa Wizara nishati, Mwenyekiti wa Bodi , wanasiasa ambao wajumbe wa bodi. hao wote wanamwongoza DG.

Sasa hata akiwa na jipya halina nafasi na yeye kubaki kama mlalamikiwa.

Tukumbuke siku za nyuma alitoa mpaka notice ya kujiuzuru sababu ya wakubwa wengi kumwingilia shughuli zake.

Dr nakuheshimu sana na nakuamini kwa umakini wako...........tumpe mwingine tuone atafanyani?
Naungana nawe, nchi yetu imejaa majungu kuliko uhalisia. Wakati huyu bwana anachukua shirika jiulize lilikuwa linapata loss kiasi gani? Imagine sasa hivi linakaribia ku brake even. Lini hiyo imetokea? Shirika linakopesheka sasa hivi. Suala la mgawo wa Umeme kwa hali shirika lilivyokuwa lisingeweza kumalizika ndani ya kipindi kifupi hiki maana alilichukua lipo hoi. Mgawo wa Umeme zinahitajika jitihada kubwa zaidi na si za TANESCO peke yake kwa kuzingatia lilipokuwa.
 
Heri mwananchi wa kawaida hana muda wa kumpima Dr. Rashid kwa vigezo vya kutowapa posho mbili mbili wabunge or the likes. Kipimo chao ni kimoja tu...Je Tanesco wanawapatia umeme wa kutosha katika kipindi chote cha mwaka kwa bei competitive???

Kwa taarifa tu, mfumuko wa bei umefikia 'double digit' na sababu kubwa inayoelezwa ni kukosekana kwa umeme kulikosababisha wazalishaji nchini kutumia nishati ya mafuta ambayo ni ghali zaidi na hivyo kupelekea kupandisha bei bidhaa wanazozalisha!!!
Double digit haijachangia na umeme pekee kama unavyodai. Uganda na Kenya ni umeme? Huoni kwamba hizo nchi zipo correlated na Tanzania. Hali ya chakula kwa kiasi kikubwa ndio imetufikisha hapa na kuyumba kwa soko la dunia.
 
By ThisDay Reporter
25th November 2009
Dr. Rashid

An intense lobby is underway for the reappointment of current Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) Managing Director Dr Idris Rashidi to continue in the post despite mounting allegations against him, THISDAY has learnt.

Rashidi's contract is scheduled to expire this month after serving at the helm of the state-run power utility for the past three years. His is a presidentially-appointed position.

Among various other things, the former Bank of Tanzania (BoT) governor has been named by Britain's Serious Fraud Office (SFO) over alleged involvement in the military radar scandal.

1)Rashidi himself was recently quoted as saying that he plans to retire from the troubled power company once his current contract expires, and has no interest whatsoever in extending the contract.

But well-placed sources have now told THISDAY that various individuals who may have influenced his initial appointment to the TANESCO position back in 2006, are now seeking to ensure he continues as MD and thus maintain a 'status quo' at the company.

2)Rashidi was appointed as TANESCO chief executive officer at the height of the Richmond power generation scandal.

According to these sources, the TANESCO board of directors chaired by Peter Ngumbulu has already formally recommended the re-appointment of Rashidi - but under controversial circumstances.

"As far as I understand, the (TANESCO) board has sent its recommendation in favour of Rashidi to President (Jakaya) Kikwete...but this was done without the consent and consensus of all members (directors) of the board," an official close to the power utility told THISDAY.

Ngumbulu was yesterday not available for comment on the implication of a split amongst TANESCO board members (directors) over the Rashidi issue, while acting board chairman Adolar Mapunda flatly declined to comment.

"I can't comment anything on that. Talk to the board chairman (Ngumbulu)," said Mapunda when reached by THISDAY.

Other members of the TANESCO board of directors are Victor Mwambalaswa, Agnes Bukuku, Juma Bakari, Vintan Mbiro, Semindu Pawa, Beatus Segeja, and Ngosi Mwihava.

Various government insiders have strongly suggested that the fact that Rashidi is the target of a serious corruption investigation into the military radar transaction should be enough to disqualify him from continued public service.

"He (Rashidi) obviously lost all credibility to be the head of TANESCO after being interrogated by SFO officials over his role in the radar corruption scandal," said one government official.

3)Apart from the radar corruption investigation, Rashidi is also widely believed to have "displayed major leadership weakness", in the words of another government insider, in pushing so hard for the purchase of rusty power generators from Dowans Holdings AS which inherited the Richmond contract.

The Ministry of Energy and Minerals is also understood to have been looking into allegations that Rashidi personally ordered the costly rehabilitation of houses owned by TANESCO, so he could purchase the property cheaply from the public utility.

More recently, the TANESCO boss has been roundly criticized by the parliamentary energy and minerals committee, and the public at large, over the passive manner in which the public utility has handled ongoing power blackouts.

4)Rashidi famously declared that he would neither accept responsibility nor blame for the rolling power blackouts, simply because his controversial plans to purchase the second-hand Dowans turbines at a highly-inflated cost were rejected.

It has been reported that more than 50 individuals had applied for the soon-to-be vacant post of TANESCO managing director by the application deadline of October 2 this year.

A special committee formed by the TANESCO board of directors to process the applications is understood to have come up with a short-list of three names.

Board chairman Ngumbulu was recently quoted by a government-owned newspaper as showering lavish praise on Rashidi and asserting that the controversial MD had enough merits to re-apply for the job.

These comments have raised speculation in government circles that Ngumbulu, as board chair, is among those in favour of Rashidi's re-appointment.

What is wrong with this guy??? So much allegation without proof!!! Is it true or majungus???

Ukiweza kusoma btn the lines nakuwa burudani sana kwani you can see the whole picture.

1)Moja kama nilivyoweka kwenye red highlights,Rashid alidhani kazi yake aliyopelekwa kuifanya imekwisha,he was wrong kwani mambo yalibadilika....Naamini kuwa yalibadilika kwasababu inavyoonyesha kwenye highlights namba..

2)Kuwa aliajiriwa makusudi ili kuja kusawazisha issue za kina Richmond AKA Dowans.

3)Inawezekana weakness zake ndio nguzo kuu muhimu ya kung'ang'aniwa na status quo.
4)Ni yao ilikuwa ni kuuwa issue ya Richmond na alishasema mwanzoni kabisa kuwa yeye hawezi kulaumiwa,inadaiwa hataki politics,lakini anacheza politics,kwa kutotaka kulaumiwa na huku ukweli huu umeonyesha ana msimamo gani na ni kwanini status quo bado wanamuhitaji...

Rashidi is also widely believed to have "displayed major leadership weakness", in the words of another government insider, in pushing so hard for the purchase of rusty power generators from Dowans Holdings AS which inherited the Richmond contract.

"Merits" amabazo zimemconvince board chairman Ngumbulu kumu endorse kwa mara nyingine tena....
Kwa kifupi there is something in common for those who wants Dr Rashid back,something to do with the status quo.
Kaazi..
 
Huu utetezi anaoufanya muheshimiwa kabwe unaonyesha kuwa kuna mengi yamejificha nyuma ya hili sakata la Tanesco na Rashidi. Ni wazi kuwa kwa nafasi yake kuna mengi anayajua ingawa hapa anakuwa mnyimi kutumwagia. Muheshimiwa tuambie nini kinaendelea huko maana tumechoka na hii tabia ya kuchaguliwa kila kitu na magazeti yaliyojaa vibaka wanaosubiri zamu yao nao wawe mafisadi.

Mimi siku hizi nimepata allergy na magazeti ya kitanzania. Imefika hatua wamiliki na waandishi wao wanajifanya kuwa ndio wenye akili kuliko watanzania wote kuanza kuwachagulia kuanzia nani ashike madaraka yale, nani ni mwema na nani mbaya jukumu ambalo hata mitume ya wazungu na waarabu iliwashinda, hadi sasa wanadai kuwa wao ndio wanajua nini iwe ajenda ya taifa letu.

Sasa waheshimiwa kama huyu Mheshimiwa Kabwe anapokuja hapa ni wajibu wake kutupa ukweli wote na sio kutudondoshea vichengachenga tu hapa.

Mheshimiwa ujana dawa ya longolongo la wazee. Tuambie nini kinaendelea huko Tanesco na huyu rashidi. Kwa nini unadhani ni bora kuwa naye yeye kuliko hao wengine wanaotakiwa wawe na hizo vested interests?
 
Other members of the TANESCO board of directors are Victor Mwambalaswa, Agnes Bukuku, Juma Bakari, Vintan Mbiro, Semindu Pawa, Beatus Segeja, and Ngosi Mwihava.

Hivi hawa wote kuna hata mmoja mwenye ABC za mambo ya umeme?

Tunaendekeza ukada wa CCM ktk utaalamu ndo maana nchi haiendi popote. Board ya shirika kama TANESCO inatakiwa iwe na members ambao ni wahandisi, wachumi, wanasheria basi. Sasa ukiangalia members wengi wa bodi za mashirika mengi ya umma unakutana na vihiyo kibao.
 
Back
Top Bottom