Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,776
- 2,389
mwandoshi wa makala hii toka gazeti la kulikoni yumo hmu janvini na huwa hachangii mada, kzi yake ni kuandika maoni ya watu kisha kupleka gazetini, na hawa kulikoni huwa hawana jipya habari zao zote 97% huwa zinatoka hku janvini then wanasema ''uchanbuzi wa kina''
Nawapongeza Kulikoni kukubali kuwa JAMIIFORUMS sasa ni uwanja wa kuchota mawazo, badala ya kuwashambulia mimi naona tuwa-incourage maana itwafanya watanzania wengi wasiojua kuwa kuna jamvi hapa watakuja na wakija tutapata tija ya mabadiriko tunayoyataka. Magazeti mengine igeni Kulikoni njooni hapa mtapata news Bin Newz
Nashangaa mawazo ya Zitto ni kama ya rais vile akisema kitu basi kinakuwa,....this sense of inferiority imetuweka wazi sana watanzania tulivyo. vita ya maneno na mawazo mapya watu waoga hivi ndio maana hata EAC hatutaki!
sad and shame.
Kuandika habari kutoka JF sio tatizo na inasaidia kutangaza JF. Hata hivyo kuandika habari maliciously kutatufanya wengine tuogope kutoa mawazo yetu kwa uhuru humu katika jukwaa letu.
Habari hii imeandikwa kwa nia mbaya.
Zitto
Mwandishi amesema habari katoa jamii forums.kunanini wadanganyika?tujadili ya Zito je rashidi pekee ndo bora aendelee au awapishe wengine?Kama kuna data watu washushe humu.kwanini aendelee au kwa nini asiendelee. NDO hoja hiyo.Siyo mwandishi jamani.Na ubora wa mtu tuangalie alipo ingia unit za umeme zilikua ngapi na sasa ni ngapi. Mgao wa umeme je ulikuwa ni mara ngapi kwa wiki au mwaka je nasasa hali ikoje.sisi mapato ya tanesko hayatuhusu. garama ya umeme umepada au kupungua.ina maana KULIKONI hawana jina la MWAANDISHI ? wanaogopa nini?
oili inamaaan hawa kulikoni hawawezi kuandika JAMIIFORUMS.COM
its about tgime wan JF mkahit back on these people
Hivi Tina ni nani aliyekwambia kuwa huyu Zitto wa JF ndiyo mbunge?Ndg. Kibunango, Je ni meneno gani ambayo gazeti limemnukuu vibaya Zitto? Tuwe makini na sweeping statements, mimi nimefuatilia kwa makini mjadala wa JF kuhusu Dk. Rashidi. Kulikoni imenukuu verbatim (neno kwa neno) michango aliyoitoa Zitto kwenye JF. Naomba upitie habari ya Kulikoni kwa makini utuonyeshe ni maneno gani Zitto amekuwa misquoted. Ni vizuri tukajenga hoja kwa facts kuliko kutoa sweeping statements.
Hivi, Zitto anaposema kuwa Rashidi ni one of the best CEOs wa Tanzania. Akatoa track record yake alipokuwa BoT na kumwagia sifa tele za "msimamo" wake wa kukataa kuburuzwa na wanasiasa. Tena akatumia takwimu ambazo bila shaka amezipata kupitia cheo chake kama m'kiti wa kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma na kusema kuwa eti Rashidi ameweza kuboresha hali ya kipato ya Tanesco. Sifa zote hizi kede kede zimetolewa kukiwa na mjadala mkali juu ya Rashidi na hatma yake. Je, ni upotoshaji au uandishi uchwara au malice kusema kuwa Zitto ampigia debe Rashidi? Wote tumeshuhudia humu kwenye JF how Zitto went out of his way to shower lavish praise on Rashidi.Jumuisho la yote kwa mwandishi wa habari hiyo ni kwamba Mh. Zitto anampiga debe Dr. Rashid ilhali Mh. ametoa ufahamu wake juu ya utendaji kazi wa Dk. Rashid.
Huu ni upotoshaji wa wazi waliofanya KULIKONI, kumbuka kwamba Mh. Zitto alikuwa akijibu hoja za baadhi ya wajumbe waliokebehi utendaji wa kazi wa Dr. na sio vinginevyo.
Hebu pitia tena hiyo habari uone ilivyo bias km inania njema katu isingekebehi na kuunga ishu na kuchanganya mada. Mbona hoja alizotoa Zitto hazipo wazi? Lakini hata hivyo Kulikoni imekuwa ikiandika saana kuhusu Rashid ilikuwa ni lazima habari iwe vile ili wasijicontradict na makala zao za siku za nyuma.Hivi, Zitto anaposema kuwa Rashidi ni one of the best CEOs wa Tanzania. Akatoa track record yake alipokuwa BoT na kumwagia sifa tele za "msimamo" wake wa kukataa kuburuzwa na wanasiasa. Tena akatumia takwimu ambazo bila shaka amezipata kupitia cheo chake kama m'kiti wa kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma na kusema kuwa eti Rashidi ameweza kuboresha hali ya kipato ya Tanesco. Sifa zote hizi kede kede zimetolewa kukiwa na mjadala mkali juu ya Rashidi na hatma yake. Je, ni upotoshaji au uandishi uchwara au malice kusema kuwa Zitto ampigia debe Rashidi? Wote tumeshuhudia humu kwenye JF how Zitto went out of his way to shower lavish praise on Rashidi.
Kuhusu gazeti la KULIKONI ku pick mjadala wa JF na kuandikia habari, nadhani ni jambo la kusifiwa na kuigwa kwani linathibitisha kuwa JK ni Home of Great Thinkers kweli na vile vile linasaidia kuleta umaarufu zaidi kwa JF na kusambaza mijadala ya humu ndani kwa umma wa Tanzania. Tukumbuke kuwa ni asilimia chache sana ya Watanzania wenye access ya Internet. Long live JF, magazeti muwe huru kusambaza mijadala ya JF ili Watanzania wote mijini na vijijini waweze kuchangia mawazo yao.
Dr Rashid ninayemfahamu
Kwa bahati nzuri nimeshiriki katika kazi maalum ya pale TANESCO wakati wa kipindi cha NET Group na baada kuingia kwa Dr Rashid pia. Watanzania tuache uchafuzi wa CVs za watu pasipo kuwa na uhakika. Kuna mabadiliko makubwa sana ambayo Rashid ameyafanya ndani ya TANESCO, ambayo ni mazuri na makubwa. Rashid alikabidhiwa mkoba wa lile shirika ukiwa na pumzi inayokaribia kufa. Jambo la kwanza la kuangalia, tazama hati za ukaguzi wa mahesabu za sasa zinazofanywa na kampuni moja ya kimataifa, (Audited financial statements) ambayo imekuwa ikikagua kampuni hiyo tangu wakati wa NETI Group. Utaona kuna mabadiliko makubwa sana. Kutoka Adverse opinions/Disclaimer opinions hadi sasa utaona atleast Qualified opinions. Ukweli ni kwamba Dr Rashid ni kati ya ma CEO makini na wazuri katika nchi hii. Ndiyo, upende usipende, pamoja na kelele nyingi na mapungufu yanayoweza kujitokeza, bado Dr Rashid ni CEO makini. Kwa wanao ongea kwa kutazama maandishi ya kwenye magazeti tu, hawawezi kuelewa!.
Siasa zinapokuwa zimeingia katika professionalism ndipo tunaona kupakwa kwa kinyesi kwa Dr Rashid. Tatizo letu wa TZ mambo ambayo yanahitaji wataalamu tunayawekea kimbelembele cha siasa, hata pasipohitajika!. Tangu tuhuma za Rashid zianze siyo leo, lakini kila siku ni tuhuma tuhuma tuhuma tu!. Hata wasiokuwa na data, ni tuhuma tu.
Jambo la pili, tazama hata maendeleo ya baadhi ya makampuni ambayo Dr Rashid anayasimamia kama Mwenyekiti wa Bodi, kwa mfano benki ya Akiba, tazama miaka miwili ambayo huyu mzee wetu Rashid ameingia kwenye board na kupewa uenyekeiti wa bodi, amefanya mabadiliko makubwa na tunaona benki hii ni kati ya benki ambazo zinakua na kufanya mabadiliko makubwa katika technolojia na utendaji pia, hapa nchini.
Tatizo letu wa TZ tunachonga sana hata pasipokuwa na data za kutosha kuendeleza mchongo!! Utakuta mwandishi wa habari au M- TZ mwenzangu, yeye pekee ni prosecutor, yeye huyo ni Forensic expert, yeye ni Auditor, yeye ni Engineer, yeye Mhasibu nk, huu ni mtazamo hasi. Lazima tufike mahali tuwe tunachonga kwa data, pale panapohitajika, si kuchonga tu!. Tunawasaidia wafanyabiashara kuuza magazeti bure!!. hali wengine wakisubiri pesa za wananchi zitumike kuwanyamazisha kuendeleza uandishi wa habari usiokuwa na tija na uliojaa udaku udaku tu!. Magazeti mengi yanajifanya yanaandika habari za uchunguzi, lakini ukisoma utaona ni UDAKU TU!. Soma hata habari hii ya Thisday, hapo juu; kwa umakini, utaona hakuna investigative journalism inayoonekana katika makala hiyo, zaidi ya kujaa udaku udaku tu!; See this "According to these sources, the TANESCO board of directors chaired by Peter Ngumbulu has already formally recommended the re-appointment of Rashidi - but under controversial circumstances............Ngumbulu was yesterday not available for comment on the implication of a split amongst TANESCO board members (directors) over the Rashidi issue, while acting board chairman Adolar Mapunda flatly declined to comment". Sasa kama hawa Thisday walikuwa wamemkosa Ngumbulu, walikuwa na haraka gani ya kuileta hii habari gazetini, kabla ya kupata uhakika wa taarifa hizi. Hata habari yenyewe haielezi, what are the contravential circumncistances.... Huu ni ubabaishaji katika uandishi wa habari. Hebu angalia, Sources za habari hawajatueleza, hata hizo contravential circumncistances hawajaeleza. Maana yake ni kwamba, sources na taarifa zenyewe wanazotaka kutuhabarisha hawazijui. Isipokuwa wanataka kuuza gazeti tu!
Ninachokiona na ambacho waandishi wengi wa habari wanakosa, ni "Report Writing Skills". Pia ninadhani, wahariri wengi, hawana uwezo mzuri wa kukaachini na kuhariri habari vyema. Pia waandishi wa habari waelewe kwamba kuwa mwandishi mzuri wa habari kunahitaji kuwa na skills zaidi ya taaluma ya uandishi wa habari. Wajitahidi waongeze taaluma, mbalimbali ambazo zitawafanya wawe wanaelewa namna shughuli zinavyofanywa katika makampuni na mashirika. Si ajabu kumkuta mwandishi wa habari aliye andika habari hii katika Thisday, hajui hata Corporate Governance, hajui hata namna masuala mbalimbali yanavyosimamiwa na kutekelezwa katika mashirika na makampuni. Yeye alivyoambiwa Ngumbulu hayupo, basi, akaona ndiyo mwisho wa fikira! Akakimbia kwenda kwenye mtambo kupeleka habari eti Habari hizi nilizoziandika ngumbulu hakupatikana kuthibitisha!!. Hata asijue kwamba suala kama hili ni sensitive, linalohitaji umakini katika kulitolea taarifa kwa maslahi ya taifa. Tatizo wanatoa taarifa kama WANAVYOPEANA TAARIFA ZA MISIBA!!.
Nadhani Thisday nao wamepoteza mwelekeo!! They are more of Majungu, kuliko investigative journalism wanayoiimba kila kukicha!
"For actions speaks louder than words, let us embrace actions more than words!!!!!"
Huyu mwandishi amefanya vibaya, wala asiwepo mtu wa kumtetea. Endapo angekuwa fair angetaja hoja za Zitto kumtetea Dr. Rashid, yeye amechukua one side of the story.
Tatizo la media za bongo, zimegawanyika katika makundi yaani zinazotetea mafisadi na kuwalima wapiganaji na zile zinazowalima mafisadi na kutetea wapiganaji. so, hii ni vita btn media groups na masalahi binafsi.
Hata hivyo, nikuambie Mhe. Zitto kwamba upande uliouchagua ktk hii issue ya umeme unachangamoto nyingi kuliko fursa. Ingekuwa ni SWOT analysis ingebidi uachane kabisa na hii issue.
Kwanza binafsi ZITO AMEKUA mtata sana kwenye sakata hili lote la umeme Tanzania, kujitokeza kwake hadharani mara kwa mara ni kielelezo cha namna anavyotetea kile anachokiamini ama anachodhani ni sahihi, ama kwa kudanganywa ama kwa utafiti wa kina wa sakata hili lote. yeye amekua akitoa hisia zake bila hofu yoyote....hii ninzuri.
Kuhusu mwandishi anaeficha identity yake kwenye swala ambalo limejadiliwa hadharani humu Jamvini ni upuuzi, ninahisi kua amewadanganya mabosi wake kua amefanya uchunguzi wa sakata hilo kisha akangundua mambo hayo, wakati reality ni kua zito alikua live humu jamvini akijieleza juu ya kwanini anaamini Dr Rashidi ni mtendaji mzuri na sio mtu wa hovyo-hovyo kama watu wengi wanavyodhani.
Mimi naamini Dr Rashid ni kiongozi wa hovyo kabisa, natatizwa hata na elimu yake, ingawa kuna mtu amenithibitishia hapa kua ,ni msomi wa aina yake mwenye kichwa makini na mjuzi aliepevuka katika mambo ya kitaaluma....
sasa kwa kushindwa kwake inaonekana alikariri darasani ama alifanya kusudi ili apate kamuhogo kake. mambo haya.
Mjadala huu umeonesha huku JF kuna wababaishaji kadhaa na wengi wanaohitaji kupisha mijadala wasioyoijua vyema. Mosi, KULIKONI limeatribute vizuri tu kwani naambiwa hata taaluma ya habari inasema gazeti likinukuu gazeti jingine au chombo kingine cha habari ni vyema likatajwa linalotumika kama chanzo na hii ni kawaida kitaaluma.
Hao jamaa wa KULIKONI ni wapambanaji kama sisi JF (labda leo tujitangaze kuwa si wapambanaji) na mambo mengi waliyoyaibua ndio tumeyajadili sisi hapa na pale nasi tulipoibua jambo nao wamekuwa wakiyasimamia. Hata hili la Rashid walilianza wao na THISDAY ndipo likaja kujadiliwa hapa.
Zitto huna haja ya kutoka JF, ulichangia mjadala kwa kuonekana ukitumia vyeo vyako vyote vya ubunge na kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ndio maana baadhi ya takwimu ulizitoa katika kumtetea Dk Idris zilitokana na hesabu zilizowasilishwa katika Kamati yako.
Hili pia ni fundisho kwako na nakumbuka uliwahi kushauriwa na mwanaJF mmoja kuhusu misimamo unayojiamini kuwa nayo kuwa wakati fulani inahitaji kupitiwa kwa makini.Labda ungekuwa na wataalamu wa mawasiluiano ya umma kwa karibu wangekusaidia nini cha kusema wapi na wakati gani.Lakini ukiacha hilo gazeti msimamo wako wa jana uliwashangaza wanaJF wengi.
Mara kadhaa ulitetea wazi humu kuwa Dk. Idris ni makini na mtawala mweledi, sasa unaogopa vipi kivuli chako jamaa walipoandika ulichokisema hasa kwa kuzingatia ulikotoka na misimamo yako ya nyuma ukiwa mpinga mafisadi, leo mafisadi unawaona most competent?
Mmeshaanza kuandika utumbo wenu sasa...!Hivi bado hamjamstukia dogo Zitto alikwishatekwa na mafisadi siku nyingi.
Mmeshaanza kuandika utumbo wenu sasa...!
Kibs Umemwona Chairman wako akibembea kule Jamaica....."angechoka" ghafla ingekuwaje pale LOL