TANAPA yawasili visiwani Zanzibar kunadi vivutio na fursa za uwekezaji

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
9d55c812-800a-42ab-b4a8-9ede091c88c5.jpeg

Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) wamewasili Visiwani Zanzibar kushiriki kwa mara ya kwanza Maonesho ya Biashara ya Kimataifa yaliyofunguliwa tarehe 10.01.2024 na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussen Ali Mwinyi eneo la Dimani - Fumba Zanzibar ili kunadi vivutio na fursa za uwekezaji zinazopatikana ndani ya hifadhi hizo zilizoenea takribani mikoa yote ya Tanzania Bara.

Akifungua Maonesho hayo, Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Hussen Mwinyi alisema, "Mbali na maonesho hayo kuwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar pia ni fursa adhimu ya kuwakutanisha wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi kubadilishana uzoefu na kujua masoko mapya ya biashara na utalii".
498697ca-402f-4c95-8fe8-e9e8cbe7140c.jpeg

798020e2-3cb8-4f74-abbc-94104879e393.jpeg
TANAPA wakiwa katika banda lililonakshiwa kwa vipeperushi, vitabu na mabango yanayoonyesha vivutio na aina mbalimbali ya utalii unaoendeshwa ndani ya hifadhi hizo, Afisa Mwandamizi Kitengo cha Utalii - Kanda ya Mashariki Apaikunda Mungure alisema, "TANAPA tumekuja kimkakati zaidi kwani tumekuwa wanufaika wakubwa wa soko hili kwa maana ndege kadhaa kutoka Zanzibar zimekuwa zikishusha watalii wengi katika Hifadhi za Taifa Nyerere, Mikumi, Ruaha na Saadani".

"Aidha, tumeshuhudia watalii wengi wanaopenda fukwe wakiwasili Zanzibar kwa wingi, hivyo tutatumia fursa hii ya maonesho kuongea na Makampuni ya Utalii, Mawakala wa usafirishaji na waongoza watalii wa Zanzibar wawe na vifurushi vya kutembelea Hifadhi za Taifa zilizoko Tanzania Bara", aliongeza Afisa Mwandamizi huyo.

TANAPA inayoshiriki maonesho hayo ya Kumi kwa mara ya kwanza Visiwani Zanzibar, inawakilishwa na Maafisa na Askari kutoka Kanda za Mashariki, Kusini, Nyumba ya Kumbukizi ya Mwl. Nyerere iliyopo Dar es Salaam na Caravan Serai - Bagamoyo.
 
Back
Top Bottom