chuki
JF-Expert Member
- Mar 10, 2011
- 2,715
- 533
Katika hali isiyo ya Kawaida tarehe 17/01/2020 TANAPA na TAWA wameingizwa mkenge na Mbunge wa jimbo la Bunda Vijijini Bonifasi Mweta Getere kwa kulipa wajumbe wa ccm ambao walikuwa wameitwa kwa kampeni za mbunge huyo.
Katika shughuli hiyo Rushwa ilikuwa wazi kwani Wajumbe zaidi ya 500 wamelipwa shilingi 50,000/- na 100,000/- kwa kigezo kuwa wamehudhuria usomaji wa utekelezaji wa Ilani.
Pesa hizo zote zimelipwa na TANAPa kwaajili ya kumpendelea mbunge huyo ili apitishwe kura za maoni.
Alipoulizwa kwanini anatumia mashirika ya umma vibaya alisema hakuna wa kumfanya kitu kwani yeye ni mjumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira na anajuana nao kwani kuna madili mengi '' wanakula" wote.
Katika mkutano huo baadhi ya viongozi wa mkoa na wilaya wa ccm wamealikwa na kugawiwa 'posho' nono ili kubariki 'ubatili' huo.
Kwani hakuna kikao cha namna hiyo cha kusoma Ilani na hakuna utaratibu huo kikanuni na kikatiba.
Katika maelezo yake mbunge amekiri kuwa amealika kikao cha 'kuwafurahisha' wajumbe ili wamkumbuke hapo baadae.
Upande wa Tanapa wanadai walikuwa wanatoa semina, hivyo kuhitimisha kuwa ni mkakati wa Rushwa ya wazi kwaajili ya kumbeba mbunge.
My take: Kwakuwa hii ni Rushwa na Uhujumu Uchumi, Vyombo vya Dola wawahoji Tanapa kwanini wanatumia vibaya Mfuko huo wa umma kwa manufaa ya mtu.
Chama cha Mapinduzi kiwahoji viongozi kwa kupokea malipo batili na kanuni ipi imeongoza kuitisha mkutano ukijumuisha wapiga debe na watu wasio wana ccm kusoma Ilani katika jimbo moja .
Rushwa Bunda ni kama samaki na Maji.
Katika shughuli hiyo Rushwa ilikuwa wazi kwani Wajumbe zaidi ya 500 wamelipwa shilingi 50,000/- na 100,000/- kwa kigezo kuwa wamehudhuria usomaji wa utekelezaji wa Ilani.
Pesa hizo zote zimelipwa na TANAPa kwaajili ya kumpendelea mbunge huyo ili apitishwe kura za maoni.
Alipoulizwa kwanini anatumia mashirika ya umma vibaya alisema hakuna wa kumfanya kitu kwani yeye ni mjumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira na anajuana nao kwani kuna madili mengi '' wanakula" wote.
Katika mkutano huo baadhi ya viongozi wa mkoa na wilaya wa ccm wamealikwa na kugawiwa 'posho' nono ili kubariki 'ubatili' huo.
Kwani hakuna kikao cha namna hiyo cha kusoma Ilani na hakuna utaratibu huo kikanuni na kikatiba.
Katika maelezo yake mbunge amekiri kuwa amealika kikao cha 'kuwafurahisha' wajumbe ili wamkumbuke hapo baadae.
Upande wa Tanapa wanadai walikuwa wanatoa semina, hivyo kuhitimisha kuwa ni mkakati wa Rushwa ya wazi kwaajili ya kumbeba mbunge.
My take: Kwakuwa hii ni Rushwa na Uhujumu Uchumi, Vyombo vya Dola wawahoji Tanapa kwanini wanatumia vibaya Mfuko huo wa umma kwa manufaa ya mtu.
Chama cha Mapinduzi kiwahoji viongozi kwa kupokea malipo batili na kanuni ipi imeongoza kuitisha mkutano ukijumuisha wapiga debe na watu wasio wana ccm kusoma Ilani katika jimbo moja .
Rushwa Bunda ni kama samaki na Maji.