TANAPA kuweni serious kidogo!!!!

TANAPA kuweni serious kidogo!!!!

Infopaedia

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2011
Posts
1,231
Reaction score
1,495
Tanapa mmetangaza nafasi za kazi, ni vizuri. Lakini mnataka waombaji wote watume maombi yao kupitia 'online application system'.

Sijaona option nyingine ya kutuma maombi zaidi ya hiyo. Hivi huwa mnatathmini kweli hali ya Tanzania na watanzania?. Online application system huwa zina mlolongo mrefu, kama sio mzoefu ni nadra sana kufanikiwa kupitisha maombi yako.

Mtoto aliyesoma wildlife management pale Pasiansi, akarudi Bariadi kusikilizia hizo ajira, leo umwambie akapambane na online application system ataweza kweli???.

Maombi kwa barua pepe ndio njia ambayo asilimia kubwa ya vijana wanamudu, hata kwa usaidizi. Tanapa ni mali ya uma, iwe inafikiria uma wa watanzania. Au kwavile mnapokea wazungu kwa wingi basi mnahisi Tanapa ni ya wazungu!!!.

Nimeshuhudia wahudumu wa internet cafe na maduka ya stationary wakishindwa kuwasaidia vijana kutuma maombi kwenye hiyo 'online system' ya Tanapa.

Sehemu ya Qualification, kuna eneo inabidi u-select result kutoka kwenye drop down menu. Lakini hiyo drop down menu haina chochote na wala huwezi andika chochote.

Na bila kujaza result huwezi endelea mbele kutengeneza profile yako ambayo ndio utaitumia ku-apply hizo nafasi. Tanapa hebu rekebisheni hiyo system, au toeni maelekezo.

Tunajua mme-out source hiyo online application system kama njia tu ya kupigia hela za umma. Tanapa haina mahitaji hayo. Mna ofisi ya rasilimali watu ambayo inaweza ikaratibu mchakato mzima wa ajira mpya.
 
Mkuu wazo lako ni zuri ila kwa dunia ya leo online application haikwepeki
Tafuta wataalamu watakusaidia(wapo wenye ujuzi hasa mjini).
Nakuelewa sana Sir Khan, lakini kwa shirika la umma wa watanzania Tanapa, bado hatujafikia hatua ya kuwa na option moja tu ya online. Sipingi uwepo wa online system. Kuwe na online, pia kuwe na option nyingine kama baruapepe, nk. Swala jingine hata hiyo online system yenyewe ni mbovu kama nilivyoeleza. Hata upate mtaalamu gani, kama system haikuruhusu kujaza kipengee fulani, huyo mtaalamu ata-fail tu.
 
Survival of the fittest usaili unaanzia hapo yakikushinda umeaga mashindano mapema tu with the fast moving world you can not avoid such means of applications. Selection ya candidates ni automatic hawana muda wa kupitia CV yko CV hutumika pale unapofikia hatua ya oral so pambana sna
 
Nadhani wameanza kupunguza washiriki kwa namna hiyo
Wenye uhitaji wa kweli watapambania
 
Nakuelewa sana Sir Khan, lakini kwa shirika la umma wa watanzania Tanapa, bado hatujafikia hatua ya kuwa na option moja tu ya online. Sipingi uwepo wa online system. Kuwe na online, pia kuwe na option nyingine kama baruapepe, nk. Swala jingine hata hiyo online system yenyewe ni mbovu kama nilivyoeleza. Hata upate mtaalamu gani, kama system haikuruhusu kujaza kipengee fulani, huyo mtaalamu ata-fail tu.
hapo jaribu kutembelea ofisi zao,unapoendelea kutupa lawama wenzako wanajiongeza utashangaa nafasi zimejaa.
Come on madam
 
Survival of the fittest usaili unaanzia hapo yakikushinda umeaga mashindano mapema tu with the fast moving world you can not avoid such means of applications. Selection ya candidates ni automatic hawana muda wa kupitia CV yko CV hutumika pale unapofikia hatua ya oral so pambana sna
well said, maana dunia ya sasa kubaki kuendekeza UJIMA ni jambo la fedheha sna. Hatuwezi kuishi kwa mazoea hata siku moja moja.. ndoman uhakiki wa vyeti vya kuzaliwa umekua simple sna.
sio mtu yupo uvinza anawaza apande bus aende dar akahakiki wakati bundle la 500 tu linatosha kukamilisha kila kitu
 
Tanapa mmetangaza nafasi za kazi, ni vizuri. Lakini mnataka waombaji wote watume maombi yao kupitia 'online application system'. Sijaona option nyingine ya kutuma maombi zaidi ya hiyo. Hivi huwa mnatathmini kweli hali ya Tanzania na watanzania?. Online application system huwa zina mlolongo mrefu, kama sio mzoefu ni nadra sana kufanikiwa kupitisha maombi yako. Mtoto aliyesoma wildlife management pale Pasiansi, akarudi Bariadi kusikilizia hizo ajira, leo umwambie akapambane na online application system ataweza kweli???. Maombi kwa barua pepe ndio njia ambayo asilimia kubwa ya vijana wanamudu, hata kwa usaidizi. Tanapa ni mali ya uma, iwe inafikiria uma wa watanzania. Au kwavile mnapokea wazungu kwa wingi basi mnahisi Tanapa ni ya wazungu!!!.
Nimeshuhudia wahudumu wa internet cafe na maduka ya stationary wakishindwa kuwasaidia vijana kutuma maombi kwenye hiyo 'online system' ya Tanapa. Sehemu ya Qualification, kuna eneo inabidi u-select result kutoka kwenye drop down menu. Lakini hiyo drop down menu haina chochote na wala huwezi andika chochote. Na bila kujaza result huwezi endelea mbele kutengeneza profile yako ambayo ndio utaitumia ku-apply hizo nafasi. Tanapa hebu rekebisheni hiyo system, au toeni maelekezo. Tunajua mme-out source hiyo online application system kama njia tu ya kupigia hela za umma. Tanapa haina mahitaji hayo. Mna ofisi ya rasilimali watu ambayo inaweza ikaratibu mchakato mzima wa ajira mpya.
Watanzania kwa kulialia hatujambo.

2018 karne ya 21 bado mtu unalalamika kufanya online application?

Vibanda vya internet kibao, simu janja kibao, tablet, iPad.

Online application ndio njia rahisi kuliko zingine, inaokoa gharama, inaokoa muda, mpaka mtu aliyeko remote area anaweza kufanya hili kwa unafuu kidogo kuliko ungesema watume kwa posta maana kuna sehemu kupata ofizi za posta ni mtihani.
All in all dunia imebadilika hebu tubadilike, huyo mtoto aliyesoma Pansiansi sio kilaza kiasi cha kushindwa kujua email, kujua kujaza online application kwenye mfumo wa Tanapa, kujua ku-scan vyeti n.k
Kama mfumo wa Tanapa unasumbua basi ni suala la kuwambia Tanapa waweze ku-resolve mbona hayo mambo ya kawaida sana hata TCU inasumbua mara kibao, UDSM inasumbua mara kibao, Necta, Nacte n.k
Tuache kulialia, tungeambiwa kutuma kwa EMS bado tungelilia gharama
 
Competence ya kutumia ICT ni moja ya vigezo muhimu karne hii ya 21. Na vyuo vinapaswa kufundisha ICT. Application zote za vyuo ni ICT based. Sasa ndo iwe ajira. Kuna faida nyingi za kutumia teknolojia. Mfano umetangaza nafasi za kazi 5 halafu waka apply watu elfu moja. Kupitia mfumo wa ICT unaweza ukaanza mchujo wa mwanzo, mfano wale ambao hawakusubmit cheti chochote au hawakutimiza masharti fulani. Secondly unaweza ukafanya aptitude test online kwa mchujo mwingine. Na tunapoelekea machine learning inaweza ikatumika kupima ubora wa barua yako ya maombi na kuchuja. Faida moja ya mashine ni kwamba inaweza kupunguza bias ya kibinadamu. Kwa kusema hayo namaanisha kwamba tusiigope sana teknolojia kwa maana ndo tunakoelea huko
 
Tanapa mmetangaza nafasi za kazi, ni vizuri. Lakini mnataka waombaji wote watume maombi yao kupitia 'online application system'.

Sijaona option nyingine ya kutuma maombi zaidi ya hiyo. Hivi huwa mnatathmini kweli hali ya Tanzania na watanzania?. Online application system huwa zina mlolongo mrefu, kama sio mzoefu ni nadra sana kufanikiwa kupitisha maombi yako.

Mtoto aliyesoma wildlife management pale Pasiansi, akarudi Bariadi kusikilizia hizo ajira, leo umwambie akapambane na online application system ataweza kweli???.

Maombi kwa barua pepe ndio njia ambayo asilimia kubwa ya vijana wanamudu, hata kwa usaidizi. Tanapa ni mali ya uma, iwe inafikiria uma wa watanzania. Au kwavile mnapokea wazungu kwa wingi basi mnahisi Tanapa ni ya wazungu!!!.

Nimeshuhudia wahudumu wa internet cafe na maduka ya stationary wakishindwa kuwasaidia vijana kutuma maombi kwenye hiyo 'online system' ya Tanapa.

Sehemu ya Qualification, kuna eneo inabidi u-select result kutoka kwenye drop down menu. Lakini hiyo drop down menu haina chochote na wala huwezi andika chochote.

Na bila kujaza result huwezi endelea mbele kutengeneza profile yako ambayo ndio utaitumia ku-apply hizo nafasi. Tanapa hebu rekebisheni hiyo system, au toeni maelekezo.

Tunajua mme-out source hiyo online application system kama njia tu ya kupigia hela za umma. Tanapa haina mahitaji hayo. Mna ofisi ya rasilimali watu ambayo inaweza ikaratibu mchakato mzima wa ajira mpya.
Mkuu nowadays hilo haliepukiki
 
Mnachoongea kiko sahihi kwa asilimia zote. Huduma za online zinarahisisha mambo mengi sana. Lakini linapokuja swala la hizo huduma za kimtandao kutolewa na taasisi zetu za kiserekali, mimi naendelea kusema bado. Tena bado sana haifai online application system ndio iwe njia pekee ya kutuma maombi kwa taasisi za serekali. Inawezekana mnasema hivyo kwakuwa hamjawahi kukutana na hizi kadhia kwenye mitandao inayomilikiwa na kampuni, taasisi, au mashirika ya umma. Labda mnatumia huduma za recruiters. Recruiters wako smart na active sana kwenye huduma za online.
Sisi watanzania kwa kuanzisha hatujambo. Kuendeleza hizo huduma ndio shida. Nenda website ya tra leo ujaribu kutumia calculator ya gharama za kuingiza gari nchini, nenda brella jaribu registration zao, nenda hata crdbbank.com ujaribu ku-verfy Visa card yako, pitia website mbalimbali za serekali zinazotoa huduma online, lazima ukwame njiani kwa sababu zilizondani ya uwezo wao. Ila tu ni kwasababu hawawezi ku-maintain hizo huduma. Juzijuzi tu hapa, kununua ticket ya ATCL online ilikuwa ni shida.
Website nyingine hata habari zilizopo mule zimeshapitwa na wakati. Website hazifanyiwi update kwa muda muafaka.
Hata wasomi wetu wa ICT sidhani kama wana chama kilicho active. Nilitegemea wao ndio wawe watch dog number moja wa kuzikemea taasisi zilizolala kwenye upande wa kutoa hukuma kwa njia za mtandao. Wataalamu wetu wa ICT katika umoja wao waangalie uwezekano wa kufanya TCRA iwe ikikagua hizi website na kuhakikisha zinafanya kazi na kutoa huduma kwa asilimia 100. Huo nimetoa mfano tu, yawezekana kukawa na chombo kingine tofauti na TCRA.
Mimi naendelea kutoafikiana na TANAPA kwa kuweka online application kama ndiyo njia yao pekee ya kupokea maombi. Kukiwa na mabadiliko chanya kwenye utamaduni wetu wa ku-maintain vitu, hapo nitaunga mkono kuwa na njia hiyo moja. Lakini kwasasa hapana, TANAPA wanawanyima watu fursa za ajira kwa uzembe wa watu wao wanaohusika na kuhakikisha online application system inafanyakazi vizuri.
Mwisho naishukuru JF kwa kutoa fursa hii. Hivi sasa ukiingia kwenye hiyo online system unaona kuna mabadiliko chanya. Unaona kabisa kuna mtu kapita na kusawazisha mambo. Pia uliyechukua hatua haraka na kusawazisha system, nakushukuru sana.
 
Nafikiri wewe ata kazi itakushinda ,kama watoto kwenda chuo wanatumia system za online ,mkopo wa elimu ya juu n.k ,jiongeze aisee siyo kila kitu kulalamika.
 
Watanzania kwa kulialia hatujambo.

2018 karne ya 21 bado mtu unalalamika kufanya online application?

Vibanda vya internet kibao, simu janja kibao, tablet, iPad.

Online application ndio njia rahisi kuliko zingine, inaokoa gharama, inaokoa muda, mpaka mtu aliyeko remote area anaweza kufanya hili kwa unafuu kidogo kuliko ungesema watume kwa posta maana kuna sehemu kupata ofizi za posta ni mtihani.
All in all dunia imebadilika hebu tubadilike, huyo mtoto aliyesoma Pansiansi sio kilaza kiasi cha kushindwa kujua email, kujua kujaza online application kwenye mfumo wa Tanapa, kujua ku-scan vyeti n.k
Kama mfumo wa Tanapa unasumbua basi ni suala la kuwambia Tanapa waweze ku-resolve mbona hayo mambo ya kawaida sana hata TCU inasumbua mara kibao, UDSM inasumbua mara kibao, Necta, Nacte n.k
Tuache kulialia, tungeambiwa kutuma kwa EMS bado tungelilia gharama



Ni kweli ila system yao bado inamatatizo. Process ni kwamba lazima ufanye registraton ndio u apply ila haikubali hivyo inakwamisha wanaotaka ku apply
 
Mkuu wazo lako ni zuri ila kwa dunia ya leo online application haikwepeki
Tafuta wataalamu watakusaidia(wapo wenye ujuzi hasa mjini).
Nafikiri mtoa mada ana maanisha tatizo ni ubovu wa application siyo jinsi ya kutumia pamoja na accessibility ....inawezekana haijawa tested vizuri bado kuna bugs
 
Nakuelewa sana Sir Khan, lakini kwa shirika la umma wa watanzania Tanapa, bado hatujafikia hatua ya kuwa na option moja tu ya online. Sipingi uwepo wa online system. Kuwe na online, pia kuwe na option nyingine kama baruapepe, nk. Swala jingine hata hiyo online system yenyewe ni mbovu kama nilivyoeleza. Hata upate mtaalamu gani, kama system haikuruhusu kujaza kipengee fulani, huyo mtaalamu ata-fail tu.
Hoja ya msingi iwe kuboresha hiyo online application kama ina kasoro. Kwa karne ya leo huwezi kukwepa hiyo kwa sababu inapunguza usumbufu kwa wote waombaji na hao TANAPA. Unataka yale mambo ya uhamiaji waombaji kujaza uwanja while wengi hawana sifa? Bora kuwa na system ya kuwa screen mapema ili ubakie na wenye sifa tuu ndiyo waitwe kwenye interview.
 
Mnachoongea kiko sahihi kwa asilimia zote. Huduma za online zinarahisisha mambo mengi sana. Lakini linapokuja swala la hizo huduma za kimtandao kutolewa na taasisi zetu za kiserekali, mimi naendelea kusema bado. Tena bado sana haifai online application system ndio iwe njia pekee ya kutuma maombi kwa taasisi za serekali. Inawezekana mnasema hivyo kwakuwa hamjawahi kukutana na hizi kadhia kwenye mitandao inayomilikiwa na kampuni, taasisi, au mashirika ya umma. Labda mnatumia huduma za recruiters. Recruiters wako smart na active sana kwenye huduma za online.
Sisi watanzania kwa kuanzisha hatujambo. Kuendeleza hizo huduma ndio shida. Nenda website ya tra leo ujaribu kutumia calculator ya gharama za kuingiza gari nchini, nenda brella jaribu registration zao, nenda hata crdbbank.com ujaribu ku-verfy Visa card yako, pitia website mbalimbali za serekali zinazotoa huduma online, lazima ukwame njiani kwa sababu zilizondani ya uwezo wao. Ila tu ni kwasababu hawawezi ku-maintain hizo huduma. Juzijuzi tu hapa, kununua ticket ya ATCL online ilikuwa ni shida.
Website nyingine hata habari zilizopo mule zimeshapitwa na wakati. Website hazifanyiwi update kwa muda muafaka.
Hata wasomi wetu wa ICT sidhani kama wana chama kilicho active. Nilitegemea wao ndio wawe watch dog number moja wa kuzikemea taasisi zilizolala kwenye upande wa kutoa hukuma kwa njia za mtandao. Wataalamu wetu wa ICT katika umoja wao waangalie uwezekano wa kufanya TCRA iwe ikikagua hizi website na kuhakikisha zinafanya kazi na kutoa huduma kwa asilimia 100. Huo nimetoa mfano tu, yawezekana kukawa na chombo kingine tofauti na TCRA.
Mimi naendelea kutoafikiana na TANAPA kwa kuweka online application kama ndiyo njia yao pekee ya kupokea maombi. Kukiwa na mabadiliko chanya kwenye utamaduni wetu wa ku-maintain vitu, hapo nitaunga mkono kuwa na njia hiyo moja. Lakini kwasasa hapana, TANAPA wanawanyima watu fursa za ajira kwa uzembe wa watu wao wanaohusika na kuhakikisha online application system inafanyakazi vizuri.
Mwisho naishukuru JF kwa kutoa fursa hii. Hivi sasa ukiingia kwenye hiyo online system unaona kuna mabadiliko chanya. Unaona kabisa kuna mtu kapita na kusawazisha mambo. Pia uliyechukua hatua haraka na kusawazisha system, nakushukuru sana.
Niko Kigoma, kuna madogo wawili niliwapa hilo Tangazo mbona wamejaza na kutuma fasta tuu? Unakwama wapi specifically??
 
Back
Top Bottom