Tamthilia ya Game of Thrones imenifanya niitilie shaka Biblia

Tatizo una uelewa mdogo wa masuala ya Imani ya Kimungu. Na kamwe Imani haithibitishwi na "Idea" za watu. Imani hujithibitisha yenyewe ukiwa unatafuta vitu vya kusoma ili kuProve imani basi hata Hadithi ya Sadiki na chitemo unaweza kuitumia.

Hiyo ni talent tu inayotoka kwa Mungu, ukisoma Kazi za Tolkien au Stan Lee utakuja kusema kwamba hawa watu walikua mashetani kwa kutengeneza imaginary characters and universe. Kwa Tolkien na Stan Lee, George RR Martin haiingii hata robo.

Soma, nikikupa kitabu kimoja cha Saint Thomas Aquinas ukakisoma kitakuondolea ufinyu wote wa imani utakaokuanao
Mkuu NiPM ivo vitabu Kaka.
 
Sababu najua hivi ndiyo vitu vyako pendwa..!
Mkuu!
Ni watu wanatabia wakisoma vitu huko basi moja kwa moja wanahusianisha na Bible. Mimi ni mpenzi wa Game of Thrones series na Vitabu na ninakubali akili ilitumika hasa kuandaa hivyo vitu ila sijawahi kuhusianisha na Biblia. Eti kwakua walitumia akili nyingi basi biblia pia iliundwa hivyo. Such a Dumbdumy pitch.

Kama ni msomaji wa High Fantasy Novel lazima ukubali RR Tolkien alikua very smart katika kutunga na kutengeneza vitu vya kufikirika. Lakini sijawahi kuona wakimuhusisha kama mtoa mada alivyofanya.
Tolkien was smart enough hadi akatengeneza lugha zake mwenyewe nyingi tu hata ukitaka kujifunza unaweza jifunza.

Hii inaitwa Tengwar language katengeneza Tolkien
images (14).jpeg
images (15).jpeg
 
Kuna kuaminishwa na kuamini ,Mimi naamini sio nimeaminishwa. I'm a living testimony.

Sema kama MTU anatabia za mwili hawezi kuyaelewa mambo ya kiroho 1 korinth 2:10-15
Hapo ndipo watu wa Imani zenu mnapokosea kudhani / kuona kwamba wengine wamepotea na nyie ndio mmeona mwanga Ingawa to each his/her own ila kuishi katika dunia yenye fikra na imani tofauti watu kama nyie hamleti harmony bali chaos....

Kitu pekee kinachowafanya watu wanafuata logic rahisi kuishi nao ni kwamba pale ikitokea walichodhani / fikiri kikiwa proven otherwise wanakubali kwamba walikosea na kufuata proven alternative..., Watu wa imani watapindisha kilichopo kiendani within wanachoamini No room for learning / uchunguzi ni always being indoctrinated
 
Pasi na shaka kwa waliobahatika kuitazama series ya GAME OF THRONES mpaka mwisho watakiri kua kwa upande wa mpnagilio wa matukio wahusika mzingara story..... ile series haina mpinzani

Ni series ambayo ukiacha kuitazama huku una fananisha au kuipambanisha na series fulani basi unaweza ukaachwa mdomo wazi na jinsi wale jamaa walivyo iandaa

Mimi ni moja kati ya watu walio tazama series hii zaidi ya mara 4 na kati ya story ambayo nimekua nikitamani kujua zaidi ni ya familia ya Tygarius (ile ya Mother dragon Daenerys )

Shahuku yangu ikanifanya niangukie kwenye vitabu vyake ambvyo vina Original story kuanzia Book one mpaka 5 ambapo kuna Dance with dragon,clush of kings ,song of ice and fire ,game of thrones a feast of crows ....

Hii story iko deep sana na sidhani kama itakapo kuja kupita miaka 100 au zaidi watakao simuliwa watasimuliwa kama fiction ..

Ni simulizi iliyo timia haswaa kuanziaa koo vizazi ramani mazingira mpaka vitu vidogo vidogo kama mapanga yale ya verilian steel yani unaweza sema ni kweli


Hii imekuja kuibua maswali mengi sana kichwani kwangu ambayo kimsingi sifurahishwi nayo ila ndio yamesha kuja..

Kama mtu mmoja au wawili wanaweza kusuka story ikatimia namna hii haiwezekani kweli kukawa na kundi la watu walio timia akili kua walikaa wakasuka zile simulizi za kutembea juu ya maji au kupasua bahati au kupaa angani au adamu na eva ... ?

Kwasababu hizi story za huku kwenye kitabu tusicho ruhusiwa kuhoji nazo zina ungano wake ila huyu jamaa wa game of thrones asee alipika bwana ...

Mimi binafsi baada ya kumaliza hivyo vitabu nimeingiwa sana ba wasiwasi juu hizi simulizi za kwenye vitabu vya kidini inawezekana zikawa ni Ngano tu ila sisi tuna zichukulia serious. . View attachment 2053525
Sishangai na wasi wasi kuhusu UKWELI wa Bibilia
Nashangaa tu kwamba eti utunzi wa GOT ndio umekufanya uhoji uhalali wa BIBILIA

Mkuu kwa muktadha wako huu we bado ni DHAIFU sana kwenye IMANI
Kuna vitabu ukisoma wewe na hakika utamkana hata Mama yako achilia mbali kutotambua uwepo wa MUNGU

GOT ni hadithi tu kuna wamba manguli wa ideology wanakujengea hoja unamkana Mungu mazima achalia mbali kutilia mashaka....... yaani una conclude mazima HAKUNA MUNGU na Bibilia ni hadithi za elfu ulela wa ulela
 
inaponishangaza biblia n nguvu yake ya kuwabadilosha watu waovu kuwa wema na nguvu yake ya kuishtaki dhamiri "consience" hapo tuu ndo inatofautiana na vitabu vingne vyote
Vitabu vya DINI ZOTE vinafanya haya unayodai BIBILIA inayafanya
 
na katiba ya tanzania inamahusiano na hii series maana si kwa yale yaliyo sukwa.
 
Kuna kuaminishwa na kuamini ,Mimi naamini sio nimeaminishwa. I'm a living testimony.

Sema kama MTU anatabia za mwili hawezi kuyaelewa mambo ya kiroho 1 korinth 2:10-15
Wakristo walioshiba imani yao wakikosa HOJA kutetea imani yao basi hukimbilia kusema haya mambo ni “ya kiroho”

Yaani hata 2+2 mkristo akiaminishwa jibu ni 10 basi ulimbana kimantiki inakuajr 2+2 ni 10 atakwambia haya ni mambo ya kiroho huwezi kuyaelewa ukiwa kimwili 😂😂😂😂

Yaani kiroho ni hakunaga kutumia akili ni kuamini tu PERIOD
Ndio maana Kibwetere aliwatia kibiri waumini wake kwa gia hii hii ya KIROHO
 
Wakristo walioshiba imani yao wakikosa HOJA kutetea imani yao basi hukimbilia kusema haya mambo ni “ya kiroho”

Yaani hata 2+2 mkristo akiaminishwa jibu ni 10 basi ulimbana kimantiki inakuajr 2+2 ni 10 atakwambia haya ni mambo ya kiroho huwezi kuyaelewa ukiwa kimwili

Yaani kiroho ni hakunaga kutumia akili ni kuamini tu PERIOD
Ndio maana Kibwetere aliwatia kibiri waumini wake kwa gia hii hii ya KIROHO

na wanao jitoa muhanga waislamu wakizani mbinguni kuna viwanja na wanawake bikra 100.sio mambo ya kiroho
 
Mtoa mada unatakiwa usome kitabu kimoja hivi ambacho nadhani hujawahi kukisoma.

Hicho kitabu chenyewe kinajisifia kwamba hakina shaka ndani yake na ni mwongozo kwa waongofu.

Na ndio kitabu pekee hapa duniani kilicho jihakikishia chenyewe kuwa ndio cha ukweli.

Kukipata we nenda duka lolote la vitabu, uliza kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake utauziwa.

Ukimaliza kukisoma tuletee mrejesho hapa.
Achana na hizo hadithi za kutunga za siku elfu moja na moja.
 
Ukisema uta question biblia unamaanisha ufahamu wako katika Mungu ni Mdogo sana.
Maana ungekuwa na ufahamu mkubwa katika Mungu ungesema kama binadamu tu wanaakili hivi Mungu ni zaidi.

Pia ungekuwa msomaji wa biblia wapo watu waliokuwa wenye akili kipindi cha farao lakini ulipokutanishwa na Mungu wa Musa akili zao hazikufua dafu.

Mshangae na Kumtukuza Mungu kwa kuwaumba watu kama hao.

Biblia imetusisitiza sana neno la Mungu likae kwa wingi ndani yenu.
Imani zetu zimekuwa nyepesi sana kutikiswa kwasababu ya uhaba wa neno la Mungu ndani mwetu.

Suleiman alikuwa na akili (hekima) sana hata malkia wa kusini alimwendea kila wakati lakini bado ukisoma kitabu chake cha muhubili utajifunza anachokwambia
MUHUBIRI 7;29
MATHAYO 12:42
Ngano
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom