Tamko la Kanisa la Morovian

Tamko la Kanisa la Morovian

Mleta mada hv umewahi shuhudia Askofu au mchungaji wa Moravian kaombea mgonjwa yeyote akapona ?Hili ni moja ya makanisa ambayo wauminia wao ni fuata upepo sijawahi ona. Wakisikia Mwakasege kaja wote wanakimbila huko,sjui kaja muhubiri fulani wote wanakimbilia huko .(The likes of KKT na Anglican).Hakuna kinachoendelea huko kwenye makanisa yao zaidi ya michango,na harambeee hasa kipindi cha uchaguzi. Hayo ni mapango ya biashara ,nawaonea huruma washirika wa hayo makanisa ni wasindikizaji wa safari ya mbinguni. Mi nilikua muumini wao nikagutuka kule sio kusali ni kupoteza mda.
Umetoka nje ya mada mkuu. Hatujadili kuombea au michango kanisani. Jadili hoja siyo mtoa hoja!
 
Askofu yuko sahihi, Kanisa limepewa kibali cha kuomba kwa MUNGU aingilie kati na kuiponya nchi, 2 Nya 7:14. Tatizo ni mtumishi yupi anaemheshimu anaona uchungu asimame amwambie MUNGU yatosha hapa tulipofika. Maana anasema anaheshimu watumishi wake.
 
Kweli Watanzania tumefika mahali pa kutukana madhehebu? Nafikiri so sawa, wewe njoo na hoja,Mungu akupe rehena maana unakoelekea siko
Mleta mada hv umewahi shuhudia Askofu au mchungaji wa Moravian kaombea mgonjwa yeyote akapona ?Hili ni moja ya makanisa ambayo wauminia wao ni fuata upepo sijawahi ona. Wakisikia Mwakasege kaja wote wanakimbila huko,sjui kaja muhubiri fulani wote wanakimbilia huko .(The likes of KKT na Anglican).Hakuna kinachoendelea huko kwenye makanisa yao zaidi ya michango,na harambeee hasa kipindi cha uchaguzi. Hayo ni mapango ya biashara ,nawaonea huruma washirika wa hayo makanisa ni wasindikizaji wa safari ya mbinguni. Mi nilikua muumini wao nikagutuka kule sio kusali ni kupoteza mda.
 
Mtu akiwa anashabikia mambo ya ccm huwa nawaza sana kama ni binadamu mwenzangu naogopa hata kumsogelea ndo maana komenti za kina elungata na barbarosa humu ndani huwa sijibu maana naogopa huenda najibishana na allien yupo zake mars huko
Huyo mtu bu hatari sana kaa naye mbali, ana roho ngumu mno.
 
MAASKOFU NA WACHUNGAJI, KEMEENI MAOVU! MSIWAOGOPE WANASIASA, WATAWALA NA MATAJIRI!

Hawa ni watu ajabu sana! Walipokuwa katika Vyuo vya Theologia na Biblia walisoma sana kuhusu ujasiri wa Askofu Mkuu Janani Luwum wa Kanisa Kianglikana Uganda jinsi alivyomkabili Iddi Amin na kumueleza aache kuua watu wake; wengi wao walisoma na kutiwa moyo na ujasiri wa Askofu Mkuu Desmond Tutu wa Kanisa Anglikana Afrika Kusini jinsi alivyopambana na mfumo wa Ubaguzi wa Rangi ambao ulitweza na kufedhehesha utu, na kuwaua watu weusi kama ndege; wapo waliosoma na kufurahia sana maandishi kuhusu Liberation Theology yaliyotolewa na Padre Gutierrez Gutierrez Gutierrez wa Roman Catholic Church kule Latin America jinsi alivyopinga unyonyaji na ukandamizaji wa wananchi wanyonge uliokuwa ukifanywa na matajiri waliokuwa wameunda ushirika muovu na watawala wakandamizaji; wapo waliotamani sana wamuone Martin Luther King Jr., yule Mchungaji wa Kibatisti jinsi alivyopambana kutokomeza ubaguzi na ukandamizaji kule Marekani, mbengu za haki zilizopiganiwa na yeye zilizopelekea Mmarekani mwenye asili ya Kiafrika Barack Obama kutawala Marekani bado inasimuliwa hadi sasa; wengine wamejaza maandishi ya Padre Profesa Martin Luther jinsi alivyotetea wanyonge na kusimamia matengenezo ya Kanisa kule Ulaya hasa Ujerumani; wengine hadi leo wanatukuza ujasiri wa Padre Profesa Jan Huss yule mwanzilishi wa u-Moravian alivyopinga uovu hadi akachomwa moto hadharani. Wengi wanafundisha na kuhubiri nadharia kuhusu haki kwa mujibu na mtazamo wa ki- Biblia huku wakikesha kusoma vitabu vya manabii kama Amos, Yeremia, Ezra, nk.

Kinachoshangaza ni kuwa wanaposikia na kuona maovu ya aina hiyo hiyo au hata yanayokithiri katika jamii zao wanafumba macho. Waumini wao wanapofanyiwa maovu na kuonewa na hata kupoteza maisha hawafumbui kinywa. Watu wengine wasiokuwa waumini wao wanapofanyiwa ukatili ndio haiwahusu kabisa! Wanasahau kuwa Nabii Amos alikemea maovu yaliyokuwa yakitendwa hata nje ya mipaka ya Nchi yake ya Yuda kwani aliwaonya watawala wa Damaska, Gaza, Tiro, Edomu, Amoni, Moabu, Israeli, nk.

Watumishi wengine wachache wakijitokeza kukemea maovu basi wao (wasiotaka kukemea) hugeuka kuwa watesi wa watumishi wanaokemea maovu! Maaskofu wengine wanadiriki hata kuwatishia kuwatimua katika makanisa Wachungaji walio majasiri wa kukemea uovu! Wanawanyamazisha kiaina. Kwao ujasiri wa Yohana Mbatizaji aliyemkemea Herode ni nadharia ya kuisoma Kanisani tu lakini isiyofaa kuiishi. Wanafikiri kuwa kukemea uzinzi na ulevi madhabahuni ndio wito pekee walioitiwa lakini ubadhilifu na uporaji wa mali ya umma pamoja na ukandamizaji na utekaji na unyanyasaji wa watu siyo dhambi ya kukemewa madhabahuni. Kwao kutumia madhabahu kukemea ulevi na uzinzi kila Jumapili ndio utumishi lakini kutumia madhabahu hiyo hiyo kukemea watu wanaoeneza chuki katika jamii na wanaotesa, kuteka na kuua watu wengine ni 'kuingiza siasa Makanisani'! Kwao kutumia madhabahu kukemea unyanyasaji katika familia ndio utumishi lakini kutumia madhabahu hiyo hiyo kukemea unyanyasaji mahali pa kazi, na katika mifumo ya kisiasa na uendeshaji wa serikali ni kufanya siasa. Kwao wanaona ni ujasiri kuwaambia waumini kuacha kuwasingizia majirani zao kama moja ya Amri Kumi za Mungu inavyotaka lakini kuwaambia wanasiasa na watendaji katika mifumo ya kiserikali na kisiasa kuacha kuwasingizia watu na kuwabambikia kesi na kuwachafua wenzao ni 'kuleta siasa Kanisani'!

Ee Mungu uturehemu na ututie ujasiri tusiache kuwaonya hata hawa Wachungaji na Maaskofu wanaoupa kisogo wito wao wa kuonya, kukemea na kushauri katika jamii ulimowatuma kukutumikia kama Maandiko yanavyotaka (Ezekieli 33:1-20). Kama tunao ujasiri wa kuwaonya na kuwakemea matajiri, wanasiasa, na watendaji wa serikali, tupe pia ujasiri wa kuwakemea viongozi wa Makanisa walio waoga. Tupe hekima na neema ya kutokuwachukia tunaowakemea. Tupo uangavu wa kiimani ili tuone pia maovu yanayoweza kutendwa na hao tunaojua wanateswa na kunyanyaswa. Ee Bwana! Fufua kazi yako katikati ya mataifa!

Ujumbe huu nimeutoa leo nikiwa nimetimiza miaka 25 ya utumishi wangu tangu nilipojiunga rasmi katika kazi ya kumtumikia Mungu (full time ministry) siku ile ya tarehe 4 Agosti 1994.

Mwana Kondoo Ameshinda Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani

View attachment 1173288
Thi Good Servant Of God, May Our Most High God Bless you and your generations
 
Mleta mada hv umewahi shuhudia Askofu au mchungaji wa Moravian kaombea mgonjwa yeyote akapona ?Hili ni moja ya makanisa ambayo wauminia wao ni fuata upepo sijawahi ona. Wakisikia Mwakasege kaja wote wanakimbila huko,sjui kaja muhubiri fulani wote wanakimbilia huko .(The likes of KKT na Anglican).Hakuna kinachoendelea huko kwenye makanisa yao zaidi ya michango,na harambeee hasa kipindi cha uchaguzi. Hayo ni mapango ya biashara ,nawaonea huruma washirika wa hayo makanisa ni wasindikizaji wa safari ya mbinguni. Mi nilikua muumini wao nikagutuka kule sio kusali ni kupoteza mda.
sasa unasali wapi mkuu??
 
Sijui nini kimewakuta Au kwa vile the one in power ni mkristu mwenzao ? Wakati wa kikwete nyaraka za maaskofu zilikua bandika bandua
Ulipaswa kukemea bila kuweka viashiria vya udini , , Kwani viongozi wa waisilamu wanafua dafu kwa huyu kiongozi ukilinganisha na tawala zingine???
 
Sahihi
Mkurugenzi wa Taasisi moja,nyeti sana hapa nchini,ni mchungaji, sasa huwezi jua kwamba aliingia katika uchungaji akiwa na mission ya kupandikiza wachungaji ambao ni feki ila watumishi wa idara yake.

Baadhi si wachungaji, ni simba katika ngozi ya kondoo, wanawinda kwa niaba ya aliyewatuma,

Ndiyo yaleyale ya kwenda kumwambia mchungaji shida zako au kutubu kwake,jioni taarifa ziko makumbusho
 
Mleta mada hv umewahi shuhudia Askofu au mchungaji wa Moravian kaombea mgonjwa yeyote akapona ?Hili ni moja ya makanisa ambayo wauminia wao ni fuata upepo sijawahi ona. Wakisikia Mwakasege kaja wote wanakimbila huko,sjui kaja muhubiri fulani wote wanakimbilia huko .(The likes of KKT na Anglican).Hakuna kinachoendelea huko kwenye makanisa yao zaidi ya michango,na harambeee hasa kipindi cha uchaguzi. Hayo ni mapango ya biashara ,nawaonea huruma washirika wa hayo makanisa ni wasindikizaji wa safari ya mbinguni. Mi nilikua muumini wao nikagutuka kule sio kusali ni kupoteza mda.
Wewe ni shabiki wa miujiza fake na wachungaji fake. Nguvu ya kutenda miujiza iko ndani ya Kila mtu ,endelea kudanganywa.
 
Kwa hiyo ni upande huu tuu ? Wale was Azana haiwahusu!!

Au sielewi!
Hawa wakristu ndo wanafaki . nyaraka za wakati wa kikwete mambo ya inchi yanapoenda fyongo zimepotelea wapi ? Waliziandika sana wakati wa kikwete. Mie sikuona nyaraka upande wa pili
 
Ulipaswa kukemea bila kuweka viashiria vya udini , , Kwani viongozi wa waisilamu wanafua dafu kwa huyu kiongozi ukilinganisha na tawala zingine???
Awamu ya tano niwakristu waliokuwa wanaandika nyaraka kuonesha kutoridhika na mambo yalivyokuwa yanaenda . hizo nyaraka zipo humu jamii forum . kwanini saizi wako kimya kama siyo wanafiki ?
 
Dah! Uwezo wako kweli wa kupambanua hii hoja ndio umeishia hapa mkuu?

Sasa, kwa uelewa wako huyo Askofu aliyetoa hili andiko ni nani na wa wapi?

Lakini pia, hayo aliyoyasema hayana mantinki? Au Mantinki ya hoja zake inaondoka kwa sababu tu jina na cheo chake haviko vile unavyotaka wewe viwe?
Uwezo wangu uhukumiwe kwa haki!!!! Leteni orodha ya maaskofu wa Moravian kama mtaliona jina lake!!!!

Ni sawa na Mimi Leo nijifanye KADINALI wa TANZANIA.

Ama nijifanye Askofu wa KKKT .....
 
Back
Top Bottom