Tamko la Kanisa la Morovian

Tamko la Kanisa la Morovian

Nilifikiri ni askofu wa MORAVIAN.....

MORAVIAN ni kanisa lenye kujitambua, kuchanganya mtu anayejiita askofu wa Moravian na kanisa la Moravian ni kulikosea kanisa
Hivi Magufuli akitoa pole kwa mauaji ya Texas si ni kwa niaba ya Watanzania?
 
2020 hakika hakika tunataka kuona kwa wazi wagombea wetu wakiwa jasiri kusema na kuweka bayana misimamo yao na kutetea:
Haki dhidi ya udhalimu , wema dhidi ya udhalimu,
Uokoaji dhidi ya Utesaji .
Utawala wa hekima na Busara dhidi ya utawala wa Maguvu.
Upendo dhidi ya Chuki.
Upotoshaji wa kuhesabu Kura dhidi ya kupindua matokeo ya kura.
Demokrasia dhidi ya udikteta.
Uokoaji dhidi ya Utekaji.
Uponyaji dhidi ya uuaji wa makusudi.
Utajiri dhidi ya umaskini.
Ukabila /Ukanda dhidi ya Utaifa.


Hii itawasaidia wale wanaotetea upande wowote kupata muda wa kueleza ni kwa nini anasimama upande mmoja wa kati ya hayo hapo juu.
Mana kama ni utekaji na utesaji ni wazi vijana wa UVIVUSisemi walishajipambanua kuwa wao watamshughulikia yeyote wanayetofautiana naye. Na wakasema dola ni la kwao kwa hiyo watafanya chocho wanachotaka.
2020 ni wakati wao wa kueleza Dunia na wapiga kura kuwa kwa nini waliamua kuhamasisha uhalifu dhidi ya binadam? Na kwa nini kwao Watu walioumbwa na Mungu sio muhimu??

Na yeyote atakayejidai kuwa anakemea wakati wa Kampeni tuu wakati alikaa kimya binadam wakiwa wanapotea na kuuawa na kutekwa atuambie kwa nini alikaa kimya wakati alikua alikua na uwezo wa kukemea ?

Nampongeza sana Baba Askofu, Hakika ameisoma na kuielewa Vizuri Biblia anayoiamini.
Mambo Mazuri yaliyoko katika vitabu vya Dini ni pamoja na kupinga uovu unaotendwa na binadam.
Wanasiasa nao ni binadam hivyo nao pia watakemewa kama binadam wengine wanavyokemewa. Hakuna binadam aliyeko juu ya Maandiko ya Mwenyezi Mungu na maelekezo na AMRI ZAKE.

Katiba yetu na Dini zote kuanzia za asili zinakataza kuua ,kutesa ,dhulma,uonevu,uongo, usingiziaji, uporaji ,wizi, rushwa, Upendeleo ,ubaguzi,dharau n.k.
Hii kuwaziba watu midomo ni ishara ya watu kusemwa watasemwa na watasutwa siyo kwa mazuri bali kwa mabaya na mambo ya kishetani wanayofanya.
 
Mleta mada hv umewahi shuhudia Askofu au mchungaji wa Moravian kaombea mgonjwa yeyote akapona ?Hili ni moja ya makanisa ambayo wauminia wao ni fuata upepo sijawahi ona. Wakisikia Mwakasege kaja wote wanakimbila huko,sjui kaja muhubiri fulani wote wanakimbilia huko .(The likes of KKT na Anglican).Hakuna kinachoendelea huko kwenye makanisa yao zaidi ya michango,na harambeee hasa kipindi cha uchaguzi. Hayo ni mapango ya biashara ,nawaonea huruma washirika wa hayo makanisa ni wasindikizaji wa safari ya mbinguni. Mi nilikua muumini wao nikagutuka kule sio kusali ni kupoteza mda.
Wee jamaa mbilona unajidhalilisha hivyo,unaonyesha ulemavu mbaya sana wa akili yako!

Yaani unanyooshea vidole madhehebu?
Hebu tuambie hao akina Pengo,na maparoko wengine wamefanya nini kukemea uovu na ukandamizaji unaofanywa dhidi ya raia,(ambao wengi wao ni waumini wa makanisa yao).

Wapo akina Barnabas Mtokambali (askofu wa TAG) wamefanya nini zaidi ya kuendelea kuaminisha umma kuwa ukae kimya ili wawe salama?

Wachache kama akina Bagonza,na Shoo angalau unaona wanasema juu ya unyanyasaji dhidi ya watu.

Kama taifa tumejiwekea misingi ya uendeshaji nchi,tumekuwa na mahakama ili zitende haki,(na haki hizo zionekane zinatendeka) lakini inapofika hatua wenye mamlaka ndo wanakuwa na maamuzi ya hata kuondoa uhai wa wanaowapinga kwa kutumia nguvu ya dola,hiyo ni hatari sana!

Mbaya zaidi,ni kwamba leo tunahudhuria ibada St.nini sijui,wakati kesho muumini wa dini hiyo hiyo anayeabudu kinyerezi anakutwa "amejinyonga na kuvishwa nguo mpya" na hakuna anayeona ni problem,tunamsubiri J.pili nyingine aje ibadani kwa mbwembwe na kamera nyingi nyingi,wakati mahala pasipojulikana kuna muumini "anashughulikiwa" kwa kutafutiwa kesi,mara uraia wenye mashaka,mara sedition,na lastly,organised crime,Money lounadering,na ukwepaji kodi!

Mapadri wote,kimyaaaaa!
Wahashamu wote,kimyaaaa!
Makadinali wote,kimyaaaa!

Tumsifu yesu kristo,tumuombee kiongozi wetu,"aendelee kufanya vizuri....,katika kuijenga nchi yetu" (kwa sauti ya upole na kiutumishi)

MUNGU BABA TUHURUMIE TAIFA LAKO!
 
Mleta mada hv umewahi shuhudia Askofu au mchungaji wa Moravian kaombea mgonjwa yeyote akapona ?Hili ni moja ya makanisa ambayo wauminia wao ni fuata upepo sijawahi ona. Wakisikia Mwakasege kaja wote wanakimbila huko,sjui kaja muhubiri fulani wote wanakimbilia huko .(The likes of KKT na Anglican).Hakuna kinachoendelea huko kwenye makanisa yao zaidi ya michango,na harambeee hasa kipindi cha uchaguzi. Hayo ni mapango ya biashara ,nawaonea huruma washirika wa hayo makanisa ni wasindikizaji wa safari ya mbinguni. Mi nilikua muumini wao nikagutuka kule sio kusali ni kupoteza mda.
Uwezo wako wa kuelewa na kuchanganua mambo na hoja ni mdogo sana. Maskini umeshindwa hata kuelewa hoja iliyopo kwenye uzi huu ni ipi na ww utoe mawazo au mchango gani, bahati mbaya zaidi ukaingiza na maswala ya madhehebu ya watu ambayo kwa fikra zako unadhani unayaelewa vizuri kumbe nako hauna unachoelewa.

Ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke, Mungu akusaidie.
 
Nilifikiri ni askofu wa MORAVIAN.....

MORAVIAN ni kanisa lenye kujitambua, kuchanganya mtu anayejiita askofu wa Moravian na kanisa la Moravian ni kulikosea kanisa
Dah! Uwezo wako kweli wa kupambanua hii hoja ndio umeishia hapa mkuu?

Sasa, kwa uelewa wako huyo Askofu aliyetoa hili andiko ni nani na wa wapi?

Lakini pia, hayo aliyoyasema hayana mantinki? Au Mantinki ya hoja zake inaondoka kwa sababu tu jina na cheo chake haviko vile unavyotaka wewe viwe?
 
Kanisa lenye heshima nilile linalokaa kimya watawala mumiani wakimaliza watu wao!
Nilifikiri ni askofu wa MORAVIAN.....

MORAVIAN ni kanisa lenye kujitambua, kuchanganya mtu anayejiita askofu wa Moravian na kanisa la Moravian ni kulikosea kanisa
 
Mababa Askofu Bagonza, Mwamakula, Munga, Shoo, nk - yaani hamjui tu ni kwa jinsi gani mnavyonibariki kwa huduma yenu hii njema ya kukemea maovu.

ee Mungu Baba - tunaomba huku tukikemea kwa nguvu zote na kwenda kinyume dhidi ya hila za yule mwovu (shetani) ili atakapoingia kwa njia moja kutaka kuwadhuru hawa watumishi wako basi akapate kusambaratishwa kwa njia saba.
katika jina lake Yesu tunaomba na kuamini, AMEN.
 
Huyu Askofu mwehu tamko lake binafsi analiitaje tamko la kanisa? Ni wapi walikaa viongozi wa kanisa kikao wakatoa Hilo tamko? Huyu Askofu hazimo kichwani.Ukitoa tamko la kanisa linakuwa Ni tamko la kikao Sio unajiibukia tu na tamko lako na kuliita la kanisa
 
Huyu Askofu mwehu tamko lake binafsi analiitaje tamko la kanisa? Ni wapi walikaa viongozi wa kanisa kikao wakatoa Hilo tamko? Huyu Askofu hazimo kichwani.Ukitoa tamko la kanisa linakuwa Ni tamko la kikao Sio unajiibukia tu na tamko lako na kuliita la kanisa
mwenyekiti wa chama chetu CCM hufanya maamuzi bila vikao rasmi.
huyu Baba Askofu labda kamuiga mkuu wa nchi!
 
Kanisa ndilo lilisababisha mauaji ya kimbari Rwanda.
Hilo Ni tamko lake binafsi Sio la kanisa lolote lenye jina la Moravian lililopo Tanzania au nje ya Tanzania.Kanisa lolote lenye jina Moraviani halijawahi kaa kikao chochote kutoa Hilo tamko.Ni tamko lake binafsi Yeye Kama yeye
 
Kanisa ndilo lilisababisha mauaji ya kimbari Rwanda.
Muogope Mungu na uwe mkweli achana na Imani za Chuki na uongo.
Unajidhalilisha na kuudhalilisha uislam wako.
Wapo Waislam wengi tu Leo hii ni waelewa sana kwenye mambo ya imani za dunia nzima kwa sasa.
Watu wanajua uko mpango wa siri wa Kishetani na umejiingiza kwa waumini na viongozi wa Dini zote. Ndio maana Dunia nzima kuna vurugu na chanzo chake ni uonevy unaotikana na watawala.

Hakuna Dini ya kweli inayoweza kukaa kimya dhidi ya udhalimu ,iwe ni ukristo au uislam au Ubudha au Upagani.

Tuwasaidie watu kujua Haki na dhulma.
Haya mambo ya kueneza Chuki za watu kidini ni upuuzi na ujinga mtupu.
Dini bila haki kwenye jamii ni upumbavu.

Rwanda Makanisa ndipo walipokua wanakimbilia watu dhaifu kama inavyokuwa kwenye nchi za kiislam kwenye Vita ambapo wale watu wasio na vurugu hukimbilia kujihifadhi.

Wanapokua wengi ni dhahiri viongozi wa Dini wanajitokeza kukemea serikali kuwa iache kuua watu wake mana inasababisha Wakimbizi kujaa kwenye nyumba za ibada na wanaotwishwa mzigo na hata kuuawa au kuandamwa ni Viongozi wa Dini waliowapokea na kuwahifadhi.
Mara nyingine wanakimbilia hata wale wanaotafutwa na wanaogombana nao.
Siku zote adui wa serikali na Chama Tawala ni yule anayehatarisha madaraka yao kwa kuwapinga.

Ni kanisa lipi Rwanda liliwahi kuingiza Sialaha na kuanzaisha Jeshi au Kundi Rasmi la kuua?
Kama ilitikea kwa kanisa moja au mawili ndio kusema ni nchi nzima?

Hivi nani anaweza kuishinda vita inayoanzishwa na Kanisa?
Hayupo Duniani hata yule baba yenu Lucifer hawezi .
Kanisa ni Kazi ya Kristo au Masihi Mwenyewe ndio maana hata Utawala Mkubwa kama wa Rumi ulinyoosha mikono na kujisalimisha chini ya Kanisa.

Kanisa kazi yake ni kusimama kwenye Ukweli.

Kanisa haliwezi kukaa kimya na kuangalia wanadam wanauawa bila sababu hasa watu wasio na madhara.
Yaani watu wasiotumia silaha kwa nini wauawe bila hata kuhukumiwa mahakamani?
Kama MTU anakosa afikishwe mahakamani mana tumejiwekea sheria.
Kwa nini wakae kimya kisa eti Rwanda walihusika kwenye mauaji?
Hivi ni namna gani Vita ya Watusi na Wahutu ingekwepeka ?

Kwa nini haikua vita kati ya Dhehebu moja na lingine au Kanisa na Misikiti au Uislam kule Rwanda?
Kwa nini ilikua ni kati ya Wahutu na Watutsi ambao wengi ni Wakristo??

Hapo inakuaje vita ya Kanisa?

Watawala wasimamie haki na sheria hakuna vurugu inayoweza kutokea mahali penye haki hiyo ni kanuni ya Imani zote kuanzia zile za asili.
Tusidanganyane kwa sababu ya kuona kuwa tunaweza kutumia risasi muda wote.
Hatuna Jeshi kubwa kama la Sadam au Gadaf lakini watu walipochoka kuongozwa kwa Risasi waligeuka na kupuuza mema yote yaliyofanywa na watawala wao.
Hata IDD Amini alikua malendo sana kwa Taifa lake kosa alilofanya ni kutojali uhai wa watu wake na haki zao za msingi akawaza kuimarisha tu utawala wake,watu wakamchoka na kumtoa kwa kushirikiana na majeshi ya wageni.

Tunayashangila haya Leo lakini Kesho wakinyamaza hawa maaskofu ujue kesho kutwa atatekwa Shekhe na kuuawa halafu wataaminishwa watu kuwa alikua gaidi na jamaii itakaa kimya mana magaidi wanaogopwa . Kumbe ni ugomvi wa kimadaraka tu au ameoneka kuwa huyo Shekhe a anaukaribu na Mtu Fulani ambaye ni tishio la Madaraka ya watu Fulani.

Haki ibaki kuwa haki hata kama imesemwa na Mpagani.

Leo hii tunamuenzi Kinjekitile Ngwale pamoja na kuwa alikua na Dini zake za asili kwa sababu tu alipigania HAKI.
 
Muogope Mungu na uwe mkweli achana na Imani za Chuki na uongo.
Unajidhalilisha na kuudhalilisha uislam wako.
Wapo Waislam wengi tu Leo hii ni waelewa sana kwenye mambo ya imani za dunia nzima kwa sasa.
Watu wanajua uko mpango wa siri wa Kishetani na umejiingiza kwa waumini na viongozi wa Dini zote. Ndio maana Dunia nzima kuna vurugu na chanzo chake ni uonevy unaotikana na watawala.

Hakuna Dini ya kweli inayoweza kukaa kimya dhidi ya udhalimu ,iwe ni ukristo au uislam au Ubudha au Upagani.

Tuwasaidie watu kujua Haki na dhulma.
Haya mambo ya kueneza Chuki za watu kidini ni upuuzi na ujinga mtupu.
Dini bila haki kwenye jamii ni upumbavu.

Rwanda Makanisa ndipo walipokua wanakimbilia watu dhaifu kama inavyokuwa kwenye nchi za kiislam kwenye Vita ambapo wale watu wasio na vurugu hukimbilia kujihifadhi.

Wanapokua wengi ni dhahiri viongozi wa Dini wanajitokeza kukemea serikali kuwa iache kuua watu wake mana inasababisha Wakimbizi kujaa kwenye nyumba za ibada na wanaotwishwa mzigo na hata kuuawa au kuandamwa ni Viongozi wa Dini waliowapokea na kuwahifadhi.
Mara nyingine wanakimbilia hata wale wanaotafutwa na wanaogombana nao.
Siku zote adui wa serikali na Chama Tawala ni yule anayehatarisha madaraka yao kwa kuwapinga.

Ni kanisa lipi Rwanda liliwahi kuingiza Sialaha na kuanzaisha Jeshi au Kundi Rasmi la kuua?
Kama ilitikea kwa kanisa moja au mawili ndio kusema ni nchi nzima?

Hivi nani anaweza kuishinda vita inayoanzishwa na Kanisa?
Hayupo Duniani hata yule baba yenu Lucifer hawezi .
Kanisa ni Kazi ya Kristo au Masihi Mwenyewe ndio maana hata Utawala Mkubwa kama wa Rumi ulinyoosha mikono na kujisalimisha chini ya Kanisa.

Kanisa kazi yake ni kusimama kwenye Ukweli.

Kanisa haliwezi kukaa kimya na kuangalia wanadam wanauawa bila sababu hasa watu wasio na madhara.
Yaani watu wasiotumia silaha kwa nini wauawe bila hata kuhukumiwa mahakamani?
Kama MTU anakosa afikishwe mahakamani mana tumejiwekea sheria.
Kwa nini wakae kimya kisa eti Rwanda walihusika kwenye mauaji?
Hivi ni namna gani Vita ya Watusi na Wahutu ingekwepeka ?

Kwa nini haikua vita kati ya Dhehebu moja na lingine au Kanisa na Misikiti au Uislam kule Rwanda?
Kwa nini ilikua ni kati ya Wahutu na Watutsi ambao wengi ni Wakristo??

Hapo inakuaje vita ya Kanisa?

Watawala wasimamie haki na sheria hakuna vurugu inayoweza kutokea mahali penye haki hiyo ni kanuni ya Imani zote kuanzia zile za asili.
Tusidanganyane kwa sababu ya kuona kuwa tunaweza kutumia risasi muda wote.
Hatuna Jeshi kubwa kama la Sadam au Gadaf lakini watu walipochoka kuongozwa kwa Risasi waligeuka na kupuuza mema yote yaliyofanywa na watawala wao.
Hata IDD Amini alikua malendo sana kwa Taifa lake kosa alilofanya ni kutojali uhai wa watu wake na haki zao za msingi akawaza kuimarisha tu utawala wake,watu wakamchoka na kumtoa kwa kushirikiana na majeshi ya wageni.

Tunayashangila haya Leo lakini Kesho wakinyamaza hawa maaskofu ujue kesho kutwa atatekwa Shekhe na kuuawa halafu wataaminishwa watu kuwa alikua gaidi na jamaii itakaa kimya mana magaidi wanaogopwa . Kumbe ni ugomvi wa kimadaraka tu au ameoneka kuwa huyo Shekhe a anaukaribu na Mtu Fulani ambaye ni tishio la Madaraka ya watu Fulani.

Haki ibaki kuwa haki hata kama imesemwa na Mpagani.

Leo hii tunamuenzi Kinjekitile Ngwale pamoja na kuwa alikua na Dini zake za asili kwa sababu tu alipigania HAKI.
Huwa sikisii.

Porojo ndefu ulizopiga hazifichi wala hazikimbizi ukweli. Wala kuacha niliyoandika na kunivaa mimi binafsi badala ya kutetea makanisa yako hakuuondoi ukweli wa ushenzi uliofanywa ndani ya makanisa huko Rwanda na kuwa mauaji yalianzia kanisani na wahusika wakuu ni viongozi wa makanisa.

Wala kupachika jina la Iddi Amin hakubadilishi kitu. Ukitaka tujadili ya Iddi Amin fungua uzi wake. Hapa ni kanisa.

Kwanza tueleze kwanini Papa kaomba msamaha kwa niaba ya kanisa? Halafu baadae utueleze kwanini wachungaji wa Rwanda walihukumiwa kule Arusha? Soma hiyoooo:

Pope apologises for church's role in Rwanda genocide | News | Al Jazeera
20 Mar 2017 · Catholic church was accused of being close to Hutu-led government in 1994 when 800,000 mostly Tutsis were killed. ... "He implored anew God's forgiveness for the sins and failings of the Church and its members, among whom priests, and religious men and women who succumbed to hatred ...

Halafu soma kuhusu Waislam wa Rwanda na kimbilio la wasio Waislam lilikuwa wapi. Kisha ongea. Kumbuka hapa umekuja patamu sana leo na tunavyoendelea naweka uchi uozo wa kanisa na iliyoyafanya huko Rwanda...

From the ashes of genocide, Islam rises in Rwanda
5 Apr 2019 · When the genocide in Rwanda began in 1994, the ... “ The [victims] went to churches thinking they will find ...
 
Mleta mada hv umewahi shuhudia Askofu au mchungaji wa Moravian kaombea mgonjwa yeyote akapona ?Hili ni moja ya makanisa ambayo wauminia wao ni fuata upepo sijawahi ona. Wakisikia Mwakasege kaja wote wanakimbila huko,sjui kaja muhubiri fulani wote wanakimbilia huko .(The likes of KKT na Anglican).Hakuna kinachoendelea huko kwenye makanisa yao zaidi ya michango,na harambeee hasa kipindi cha uchaguzi. Hayo ni mapango ya biashara ,nawaonea huruma washirika wa hayo makanisa ni wasindikizaji wa safari ya mbinguni. Mi nilikua muumini wao nikagutuka kule sio kusali ni kupoteza mda.
Babu wa loliondo aliyekuwa anawaombea, kuwatapisha na kuwatoa mavirus viongozi wakubwa wa kitaifa hakuwa mchungaji wa KKKT? Wacha kujitoa ufahamu? Ogopa wchungaji au maaskofu wasiowajibika popote kama akina Gwajima, mzee wa bapa, mwingira, kakobe and the like....janjajanja nyingi.
 
Sijui nini kimewakuta Au kwa vile the one in power ni mkristu mwenzao ? Wakati wa kikwete nyaraka za maaskofu zilikua bandika bandua
Kwa hiyo ni upande huu tuu ? Wale was Azana haiwahusu!!

Au sielewi!
 
Babu wa loliondo aliyekuwa anawaombea, kuwatapisha na kuwatoa mavirus viongozi wakubwa wa kitaifa hakuwa mchungaji wa KKKT? Wacha kujitoa ufahamu? Ogopa wchungaji au maaskofu wasiowajibika popote kama akina Gwajima, mzee wa bapa, mwingira, kakobe and the like....janjajanja nyingi.
Gwajima wamempiga stop
 
huyo nabii amosi ndio huyu amosi makala aliyetumbuliwa Ukuu wa nkoa
 
Huyu askofu huwa anajitambiua sana pamoja na yule wa Karagwe Askofu Bagonza na Askofu Munga. Hawa wengine akina Kakobe, Pengo, Gwajima ni maaskofu wa kukemea uzinzi na ulevi tu lakini maovu wanayofanyiwa binadamu wao hawaoni
 
Back
Top Bottom