Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,615
TAMKO LA KAMATI YA UTETEZI YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA DHIDI
MAMIA YA WANAFUNZI WA ZANZIBAR KUFUTIWA USAJILI WA MTIHANI (ACSEE 2013)
Ikiwa bado machozi hayajatukauka katika nyuso zetu kwa tukio la Mei mwaka huu baada ya maelfu ya wanafunzi wa Zanzibar kubatilishiwa
matokeo yao ya somo la Dini "Islamic Knowledge" ya Kidato cha Sita kwa mwaka 2012 na linaloitwa Baraza la Mtihani Tanzania (NECTA) .
Aidha, ni miezi michache tu tangia kufutiwa kwa matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne(CSEE) mapema mwezi Februari mwaka huu
ambapo wanafunzi 3,303 kati ya wanafunzi 450,324 waliofanya mtihani mwaka mwaka 2011 na kuifanya nchi yetu Zanzibar kuwa muhanga mkuu
wa suala hili kwa zaidi ya shule ya 30 kufutiwa matokeo hayo ikwemo Skuli ya Sekondari Mazizini, Hamamni, Mikumguni, Regeza Mwendo,
Filter, Laureate, High View na nyingi nyenginezo.
Katika hali isyotarajiwa, mnamo tarehe 22/12/2012 skuli mbali mbali za sekondari hapa Zanzibar zilipokea barua yenye Tarehe 18/11/2011
kutoka Baraza la mtihani Tanzania (NECTA) zilizoorozesha majina mbali mbali ya wanafunzi ambao tayari walishatambuliwa usajili wao kabla na
hatimae kubatiliwa usajili wao katika barua hizo.Miongoni mwa shule zilizokumbwa na kadhia hio kwa Mkoa wa mjini Magharibi ni pamoja na
Haile Sallasie (wanafunzi 56), Mwanakwerekwe "C" (36), Hamamni (35), Chukwani (15), K/samaki (12), Kiponda (11), Laureate (10) ,
Vikokotoni (3) na kwa upande wa Pemba ni Mchangamdogo (24) na CCK Kiuyu (8) na nyingi nyengine ambazo bado takwimu zake hatuzipata
kwa wilaya mbali mbali Zanzibar , idadi hizi zinakamilisha jumla ya wanafunzi 215 waliofutiwa usajili huo kwa skuli hizi 11 tu.Kwa mujibu wa barua
hizo, wanafunzi hao wamezuiliwa usajili kwa kisingizio cha kutotimiza sifa za kuwa na alama 5 (5 PASSES) katika matokeo ya mitihani yao ya
Form IV "Certificate of Secondary Education Examination "(CSEE) ukizingatia wanafunzi hao walitangazwa na kupangiwa shule mbali mbali na
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar mnamo April mwaka 2011 na ambao walitarajiwa kufanya mtihani yao ya ACSEE mnamo
February 2013.Kwa masiktitiko na hudhuni kubwa, leo hii tunaletewa taarifa kuwa wanafunzi hawa hawana sifa za kufanya mtihani huo (ACSEE)
katika kipindi ambacho tayari wameshakamilisha mashariti (conditions) yote muhimu ya mtihani huo ambapo ni pamoja na kulipia ada ya 45,000
Tsh (registration fee) na kufanya "project" na wamebakisha miezi 2 tu kufanya mitihani hiyo.Kwa kuwa hali hii inakandamiza juhudi za serikali yetu
tukufu katika kuendeleze na kukuza kiwango cha elimu pamoja na kupambana na Umasikini Zanzibar na vile vile kuhatarisha kushuka kwa
kiwango cha wasomi nchini kwetu na hatimaye kudunisha maendeleo ya Zanzibar.Kufuatia kadhia hii, Wanafunzi wa sekondari kutoka shule mbali
mbali za Mkoa wa Mjini Magharibi ikwemo Hamamni, Haile Sallasie, Vikokotoni, Chukwani, Mwanakwerekwe "C", Kiponda, na Lumumba
tuliamua kukutana pamoja siku ya Jumamosi ya 25/11/2012 ili kuweza kuungana kupigania haki za wanafunzi wenzetu ambao kwa sasa wapo
katika hali tatanishi.Katika mkutano huo ambao ulihudhuriwa na zaidi ya wanafunzi 70 ikiwa ni wawakilishi kutoka shule mbali mbali , tuliamua
kuteau kamati maalumu kuweza kufanikisha utetezi wa suala hili ambayo iko chini ya ndugu Omar S. Omar (Mwanakwerekwe "C") ambaye ni
mweyekiti wa kamati hio akisaidiwa na Rahma Mbarak Shaali (Vikokotoni), makamo mwenyekiti wa kamati hio ya muda, naye ndugu Rashid
Mohammed Rashid (Lumumba) alichaguliwa kuwa ni Msemaji wa Kamati hio pamoja na ndugu Saleh Abdallah Khatib (Haile Sallasie)
alichaguliwa kuwa Katibu, zaidi ya viongozi hawa wane (4) kamati pia imeundwa na wajumbe wengine 8 ambao ni Said Bakar Said
(Mwanakwerekwe "C") , Seif Khamis Mbarouk (Vikokotoni), Aisha Moh'd khamis (Mwanakwerekwe "C") , Mohammed Khatib Mohammed
(K/samaki), Hamad Khamis Ahmed (Kiponda), Hassan Ally shee (Lumumba), Suleiman Juma Khamis (Kiponda), na Haji Ali Abdalla
(Vikokotoni).Kamati iliweza kuandaa maadhimio manne (4) ambayo yameweza kufikishwa katika sehemu husika ambayo ni haya yafuatayo ,
kwanza, "Tunaitaka Wizara ya Elimu na Mafunzo Ya Amali Zanzibar
(WEMA) kuhakikisha wanafunzi wote walofutiwa usajili wanasajiliwa na kufanya mitihani mnamo tarehe 08/02/2013 kama wanavyotarajiwa
kufanya wanafunzi wengine", Pili, " wanafunzi wote wa Zanzibar wa Msingi na Sekondari kwa kitu kimoja kupinga uamuzi batili wa Baraza la
mtihani Tanzania NECTA na kuwa tayari kuungana pamoja kutetea na kulalamikia kadhia hii katika ngazi zote zinazohusika" , Tatu, "Kamati mbali
mbali za wazazi za shule za Zanzibar na wazanzibar wote Unguja na Pemba kuwaunga mkono wanafunzi hawa katika kudai haki zao", na Mwisho
ni "Tunawaasa Wanafunzi wote Zanzibar kuwa pamoja na kushiriki maandamano ya Amani yatakayoratibiwa na Kamati endapo tatizo hili
halitopatiwa ufumbuzi kwa wakati stahiki".Katika kufanikisha maadhimio hayo Kamati imeweza kwa kushirikiana na vyombo mabli mbali vya
habari kufikisha ujumbe huu kwa walengwa na wahusika , kamati iliweza kufanya vipindi cha moja kwa moja na vya habari kupitia Radio Nuru Fm,
Hits Fm na Zenji FM, Tv Iman, Radio Iman, ZBC Tv na vyingi vyengine.
Kutokana na juhudi za kamati kutaka kuonana na Waziri wa Elimu Zanzibar kugongwa mwamba, kamati imeweze kupeleka barua rasmi katika
wizara hio husika kulalamikia kadhia hio pia kamati imepeleka barua za malalamiko kwa Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi.Zaidi ya majibu
aliotoa Katibu wa Wizara ya elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Kupitia kituo cha Zenji Fm radio tarehe 26/11/2012 kuwa watalifanyia kazi
suala hili na majibu ya Waziri wa elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mh: Ali Juma Shamuhuna kwa kusema NECTA na Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi Haiwapi ushirikiano wa Kutosha katika baadhi ya maamuzi ya mambo yao hususani yanayoyohuisana na mitihani , vile vile na
kauli ya Muheshimwa Makamo wa Kwanza wa Raisi Maalim Seif Sharif Hamad kuzitaka wizara mbili hizi za elimu kukaa pamoja kulitafutia
ufumbuzi suala hili, aliyoyasema ofisi za wizara ya Elimu Mazizini Zanzibar mnamo 27/11/2012, Kamati bado haijapokea majibu yoyote rasmi
kutoka sehemu husika na vile vile haijaridhishwa sana na majibu yaliyotolewa na hivo inasisitiza hatua za haraka kuchukuliwa.
Mwisho, Kamati inasiisitiza kuweza kupatiwa ufumbuzi wa haraka kwa suala hili kwani huenda likaleta janga kubwa katika mustakabali mzima wa
elimu katika nchi yetu ya Zanzibar
MSEMAJI MKUU WA KAMATI,
………………………….
RASHID MOH'D RASHID (LUMUMBA )
Email: Rashidmohd1@live.com 28/11/2012