Tamasha la "Wasanii wa Mabadiliko"

Tamasha la "Wasanii wa Mabadiliko"

VIPI ROMA na yeye alikuwepo?? Kama bado na yeye ajiunge na TIMU.

peperusha BENDERAAAAA
VIVA ROMA
 
Hiyo ndo akili...strategic campaign! Lowasa na campaign team yake wako vizuri
 
Safi sana wasanii wa mabadiliko. Rasimisheni ushirika wenu halafu muwe na number za Mpesa, Tigo na airtel money tuwaunge mkono financially na vibuku, jero msimbazi si unajua sie ni malofa wenzenu

wazo zuri sana hili...ili ikiwezekana wapite kila pembe ya hii nchi
 
Mauno mauno ndio mtaji wao. Sasa wasemapo kuwa hicho ni kioo cha jamii, sijui ni jamii gani hiyo.
ImageUploadedByJamiiForums1441962583.102329.jpg
 
Wamakonde wameahidi shughuli zote za kiuchumi kusimama Tar 21/09/2015 kwaajili ya mapokezi ya mgombea urais wa UKAWA. Wamehimiza watu kufanya manunuzi sokoni na madukani siku moja kabla ya tukio hilo.
Waambatane na Viva Roma
 
Kweli huu mwaka mtam vyama vinatumia rasilimali zao kwa nguvu zote
 
Msimu wa mavuno huu, kama msanii amelala inakula kwake. Wengine Chadema wengine CCM.
 
Ikitokea wakazunguka nchi nzima watafunika kampeni za wagombea uraisi wote.
 
Nimefurahi na kufarijika sana sana tena sana kwa hawa wasanii kukubali mabadiliko na kujiunga na sisi Malofa na Wapumbavu sisi tupo bega kwa bega nao na tutaziunga mkono kazi zao za sanaa.
 
Safi wasanii wa mabadiliko mko juu..kanyaga twende karibu tutafika
 
tupia number ya tigo pesa tuwachangiye nauli na malazi !
 
Nimesikia jana kwenye radio station moja nikacheka sana.
Eti mkoloni anasema alienda kwenye mkutano mmoja wa mgombea akakuta kakusanya nyomi ya watu, kwa hiyo akaamua kudadisi na kumtoa mtu mmoja kwenye ule umati na kumuuliza kafuata nini hasa pale.
Anasema ndio akamwambia yeye kafuata kofia maana jua kali sana.
20150907040704.jpg

Msanii Mkoloni akiimba katika Tamasha la Wasanii wa Mabadiliko lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Mtwara. Lengo la Tamasha hilo ni kuwahimiza wananchi kujitokeza kupiga kura Oktoba 25, 2015.
 
Back
Top Bottom