Tall building a threat to Ikulu

unajua mkuu akili za viongozi wetu (sijui ni waafrika sote) zina walakini na inatupasa kufanya kazi zaidi ili kuuondoa huo uwalakini au kuukubali!

Raisi mwingine mstaafu yeye aliona 'ujiko' ilikuwa ni kuishi maeneo ya Msasani kwa vile Nyerere ndipo aliishi akaamua kufight na kupata kiwanja pale kwa imani kuwa ndicho 'kitongoji' cha wakubwa. Mwingine naona amependelea milimani huko lakini huwezi jua labda huyu kaamua ajenge hapohapo ikulu ili isiwepo tofauti baada ya kuachia madaraka!

Lile jengo lina maelezo mengi lakini nilivyofuatilia tangia mwanzo, ni kweli walioko madaraki wanaelewa kiachoendelea na la kuchukua appartments za juu ni yale yale ya EPA. Kwamba serikali inachukua floors za juu alafu inakuwa inalipa kodi mara 20 ya bei za soko kwa kisingizio kuwa ni 'kulinda usalama wa ikulu' wakati akaunti inayopokea hizo pesa imilikiwa mmoja wa hao.
Tutaambiana mbele ya safari


 
Hilo jengo ni blunder na litabakia kuwa aibu ya uongozi uliokuwepo wakati linajengwa!
 
MI niishauri serekali ilinunue jengo hilo ili walitumie kwa shighuli za ki usalama zaidi, au lipewe kwa usalama wa taifa. si sahihi kabisa kwa jengo refu kama hilo kujengwa ikulu. kama kawa serekali ilikuwa imelala mpaka likafikia hapo, TAKUKURU mpo hapo??.
 
Mkuu UTAJUA acha kuishi katika zama za kufikirika, dunia yetu imebadilika sana mtu anayetaka kufanya madhara ikulu haitaji kupanda juu ya mtu mrefu au ghorofa jirani na ikulu. Mhalifu makini ambaye ndiye real threat ya usalama wa ikulu na nchi kwa ujumla kwa msaada wa teknolojia ya kisasa anaweza kufanya lolote bila hata kuisogelea ikulu wala Tanzania. hivyo tuache woga tuna tatizo kubwa la makazi mijini inapotokea watu wenye uwezo wanashusha majengo kama hayo tusiwakatishe tamaa kwa visingizio vya kiusalama visivyokuwepo.
 
Hilo jengo ni blunder na litabakia kuwa aibu ya uongozi uliokuwepo wakati linajengwa!

chiligaji alikuwa waziri enzi hizo. Na nakumbuka mwaka jana alibanwa kwenye facebook na akajitetea kuwa yeye hakuhusika ila ni manispaa. Mimi navyoona solution ni kubomoa tu.
 
hakuna jipya chini ya jua siku hizi hata matapishi nayo watu watahalalisha kuwa chakula upumbavu mtupu kwa hiyo kama teknolojia imekua ndo watu waishi holela holela, basi hakuna haja ya kuvaa nguo tembeeni uchi kwa sababu teknolojia imekua.THINK BIG and be a reasonable man.
 
dalili za serekali inayoanguka ni kushindwa kung'amua hata vinavyoonekana kwa macho.." MUSA alipogeuza maji kuwa DAMU misri farao aliagiza wachawi wake pia wageuze machache yaliyobaki kuwa DAMU ili wamjibu MUSA...instead ya kuyageuza yaliyokuwa DAMU kuwa fresh tena..." MWISHO WA DORA HII UKO KARIBU SANAAA
 

Hili suala limenza kuongelewa humu JF tangia msingi unaanza kujengwa pale. Wengine tulikuwa tukipata chakula cha mchana pale tunapaita Holiday Out! Hata Container la CCM limeondolewa pale imekuwa parking.

Nadhani walijiridhisha.
 
mbaya zaidi kulikuwa na open space ambayo watoto wa mitaani walikuwa wakicheza mpira wameichukua na kuigeuza parking
 
Tulishaijadili hii miaka 10 iliyopita. Nitatizo kwa usalama wa rais wetu,lakini kwa rais kama wa Marekani sio tatizo kwani walinzi wake watayatumia hayo magorofa kuning'inia na kudhibiti usalama wote. Hakuna intelijensia ya Kamanda Mwema na Kova itakayoruhusiwa maeneo hayo. Kwanza system zote za mawasiliano zitazimwa.
 
Haya mabo yanaweza kutokea Tanzania tu ambako wenye pesa ndiyo wanaiamulia serikali ifanye nini
 
wale jamaa wameshapigwa stop, wameambiwa wakajenge pale karibu na uhamiaji zamani karibu na station maeneo ya tra. W0ashaanza kujenga tayari. itakuwa gorofa 22.
 
Hili suala limenza kuongelewa humu JF tangia msingi unaanza kujengwa pale. Wengine tulikuwa tukipata chakula cha mchana pale tunapaita Holiday Out! Hata Container la CCM limeondolewa pale imekuwa parking.

Nadhani walijiridhisha.
Mkuu Kimbunga nimekumbuka mbali ulivyotaja Holiday Out tunakula pale halafu watoto wa IFM tunawapeleka Holiday Inn maisha haya.

Kujenga ghorofa pale wala sio tatizo tukiona Ikulu ya Hong Kong au Kuala Lumpur zilivyozungukwa na maghorofa wala tusingelalamika na kighorofa kimoja.
 
Last edited by a moderator:
Jengo lenyewe ni mali ya serikali kupitia LAPF, hata hivyo Ikulu rasmi itahamia Dodoma na pale Magogoni itabakia Ikulu pale wanpokuwa Dar kikazi.
 
Wewe umekurupuka na kuangalia usalama kama kuchungulia ndani. Kumbe usalama ni pamoja na faragha ya rais na kujua nani kaingia nani katoka. Majasusi watapanga ktk hilo jengo na kufuatilia nyendo za kila anayeingia ikulu
 

Kumbe mkuu ritz nawe ulikuwa ukienda pale kwa akina Mkongwe na group lake kupata msosi wa kiswahili na samaki wa ferry huku ukitozwa na vijana wa IFM! Kile kilikuwa kijiwe changu mkuu hasa pale kwa yule General Mstaafu kama unampata ambaye ndiye mwenye ile nyumba.
 
Last edited by a moderator:

Wakati naingia jeshini eti mnafundishwa kuji camouflage kwa kutembea na kichaka. Unabeba chaka unakimbia hadi mahala unapozi kisha unacharge na chaka lako! Siku hizi ukikimbia na chaka mtu anakuona tu akiwa mbaaaali anakutumia kitu kinakusambaratisha; manake atashangaa kuona chaka lina move!

Mkuu kweli siku hizi mambo ni high tech! Unatumiwa ndege isiyo na rubani inakufuata hadi chumbani na hai miss target. Hilo la kuchungulia physically wala halina shida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…