Talaka, ni suluhu ya migogoro ya ndoa?

Nakubaliana na wanaosema talaka ni suluhisho la "last resort". Njia nyingine zikishindwa, badala ya kuendelea kuishi katika hali ya kutegana; akikosea nammaliza; basi talaka ndo njia inayopendekezwa na wataalam wengi. Talaka haiepukiki kwenye mahusiano yaliyokwisha haribika na talaka ni suluhu haswaa.

Tatizo wengi wanatoa au kuomba talaka kama fimbo ya kuwachapia wenzao hasa pale wanapoona wenzao hawana kipato cha kuwakidhi pindi ndoa inapovunjika. Haya ni matumizi mabaya. Ila kwa kutatua migogoro iliyoshindikana ni afadhali talaka.
 
inategemea na aina ya matatizo.kama makubwa mno,talaka is the best option.mfano mume au mke imegundulika anataka kumuua mwenzake,mfano umeweka sumu kwenye chakula,au mume kutembea na mtoto wake{kwa upande wangu mimi,hilo halivumiliki}nitamuamini vipi huyo mume tena?au unapigwa kila siku,ukiendelea kukaa mwisho utakuwa kilema.ila matatizo madomadogo unajitahidi kukomaa nayo

Kisukari mfano wako nimeukubali, ila si unajua binadaamu hususan wanandoa tunapaswa kuwa na mioyo ya kusamehe hususan kwa tatizo kama la kupigwa?
 
Talaka ni kitu kibay Yet sio jibu au suluhu ya migogoro ya kindoa

Matatizo ya ndoa ili yapate majibu ya kweli ni wahusika :)embarassed2::embarassed2::embarassed2::embarassed2::embarassed2:) kukaa na kushughulikia tofauti zao wakimshirikisha Mungu ili shetani asipate nafasi ya kuwapa mafundisho ya uongo kuona kuachana ndio majibu

Hahitajiki mtu wa tatu ktk matatizo ya ndoa

Ni Mungu na WAWILI wahusika

...kuna neno umelisahau hapo....Linaitwa (KUKUBALI "KWA ROHO SAFI")....
huwezi sema wahusika wakae iwapo mmoja, au wote hawajaridhia.
 
As much as TALAKA sio kitu kizuri, Sometimes ni suluhisho..... Kuna vitu havivumiliki jamani.... Kuna vitu vinauma Mno!!!

...naaam, tena kwa msisitizo nakubali liwe suluhisho la mwisho kuokoa
"uhai" wa mhusika au wahusika.... Kinachouma sio njaa, kiu, au tumbo...

Kwenye mapenzi kinachouma ni ROHO!
 
Mhuuuu! imebidi nigune kwa urefu.
Hii ni ishu tata na tambuka.

Hata sijui kama ni suluhisho, jambo la kuogofya, au ni ujinga. Maana heshima ya kuwa na ndoa watu tunaipenda lakini yaliyoko huko ,ni utata mtupu na saingine watu hawana talaka lakini pia ndoa huna , kwa maana ya uhalisi wa maisha ya ndoa.

Sijui hata kama nimesema jambo lenye mashiko ( substance) hapo juu lakini ngoja tusikie wanazuoni wengine watasemaje.

Binafsi yangu, topic hii inanigusa kiaina maana....
 
Wanawake wamekili kuwa ni kweli wanatoa vipigo kwa sababu wengi wamekuwa wanaume wa kuvaa Suluali tu, hawana lolote kuanzia Chumbani hadi Sebuleni, na wengine wanaishia kwenye Ulevi na wanawake, wakisahau wajibu wao kama Baba wa familia. Hayo ni ya Nairobi, hebu jiulize Ndoa yako ikoje? Ungefanyika utaratibu wa kukusanya taarifa za kila Ndoa, tungeshangaa kuona unyanyasaji mkubwa zaidi ya huo wa wenzetu wa kenya. Watu usiku hawalali ni mizozo usiku kucha utafikiri Vuvuzela, Ukatili wa kupigana na kutukanana ni mambo ya kawaida, Uaminifu katika Ndoa unakuwa adimu, upendo wa kweli na Furaha vinapotea kila kunapokucha, Vitendo vya kutelekeza familia na kuhamia kwa nyumba ndogo vinaendelea kushamiri, hivi mnafikiri kununiana mnapokuwa mumekoseana ndiyo suluhisho? Hilo ni pepo la hasira, tunalikemea kwa jina Yesu litoke, ili tabasamu na vicheko virudi.


Mtumishi wa Mungu Paulo anasema “Tukijua neno hili ya kuwa utu wetu wa kale ulisulubishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike” Wewe mwanaume na mwnamke unayejiita Mtu wa Mungu, Sulubisha miguu yako isipige mateke wenzio wala kunyatia nyumba za wageni kwa Zinaa, Sulubisha Midomo na Ulimi visitoe matusi na kupiga kisi makahaba na wezi wa mapenzi pia visulubiwe ili visilambe Vileo, Sulubisha macho yasiwe mepesi kukonyeza wake na waume za watu na yasione yasiyofaa, Sulibisha mikono isiwe myepesi kupigana na kukumbatia vifua vya asiye mpenzi wako, Sulubisheni Moyo usijae tama mbaya ya zinaa, hasira, chuki, kiburi, ukaidi, Roho mbaya, visasi n.k. Viungo vyote vya siri vinavyowaka tamaa mbaya ya mwili vinapaswa kulubishwa. Neno linasema “Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulubisha MWILI pamoja na MAWAZO yake mabaya na tama zake” Wagalatia 5:24. Matatizo yote yanayozikabili Ndoa za siku hizi yanasababishwa na wanandoa kutokuwa na Yesu katika maisha yao. Kusulubisha mwili ni kuua Utu au Tabia za Kale za Dhambi na kuzaliwa katika Kristo kwa Imani ili tuwe na Upendo ambayo ni tabia ya Mungu.
 
Back
Top Bottom