Bundewe
JF-Expert Member
- Jun 14, 2011
- 400
- 141
Katika uchaguzi wowote, ni jambo la kawaida kuwa na kura chache zinazoharibika, hii inatokana na mambo mengi ikiwa ni pamoja na uelewa mdogo wa baadhi ya wapiga kura, maelekezo kuwa na utata au hata wapiga kura kupiga "kura za maruhani" kama ilivyotokea miaka ya nyuma huko Pemba.
Takwimu za uchaguzi wa ubunge katika jimbo la Bariadi Magharibi 2010 hata hivyo zinashangaza ambapo inaonesha kwamba Chenge amepata kura 50,107 = 30%, Isaac Cheyo kura 34,298 = 20% kura zilizoharibika ni 78,171 = 46%. Inawezekanaje kura zilizoharibika kuwa nyingi kiasi hiki? Nyingi kuliko kura alizopata mshindi??? Hii sio namna nyingine ya kuchakachua matokeo.....?
Katika jimbo hilo hilo, kura za urais zilizo haribika ni 3,047 sawa na 3.3%.
Takwimu za uchaguzi wa ubunge katika jimbo la Bariadi Magharibi 2010 hata hivyo zinashangaza ambapo inaonesha kwamba Chenge amepata kura 50,107 = 30%, Isaac Cheyo kura 34,298 = 20% kura zilizoharibika ni 78,171 = 46%. Inawezekanaje kura zilizoharibika kuwa nyingi kiasi hiki? Nyingi kuliko kura alizopata mshindi??? Hii sio namna nyingine ya kuchakachua matokeo.....?
Katika jimbo hilo hilo, kura za urais zilizo haribika ni 3,047 sawa na 3.3%.