Takukuru yenye meno, sio tu ya maneno

Takukuru yenye meno, sio tu ya maneno

G. Activist

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
482
Reaction score
125
Mh. Silinde Mbunge wa Mbozi Magharibi, anahitaji PCCB wabadirike wasiwe ni watu wakuongea tu, bali iwe ni takukuru yenye meno pia.

Takukuru yetu inameno tena makali kweli, kwenye rushwa ndogondogo, ila mafisadi wanaoweza kutikisa nchi, hao takukuru yetu imewashindwa kabisa.... Tunaenda wapi?????
 
Takukuru ni mbwa alie ng'olewa meno ili asije aka ng'ata hadi wamiliki wake. Ndiyo maana makali ya Takukuru ni kwenye kukamata watoa na wapokea rushwa wadogo tu.
 
Inawezekana viongozi wengi wako makini katika kufanya vitendo vya kifisadi kwa kuwatumia wasaidizi wao na hivyo kuwa vigumu kuwakamata wao wenyewe. Ni kama ilivyo biashara ya unga ambapo suppliers wakubwa siyo rahisi kukamatwa na wanabaki kukamatwa watu wadogo wadogo wanaobeba kete chache kwenye matumbo yao.
 
Nimeona kwenye itv jioni hii. Takukuru wamejipongeza kwa kupeleka kesi tano za ufisadi.
 
ni kweli mkuu usipate shida hata mwanafunzi hujipongeza kwa kuongoza ktk darasa lake bila kuzingatia uwezo wa washindani wake hivyo hosea yuko sahihi kujipongeza maana anaona amefanikiwa wakati sisi tunaona hakuna kitu kafanya na hivi sasa yuko hewani kupitia itv na se.munzv
 
Sioni sababu ya kujipongeza eti kwa kupeleka kesi 5! wameshinda hizo kesi?! tena hawa ndio walarushwa wakubwa! udhaifu huo!!!
 
Sioni sababu ya kujipongeza eti kwa kupeleka kesi 5! wameshinda hizo kesi?! tena hawa ndio walarushwa wakubwa! udhaifu huo!!!

kwa kweli ni taasisi ya kustawisha rushwa tu hapo bongo
 
mnafiki huyu sijawahi kuona....Mbunge Laizer na mwenzie walipokamatwa kwa kutoa rushwa wakati wa uchaguzi wa magamba mwaka 2007 aliamuru kamanda wa mkoa asitangaze, wakati habari zinamfikia kamanda wa mkoa wa Arusha tayari press conference ilikuwa inaendelea....kilichofuatia ni uhamisho kwa kamanda kwenda Manyara, na yule wa Arumeru akatupwa kusini....kesi haikufikiswa mahakamani na Laizer anatamba mitaani. Mama Batilda alikamatwa kwa kutoa rushwa wakati wa uchaguzi wa 2010.( alikamatwa saa nne usiku yeye huyo huyo akaamuru aachiwe na wasimfuate fuate (kumbukeni jinsi kamanda Lema alivyo wavamia PCCB arusha kwa kutofanyia kazi taarifa walizokuwa wanapewa). Kilichofuata ni kuwalima uhamisho watumishi wa takokuu wapatao 8 wakati kampeni zimepamba moto....huyu ni mnafiki tu kama wanafiki wengine wa TISS
 
Tatizo lenu wabongo ni kuongea bila kuwa na chanzo sahihi cha Taarifa...mmezoea kuyapika majungu tu sasa sielewi dizaini huwa mnatumwa kuja kusema mineno ya uongo humu kwenye JF??? Tushukuru hata huyu Hosea ametoa taarifa yake kwenu wananchi namna alivyotekeleza malengo yake...hivi ni nani kiongozi wa chombo cha dola ambaye huwa na courage ya kuongea nasi wananchi kama Hosea???!!!acheni majungu na uongo bana...jamaa ni jembe sio mchezo...mimi kwa umri wangu nilioishi sijawahi kusikia Ma-hosea wa miaka ya nyuma wamefanya lolote pale TAKUKURU!!!???alikuwepo mjeshi pale akatoka kapa bila hata kufikisha angalau kigogo mmoja mahakamani...tujaribu basi hata kumpongeza Hosea kwa mzigo alioupiga katika hii miaka michache aliyokalia kile kiti...
Najua ipo mijitu inatumwa kuleta majungu humu ili wananchi tumuone Hosae hachapi kazi acheni huo u-pimbi nyie wehu, angalau mwana awe anapongezwa hata kama hakufaulu kwa asilimia 100 darasani enyi makalaghabaho...!!!
 
Kitu cha kwanza kukifumua tukipata chama kingine kushika dola ni TISS,PCCB na Police!!hatushangai maana ndio zao kushafisha mafisadi
 
Mnasahau hao wavutaji wa rushwa wadogo kama polisi wanaweza kuua mamia barabarani...rushwa ni rushwa tu, kama wanawakamata wala rushwa wadogo tuwapongeze basi kwani wanasidia mpate hata asprini pale muhimbili nyie pimbi, wasingekuwa wao tungetoa rushwa hata kupata panadol hospitali.
Mimi nawashangaa sana wabongo wenzangu...hivi hiyo mikesi mikubwa ya akina mramba, yona, liyumba, mataka, mgonja, mahalu na wengineo wengi ni kesi ndogo???...mnataka baba zenu wapelekwe mahakamani ndio muone ni kesi kubwa...kalaghabaho wa mawazo kweli nyie...!!!
 
Back
Top Bottom