TAKUKURU yawakamata aliyekuwa makamu wa rais wa kampuni ya Acacia, Deo Mwanyika na Alex Lugendo

Mmexico

JF-Expert Member
Nov 1, 2016
369
328
Boss wa zamani wa ACACIA Deo Mwanyika (Vice president) jana alilala Lupango akihusishwa na tuhuma za rushwa alizofanya akiwa madarakani.

Mwanyika amekamatwa jana pamoja na ofisa mmoja wa Serikali Mr Lugendo na kulala kituo cha polisi SURRENDER na leo atafikishwa Mahakama ya kisutu kusomewa mashtaka.
Hawa wataongezeka kwenye list ya maafisa wa zamani na wasasa wa ACACIA/Serikali/NGO's na wawakirishi wa wananchi wanaohusishwa na rushwa za ACACIA.
Naona JPM kawashika pabaya sana hawa jamaa, ngoja tuone mwisho wake.

=====

Dar es Salaam. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imemkamata aliyekuwa makamu wa rais wa kampuni ya Acacia, Deo Mwanyika na Alex Lugendo ambaye ni mshauri wa Serikali ndani ya kampuni hiyo ya uchimbaji madini.

Mwanyika aliyejiunga na Acacia mwaka 2001 akiwa ameitumikia kampuni hiyo kwa nafasi mbalimbali kwa miaka 17, alitangazwa kujiuzulu Agosti 24 kwa barua ya ofisa mtendaji mkuu wa Acacia, Peter Galeta kwenda kwa wafanyakazi wote wa kampuni hiyo.

Akizungumza na Mwananchi jana, naibu mkurugenzi mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo alisema wanawashikilia wawili hao tangu juzi na leo wanaweza kufikisha mahakamani kwa hatua zaidi.

“Tumewakamata kwa tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi katika tasnia ya madini,” alisema Mbungo.
“Lakini hawa wakiwa viongozi waandamizi walishindwa kusimamia nchi ipate mapato kama ilivyotakiwa.”

Naibu mkurugenzi huyo alisema wamefanya mahojiano na watuhumiwa hao kwa kipindi kirefu.
“Baada ya kukamilisha mahojiano tangu tulipowakamata jana (juzi), leo (jana) tuliwapeleka mahakamani lakini kutokana na sababu zilizojitokeza walishindwa kupandishwa kizimbani lakini kesho (leo) natarajia itawezekana,” alisema.
IMG-20181017-WA0019.jpeg
 
acacia itaondoka na wengi sana.. maana ilikuwa project kubwa sana yenye hela nyingi sana.. tangu enzi za barrick...

sitashangaa kumuona mzee wa madili na yeye akawemo.. joka la makengeza. ila jela hatakuwemo maana wanasema kasoma havard majaji wanamuogopa
 
Ile mahakama ya mafisadi ilikua na haja ya kuwepo kweli?
Ipo kwa ajili ya akina nani? Ni kwamba mahakama zilizopo zilishindwa kazi au kesi za ufisadi ni nyingi kiasi kwamba zilihitaji mahakama maalum?
Ilikuwa na haja kuwepo but kwa sasa haina haja, sababu tunaleana na kuoneana huruma
 
........................., kuna watu walitafuna nchi hii kushoto-kulia..... with thinking kwamba, their crimes will never catch up with them. At the end of the day there is only one lesson in life. Crime doesn't pay. Hata asingekuwa JPM someone else would have held these guys accountable. In one way or another.

They fleeced the mining sector with impunity!

My only wish, let these people have their day in court. wajibu makosa yao.

JPM na madhaifu yake yote, hakika kwa wenye nia ya kuelewa ametufundisha somo kubwa sana... .....Wakati si milele!
 
Boss wa zamani wa ACACIA Deo Mwanyika (Vice president) jana alilala Lupango akihusishwa na tuhuma za rushwa alizofanya akiwa madarakani.

Mwanyika amekamatwa jana pamoja na ofisa mmoja wa Serikali Mr Lugendo na kulala kituo cha polisi SURRENDER na leo atafikishwa Mahakama ya kisutu kusomewa mashtaka.
Hawa wataongezeka kwenye list ya maafisa wa zamani na wasasa wa ACACIA/Serikali/NGO's na wawakirishi wa wananchi wanaohusishwa na rushwa za ACACIA.
Naona JPM kawashika pabaya sana hawa jamaa, ngoja tuone mwisho wake.View attachment 900753
Hakuna dhambi isiyokuwa na expiry date.
Mwanyika alitesaaa huku akishiriki kuiibia nchi sasa yamefika mwisho
 
acacia itaondoka na wengi sana.. maana ilikuwa project kubwa sana yenye hela nyingi sana.. tangu enzi za barrick...

sitashangaa kumuona mzee wa madili na yeye akawemo.. joka la makengeza. ila jela hatakuwemo maana wanasema kasoma havard majaji wanamuogopa
Huu unafiki una mwisho wake.Muda wa huyo anaemlinda ukiisha kama atakuwepo atafikishwa kwenye sheria.Muda Huu walitakiwa waondoke.
 
........................., kuna watu walitafuna nchi hii kushoto-kulia..... with thinking kwamba, their crimes will never catch up with them. At the end of the day there is only one lesson in life. Crime doesn't pay. Hata asingekuwa JPM someone else would have held these guys accountable. In one way or another.

They fleeced the mining sector with impunity!

My only wish, let these people have their day in court. wajibu makosa yao.

JPM na madhaifu yake yote, hakika kwa wenye nia ya kuelewa ametufundisha somo kubwa sana... .....Wakati si milele!
"Wakati si milele" hilo neno ujue hata yeye linamgusa kama anatenda uovu juu ya wanadamu wenzake!
 
Back
Top Bottom