TAKUKURU baada ya Aveva, kamateni pia Anna Tibaijuka, askofu Kilaini na wengine

magode

JF-Expert Member
Oct 2, 2014
2,201
3,322
Wanabodi, Salaam;

Jana kuna taarifa zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii juu ya kukamatwa kwa mwenyekiti wa Simba FC na baadae kuthibitishwa na maafisa wa TAKUKURU kwa kile walichoeleza kuwa Aveva alichepusha fedha za usajili wa Emmanuel Okwi. Yaani makosa ya Aveva ni kupitisha fedha za simba kwenye akaunti yake binafsi.

Sakata la Aveva halina tofauti na sakata la fedha za Escrow alizogawa James Lugemalira kwa baadhi ya taasisi lkn fedha hizo zikaingizwa kwenye akaunti binafsi. Mfano, askofu msaidizi wa jimbo la Bukoba Methodius Kilaini pesa za kanisa ziliingizwa kwenye akaunti yake binafsi, halikadhalika Anna Tibaijuka aliwekewa pesa za shule katika akaunti yake.

TAKUKUU huenda wakati ule haikuwa na makali kama haya iliyonayo kwa sasa. Nawakumbusha hilo deal. Pia ikibidi na wale waliotajwa kubeba fedha kwenye viroba katika benki ya Stanbic. Isiwe nongwa kwa Aveva tu.

Nawasilisha!
 
Nimekuwa najiuliza iwapo Rais wa klabu ya Simba Bw.Aveva amekamatwa Kwa kosa la kuhamisha Fedha kutoka Akaunti ya Klabu ya Simba Na kuziweka kwenye Akaunti yake.

Nilidhani kosa alilokamatiwa Rais huyo kosa hilo limefanywa pia na Anna Tibaijuka na Askofu Kilaini kwa kuwekewa fedha kwenye akaunti zao binafsi badala ya akaunti ya Shule na Kanisa, mbona hawa hawajakamatwa?
 
Haupo sahihi mkuu, kwa mujibu wa mama Tibaijuka alidai kwamba zile hela zilikuwa msaada kwa ajili ya shule yake.

Ni dhahiri hela zile zilitolewa kwa njia ya hundi, sasa hatujui kwamba hundi ile iliandikwa majina ya nani(Payee).

Kama iliandikwa majina ya mama basi ilikuwa ni sahihi kuingia kwenye account yake. Lakini kama iliandikwa majina ya shule(Payee) badala yake ikaingizwa kwenye account ya mama hapo pana tatizo.

La Aveva inaonyesha hela ilitumwa moja kwa moja kwenye account yake na siyo account ya SSC, kisha yeye akaanza kufanya miamala kwa watu tofauti.

Simba wanadaiwa TRA, wamekwepa makusudi kulipa kodi.
 
Haupo sahihi mkuu, kwa mujibu wa mama Tibaijuka alidai kwamba zile hela zilikuwa msaada kwa ajili ya shule yake. Ni dhahiri hela zile zilitolewa kwa njia ya hundi, sasa hatujui kwamba hundi ile iliandikwa majina ya nani(Payee).

Kama iliandikwa majina ya mama basi ilikuwa ni sahihi kuingia kwenye account yake. Lakini kama iliandikwa majina ya shule (Payee) badala yake ikaingizwa kwenye account ya mama hapo pana tatizo.

La Aveva inaonyesha hela ilitumwa moja kwa moja kwenye account yake na siyo account ya SSC, kisha yeye akaanza kufanya miamala kwa watu tofauti.

Simba wanadaiwa TRA, wamekwepa makusudi kulipa kodi.
 
Haupo sahihi mkuu, kwa mujibu wa mama Tibaijuka alidai kwamba zile hela zilikuwa msaada kwa ajili ya shule yake.

Ni dhahiri hela zile zilitolewa kwa njia ya hundi, sasa hatujui kwamba hundi ile iliandikwa majina ya nani(Payee).

Kama iliandikwa majina ya mama basi ilikuwa ni sahihi kuingia kwenye account yake. Lakini kama iliandikwa majina ya shule(Payee) badala yake ikaingizwa kwenye account ya mama hapo pana tatizo.

La Aveva inaonyesha hela ilitumwa moja kwa moja kwenye account yake na siyo account ya SSC, kisha yeye akaanza kufanya miamala kwa watu tofauti.

Simba wanadaiwa TRA, wamekwepa makusudi kulipa kodi.
mh!
 
Ni wajibu wa mleta uzi kutokuwa mjinga au kuzuia kusambaza ujinga wake kwa umma. Kosa la Aveva si kupitisha pesa za SS kwenye akaunti yake binafsi bali ni kuchepusha malipo ya Okwi yasipitie akaunti ya SS ili kukwepa kodi ambayo SS inadaiwa na TRA (an intentionally committed crime to evade SS' tax onus). Pesa ya Tibaijuka haikukusudia kukwepa kodi ya shule yake - iwe yeye binafsi au shule. Shule yake haikuwa na deni la kodi. Tena angekuwa na mpango wa kukwepa kodi basi pesa ile angeichepushia kupitia akaunti ya shule. Lakini alifanya kinyume chake. Tayari TRA imemfikisha mahakamani, alionekena na hatia ya kutolipia kodi ya mapato husika (siyo kukwepa kodi). Amelipa zaidi ya sh. millioni 500 ikiwa ni kodi ya mapato aliyoyapata kutoka kwa Rugemalira. Kilaini alipokea sadaka na kuipeleka kanisani kwake. Ndio maana hata TRA hawajaangaika kumdai kodi. Kuna utaratibu wa kisheria ku-declare mapato ya msaada TRA alioufuata. Tibaijuka hakufanya hivyo ikala kwake. Tusichanganye mambo.
 
Haupo sahihi mkuu, kwa mujibu wa mama Tibaijuka alidai kwamba zile hela zilikuwa msaada kwa ajili ya shule yake. Ni dhahiri hela zile zilitolewa kwa njia ya hundi, sasa hatujui kwamba hundi ile iliandikwa majina ya nani(Payee).

Kama iliandikwa majina ya mama basi ilikuwa ni sahihi kuingia kwenye account yake. Lakini kama iliandikwa majina ya shule (Payee) badala yake ikaingizwa kwenye account ya mama hapo pana tatizo.

La Aveva inaonyesha hela ilitumwa moja kwa moja kwenye account yake na siyo account ya SSC, kisha yeye akaanza kufanya miamala kwa watu tofauti.

Simba wanadaiwa TRA, wamekwepa makusudi kulipa kodi.
Hakika uko sahihi
 
Wanabodi,
Salaam;

Jana kuna taarifa zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii juu ya kukamatwa kwa mwenyekiti wa simba fc na baadae kuthibitishwa na maafisa wa Takukuru kwa kile walichoeleza kuwa Aveva alichepusha fedha za usajili wa Emmanuel okwi.

Yaani makosa ya eveva ni kupitisha fedha za simba kwenye akaunti yake binafsi.

Sakata la aveva halina tofauti na sakata la fedha za escrow alizogawa James Lugemalira kwa baadhi ya taasisi lkn fedha hizo zikaingizwa kwenye akaunti binafsi. Mfano,askofu msaidizi wa jimbo la bukoba methodius kilaini pesa za kanisa ziliingizwa kwenye akaunti yake binafsi,halikadhalika Anna Tibaijuka aliwekewa pesa za shule katika akaunti yake.

Takukuru huenda wakati ule haikuwa na makali km haya iliyonayo kwa sasa. Nawakumbusha hilo deal. Pia ikibidi na wale waliotajwa kubeba fedha kwenye viroba ktk benki ya stanbic. Isiwe nongwa kwa eveva tu.

Nawasilisha!
Hujatoa sababu za kimsingi badala yake unaonekana umekurupuka. Ni kwanini umeunganisha haya matukio? Ni kwanini kati ya lundo la wanufaika wa escrow umeishia kuwaona hao wawili pekee na kuwaacha wengine? unafananishaje jambo X na Y?
 
Alichofanya Aveva ndicho alichofanya Rage kweny mauzo ya Samatta na ochan bahati mbaya kwake huu ni utawala mwingine na umelenga kuwabana wakwepaji kodi na wala rushwa ila ni vema takukuru ikarudi toka nyuma kusudi iwabane toka nyuma ndio watajua kwanini hivyo vilabu vinalalamika havina pesa na pia wamshugurikie Idd Simba kwani alifanya mchzo huohuo wakati uda ikiuzwa
 
Ni wajibu wa mleta uzi kutokuwa mjinga au kuzuia kusambaza ujinga wake kwa umma. Kosa la Aveva si kupitisha pesa za SS kwenye akaunti yake binafsi bali ni kuchepusha malipo ya Okwi yasipitie akaunti ya SS ili kukwepa kodi ambayo SS inadaiwa na TRA (an intentionally committed crime to evade SS' tax onus). Pesa ya Tibaijuka haikukusudia kukwepa kodi ya shule yake - iwe yeye binafsi au shule. Shule yake haikuwa na deni la kodi. Tena angekuwa na mpango wa kukwepa kodi basi pesa ile angeichepushia kupitia akaunti ya shule. Lakini alifanya kinyume chake. Tayari TRA imemfikisha mahakamani, alionekena na hatia ya kutolipia kodi ya mapato husika (siyo kukwepa kodi). Amelipa zaidi ya sh. millioni 500 ikiwa ni kodi ya mapato aliyoyapata kutoka kwa Rugemalira. Kilaini alipokea sadaka na kuipeleka kanisani kwake. Ndio maana hata TRA hawajaangaika kumdai kodi. Kuna utaratibu wa kisheria ku-declare mapato ya msaada TRA alioufuata. Tibaijuka hakufanya hivyo ikala kwake. Tusichanganye mambo.
Wengine ndo tunasikia leo km Tibaijuka alifikishwa mahakamani. Ahsante kwa ufafanuzi. Hebu nisaidie kidogo,umesema Tibaijuka alifikishwa mahakamani na kuilipa TRA zaidi ya Tsh.500/=ml. Hapo unamaanisha alikutwa na hatia au mahakama alimwamuru alipe kodi tu aliyoikwepa!!??
 
Pesa yote ya Escrow ilitumwa kwa bank transfer...TISS hakuna hundi!! Direct toka Mkombozi kwenda kwa Mama Tiba! Msipindishe maneno!
Haupo sahihi mkuu, kwa mujibu wa mama Tibaijuka alidai kwamba zile hela zilikuwa msaada kwa ajili ya shule yake. Ni dhahiri hela zile zilitolewa kwa njia ya hundi, sasa hatujui kwamba hundi ile iliandikwa majina ya nani(Payee).

Kama iliandikwa majina ya mama basi ilikuwa ni sahihi kuingia kwenye account yake. Lakini kama iliandikwa majina ya shule (Payee) badala yake ikaingizwa kwenye account ya mama hapo pana tatizo.

La Aveva inaonyesha hela ilitumwa moja kwa moja kwenye account yake na siyo account ya SSC, kisha yeye akaanza kufanya miamala kwa watu tofauti.

Simba wanadaiwa TRA, wamekwepa makusudi kulipa kodi.
 
Back
Top Bottom