Takataka tanzania

mjukuu2009

Member
Jul 6, 2009
89
4
Kumekuwa na tabia yakutupa takataka ovyo ovyo apa nchini kwetu sasa sijui amna mamlaka za kusimamia ili swala au ndio mamlaka ziko likizo!?uku mtaani kimara matangini kwetu ata ilo gari lakutupa taka alijawai kupita karibuni mwaka sasa watu wameamua kutupa taka mtoni au kwenye mifereji.
Kitu kingine kinacho sikitisha ni tabia ya watu kulakula ovyo kwenye magari na wakimaliza kula au kunywa wanafungua dirisha anatupa bila kujali,aswa watu wanaoendesha magari ya kifahari kama vile Prado/VX/benz/range rover na wakiongozwa na magari ya serikali,sasa mpaka mtu ana kuwa mkurugenzi serikalini lakini hana elimu yakutunza mazingira hii inamanisha apa Tanzania Elimu inayotolewa haitusaidi au haitoshelezi!?
Nawaomba mjirekebishe jamani vyeo vyenu na matendo yenu ni tofauti.kufagia gari ni rahisi kuliko kufagia barabara kwani barabara zinaanzia km3 kwenda juu wakati gari nzima ni mita3 maximum.
Asante,tuzidi kukumbushana nchi haina pesa za kulipa wafagizi kila sehemu.
 
Back
Top Bottom