Taifa ni salama zaidi, likibakia chini ya CCM

Taifa ni salama zaidi, likibakia chini ya CCM

Ukawa hawajajipanga...

Hawana watu wasiozidi hata mkono mmoja wenye weledi wa kusimamia rasilimali za Taifa hili...

Wapo katika kujaribu bahati yao ya kwenda Ikulu...

Mustakabali ya maisha ya watu si mahali pa mizaha na maabara za uongozi,

Nimekua nikifuatilia kauli na mienendo ya viongozi wategemewa wa Chadema, NCCR, CUF na NLD, kwa ujumla wake, wanakosa weledi, uzalendo na nia ya dhati kututoa katika changamoto kama Taifa,

Wengi wao, wanajaribu bahati zao.....

Sasa ni hatari mno, kumpa mtu nafasi ambayo alikua akijaribu tu bahati yake, bila kua na mipango dhabiti ya kuitumikia nafasi husika.

Mwananchi ipe thamani kura yako, kwa kuiacha nchi katika mikono salama ya CCM.

Ukawa, nakuhakikishia, hakuna watu wa kulipeleka taifa hili mbele.

Oktoba 25, fanya Uchaguzi sahihi, linda nchi yako.

mkuu stroke nadhani unashindwa kutofautisha salama,amani na utulivu.
 
Last edited by a moderator:
Kwa vile una ulaji CCM. Umeona lakini watoto wetu na mama zetu huku ninyi mkiwa na vitambi. Subirin laana ya Mungu ninyi na vizazi vyenu. Watu hawawezi kuharibu nchi hivi na Msipate hadhabu mbele ya Mungu. Mheshimiwa Magufuli mwenyewe ni shahidi ni kwa vile tu hana jinsi yuko tayari kuikimbia CCM. Angalia mweshimiwa anavyosema jinsi CCM imetesa wananchi. Hotuba zake ni kama mpinzani wa CCM ni kwa vile tu ninyi mmeshiba na hamjihi kilio cha mtanzania. Angalau kidogo Mheshimiwa Magufuli anajua na amesema CCM kuja mafisadi. Ninamaliza,
 
kwa sasa ccm wamebaki wachumia tumbo tu na majizi. hakuna jipya. ni wakati wa kuingiza kizazi kipya kuendeleza nchi yetu..
 
Ukawa hawajajipanga...

Hawana watu wasiozidi hata mkono mmoja wenye weledi wa kusimamia rasilimali za Taifa hili...

Wapo katika kujaribu bahati yao ya kwenda Ikulu...

Mustakabali ya maisha ya watu si mahali pa mizaha na maabara za uongozi,

Nimekua nikifuatilia kauli na mienendo ya viongozi wategemewa wa Chadema, NCCR, CUF na NLD, kwa ujumla wake, wanakosa weledi, uzalendo na nia ya dhati kututoa katika changamoto kama Taifa,

Wengi wao, wanajaribu bahati zao.....

Sasa ni hatari mno, kumpa mtu nafasi ambayo alikua akijaribu tu bahati yake, bila kua na mipango dhabiti ya kuitumikia nafasi husika.

Mwananchi ipe thamani kura yako, kwa kuiacha nchi katika mikono salama ya CCM.

Ukawa, nakuhakikishia, hakuna watu wa kulipeleka taifa hili mbele.

Oktoba 25, fanya Uchaguzi sahihi, linda nchi yako.

lugha za vitisho kama bwana pombe hazitakiwi, wache wananchi waamue wenyewe, nyie ndio mtaleta maasi
 
Ukawa hawajajipanga...

Hawana watu wasiozidi hata mkono mmoja wenye weledi wa kusimamia rasilimali za Taifa hili...

Wapo katika kujaribu bahati yao ya kwenda Ikulu...

Mustakabali ya maisha ya watu si mahali pa mizaha na maabara za uongozi,

Nimekua nikifuatilia kauli na mienendo ya viongozi wategemewa wa Chadema, NCCR, CUF na NLD, kwa ujumla wake, wanakosa weledi, uzalendo na nia ya dhati kututoa katika changamoto kama Taifa,

Wengi wao, wanajaribu bahati zao.....

Sasa ni hatari mno, kumpa mtu nafasi ambayo alikua akijaribu tu bahati yake, bila kua na mipango dhabiti ya kuitumikia nafasi husika.

Mwananchi ipe thamani kura yako, kwa kuiacha nchi katika mikono salama ya CCM.

Ukawa, nakuhakikishia, hakuna watu wa kulipeleka taifa hili mbele.

Oktoba 25, fanya Uchaguzi sahihi, linda nchi yako.
Zikiwa zimebaki siku chache sana kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Urais, Ubunge na udiwani hali ya Kisiasa imefikia patamu sana.Bila kumumunya maneno naomba niseme hali ya Chama cha Mapinduzi ni dhoofu sana.Wananchi wamepania kutoa adhabu kali kwa CCM na wagombea wake wa Urais, Ubunge na Udiwani Nchi nzima. Hii ni kutokana na mambo 40 yafuatayo ambayo CCM na Serikali zake imeshindwa kuyatatua kwa muda wa miaka 54 iliyokuwepo madarakani;


1. Kushindwa kutimiza ahadi nyingi zilizotolewa wakati Benjamin Mkapa anaomba ridhaa na zile lukuki ambazo Jakaya Kikwete aliahidi kushindwa kabisa kuzitekeleza.
2. Huduma mbovu za afya (Hospitali hazina dawa,Utendaji mbovu na miundombinu hafifu)
3. Elimu duni katika shule za Serikali kutokana na ukosefu wa Vitabu,walimu,maabara,mabweni,viwanja vya michezo na miundombinu rafiki n.k
4. Watumishi wa Umma kutokupata maslahi yao kama mishahara kwa wakati,malipo ya likizo,usafiri,kujiendeleza n.k
5. Migogoro ya ardhi iliyoasisiwa na Viongozi walafi na wenye tamaa
6. Migogoro ya wakulima na wafugaji (Kiteto,Malinyi,Kongwa n.k)
7. Ushuru wa mazao kwa wakulima kuzidi kipimo kiasi cha kuwakatisha tamaa
8. Wavuvi kubanwa kwa matumizi ya nyavu zilizozuiliwa wakati wafanyabiashara wanaziuza bila tatizo lolote
9. Rushwa iliyokithiri kupitiliza (Imeathiri watu wa kipato cha chini kwa Kiasi kikubwa)
10. Ubovu wa barabara za kuunganisha Mikoa,Wilaya na Kata
11. Sheria kandamizi dhidi ya Wawekezaji wa ndani,wafanyabiashara na wajasiriamali,
12. Utesaji wa Wananchi (Operation Tokomeza)
13. Ukosefu wa ajira kwa vijana na wanawake
14. Kukosekana kwa mikopo nafuu kwa ajili ya kuwakwamua wanawake na vijana.
15. Ajira za upendeleo (BoT,TRA,Uhamiaji)
16. Mgao wa Umeme pamoja na kukosekana kwa nishati hii maeneo mengi nchini
17. Magonjwa ya mlipuko kama Kipindupindu
18. Ajira za watoto machimboni,biashara ndogondogo na Serikali haina hata mpango wa kuwaokoa,
19. Michango kandamizi na kodi mbalimbali
20. Wakulima kukopwa mazao yao waliyotumia jasho kubwa kuzalisha
21. Wakulima kukosa pembejeo na masoko kwa ajili ya bidhaa zao
22. Viongozi kutobiwa nje badala ya kuboresha Hospitali zetu
23. Viongozi kulipana mishahara mikubwa na posho lukuki ilhali walipa kodi maisha yao kuwa magumu.
24. Kufa kwa Viwanda ambavyo viliajiri watu wengi na kuzalisha bidhaa bora za Tanzania
25. Bidhaa zisizo na viwango kujazana Tanzania pasipo jitihada za kuzizuia
26. Nchi kugeukla kuwa ya kutumia bidhaa za nje kuliko za ndani
27. Siasa za Maji taka (Matusi,kejeli,vijembe badala ya kutoa hoja kwa wananchi)
28. Serikali kutokutoa sapoti kwa Viwanda vya ndani pamoja na wawekezaji Wazalendo
29. Mlolongo wa kodi na michango kwa wawekezaji wa ndani (Hudidimiza maendeleo yao)
30. Matumizi mabaya ya madaraka kwa Viongozi wa Umma na Wanasiasa
31. Uharibifu mkubwa wa Mazingira na Serikali kutokuchukua hatua stahiki
32. Mlolongo wa Taasisi zinazokusanya Mapato kwa wawekezaji wadogo kama TRA,OSHA,TCCIA,TBS,WCF,Industrial Licence,Busness Licence,CESS za Halmashauri za Vijiji na Wilaya,TANESCO,NEMC,Maji etc
33. Msongamano wa magari katika Majiji na miji na jitihada ndogo za kukabiliana na tatizo husika
34. Taifa kutokuwa na vipaumbele na utatuzi wa matatizo kuwa wa kuzima moto
35. Kauli chafu za wanasiasa na Viongozi waandamizi baada ya kuwa wamevimbiwa madaraka
36. Katiba isiyokidhi wakati na hali ya Kisiasa,Kiuchimi na Kiutamaduni.
37. Taifa kupoteza misingi ya umoja,mshikamano na kudharaulika duniani kote
38. Tatizo la madawa ya kulevya yanayoingizwa Nchini na Wafanyabiashara wanaofahamika
39. Matumizi ya vyombo vya dola kuwanyamazisha wapenda mabadiliko kwa manufaa ya CCM
40. CCM kuishiwa pumzi ikiwa katikati ya mlima na dereva kuonekana dhahiri akiwa amepoteza dira na mwelekeo asijue la kufanya!!!
Kwa wakati huu,nathubutu kusema,Naichagua UKAWA,...sio kwa sababu za uimara wa CDM,CUF,NLD,NCCR MAGEUZI ama Uimara wa UKAWA la hasha!!Ila ni kwa sababu ya udhaifu wa CCM na ahadi ilizoshindwa kuzitekeleza kwa miaka 54 mfululizo.“ALUTA Continua, Victoria Ascerta”.... “The Struggle Continues, Victory is Certain”; ...Mapambano yanaendelea, Ushindi unakuja!!
 
Magufuli anasema ataanzisha Mahakama ya mafisadi ,Bila kusema nitabadili katiba Kama si usanii ni nini,

Kuna mawili ,

1) utakuwa unafaidika na ccm kwa njia moja au nyingine kwa kupewa hela , kwa kipindi ichi tena hela yenyewe haizidi laki tano, au inakazi ccm au mzazi wako ndio anapo patia kula Yake na Kutuibia vilevile

2) ama akili Yako ni ndogo Sana na hatistaili ata kukujibu au kukuelewesha kwa sababu hautaelewa ata aje Nani ,. Na Hilo pole Sana
Mkuu cha muhimu ni kuwa na uthubutu wa kuwashughulikia mafisadi na majizi,kiongozi mwenye guts za kuwatia mbaroni majizi/mafisadi/wakwepa kodi sugu ni Mh.Magufuli basi,viongozi wa vyama vingine specifically CHADEMA hawana ubavu/nia thabiti ya kutuondolea balaa la kudi hilo ovu,narudia kuwakumbusheni kwamba EDO hawezi hata siku moja kuwatia mbaroni wapiga deal wenzake badala yake atawakabidhi visima vyetu vya gesi na mafuta,migodi ya madini,kandarasi zote nchini,mbuga za wanyama,ranch zote nchini - wewe usione wafanya biashara wakubwa wanamu-finance wazi wazi na wengine kwa kificho mkafikiri wana uchungu wa kweli wa kuleta mabaliko ya kweli nchini wao na EDO ni waigizaji tu nia yao waingie IKULU wafanye mambo yao hawatakuwa na habari na walala hoi wala nini sijui - Kambarage was right all along yeye kama mwalimu aliye kubuhu kwenye nyanja za kuwasoma watu aliwahi kumkatalia hasiwe Rais wa Taifa letu kwa sababu na ushahidi wa kweli,repeat Mwalimu had good reasons kumkatalia na sababu ziko valid mpaka sasa in otherwords hajabadirika chochote zaidi ya cosmetic change lakini deep down yuko vile - labda niwaulizeni swali dogo,tangu lini mkamuona EDO amevaa nagwanda ya CHADEMA sasa kisaikolojia what does that tell U about his PERSONA? got it! Hana time na CHADEMA wala UKAWA yeye na Mh.Mbowe wote wanadanganyana kila mtu anamtumia mwenzake kwa lengo maalum, sina nia ya kumsema vibaya lakini nataka kuwakumbusha Watanzania wenzangu kwamba tusifanye makosa ya kukabidhi Taifa letu Viongozi ambao hawatabiriki na wenye track record yenye walakini mkubwa - tukifanye majaribio jamani mpaka tuje kumpata Putin taifa letu litakuwa limepigika kweli kweli kiuchumi kuliko Urusi enzi za Yeltsin mimi sichoki kuwakumbusha hilo kila siku,EDO aendeleze biashara zake na maranch mambo ya kutaka Urais asahau,mwalimu aliwahi kumpa ushauri kama huo Mh.Mrema lakini akampuuzia baada ya kulewa na ushebeki wake kulisukuma gari lake kila anako pita walipo mpachika jina la Urais ndio kajisahau kabisa akijiona kana kwamba njia ya kwenda IKULU tayari, kasahau kwamba watu wanao udhulia mikutano ya kampein ni asili mia 30 ya idadi ya wapiga kura wote naona na Lowassa ama amini hivyo!! CCM ilisha ng'amua ukweli wa asili mia 30% ndio maana inafanya mambo yake kimya kimya - come 25th Obtober CCM itawashangaza sana.
 
Back
Top Bottom