Taifa hili...............

Taifa hili...............

Taifa ambalo punda wa masikini ni punda wa kweli na wanatumika kubeba mahitaji muhimu ya binadamu wakati huo huo punda wa mafisadi ni binadamu wenzao na wanatumika kubeba madawa ya kulevya.
 
Taifa ambalo linaendeshwa Kwa matukio hili kuwapumbaza raia wake.
Taifa la wananchi wavumilivu duniani mpaka majirani zetu wanatushangaa.
Taifa la watu wanafiki kuwahi kutokea,kwani kabla ya uchaguzi wananchi wanaonekana kuwa na ari ya kuleta Mabadiliko lakini wakati wa uchaguzi wanachagua chama kilekile wanachokilalamikia Kwa umaskini na shida zao
 
taifa pekee duniani ambalo linaruhusu fao la kujitoa.....its positive kwa sisi wa hali ya chini
 
si kwa kuwa matumaini ya kesho yemefifia mkuu
taifa pekee duniani ambalo linaruhusu fao la kujitoa.....its positive kwa sisi wa hali ya chini
 
Taifa ambalo wananchi elfu ishirini wanaporwa ardhi na serikali na kupewa mzungu bureeeeee. Taifa ambalo wachimbaji wadogo wanaporwa machimbo yanapewa wazungu. Hakika haya mawili yanaweza kuleta machafuko.
 
Taifa lenye watu wengi wanaojua vyanzo vya matatizo ya nchi ila wanaishia kunyoshea kidole kwa viongozi wakati mabadiliko yanaanza kwa mtu mmoja tena bila kujali wa pembeni yako atabadilika au laa...
 
Taifa ambalo ukiwa upinzani wewe ni muuaji na gaidi
 
Taifa ambalo lina wachambuzi wa siasa wengi kuliko nchi zote za maziwa makuu.......
 
Taifa ambalo maksi zikiwa juu wanafunzi hufaulu, na maksi zikishushwa wanafunzi hufeli
 
Taifa ambalo hata mkuu wa kaya hajui nikwanini nchi ni maskini na watu wake wanaishi maisha yakifukara'' wakati nchi ina utajiri mwingi.
 
taifa ambalo muiba kuku anachomwa moto bali muiba mali za uma anajinafasi mtaani tu
 
Taifa ambalo serikali yake inaeendeshwa kwa kauli mbiu
 
Taifa ambalo wanafunzi hawajui kusoma na kuandika lakn wanafaulu mtihani wa taifa.
 
Taifa ambalo wananchi wanakula mapanki ya samaki minofu inaenda Ulaya.
 
Taïfa ambalo mkuu wa nchi anawajua wauza un ga il à hataki kuwataja
 
Taifa linalo iga mambo ya BRN kutoka Malasya wakati mazingira yake ni tofauti
 
Taifa ambalo intelijensia inakamata wapinzania hku ikishindwa kukamata watoto w mbwa mwitu, hku rpc mwenyewe makengeza akibwelabwela 2
 
Back
Top Bottom