Tahadhari ya Mvua kwa mikoa ya Pwani

Tahadhari ya Mvua kwa mikoa ya Pwani

ni maeneo ya buyuni-chanika,
wamesombwa na maji ya mvua.
Hali ni mbaya,

sijui jinsi ya ku-upload picha wa dau mtanisamehe!
poleni..... Ila na wewe sahihisha kingereza chako kwenye kchwa cha habari ukishindwa omba msaada tutani.....
 
Sio siri maeneo mengi ya Dar kwa sasa ni hatari kwa kuishi na iwapo mvua itaendelea kwa masaa kadhaa kuanzia sasa tutrajie maafa makubwa mno.

EE MWENYEZI KWAKO TUNAOMBA KILA KILICHO CHEMA IKIWAMO MVUA YENYE KULETA NEEMA PIA NA SIYO MAAFA KAMA TUNAYOANZA KUYASHUHUDIA KWA SASA.
 
Wamekufa baada ya basi la UDA kujaribu kupita kwenye mkondo wa maji ya mvua yaliyokuwa yakipita juu ya barabara na basi hilo kusukumwa na maji hadi pembezoni mwa barabara, ndipo raia hao waliruka na kuchukuliwa na maji hayo yaliyokuwa na kasi kubwa yakitokea milima ya Kisarawe.
 
serikali kupitia kitengo cha maafa wachukue hatua za makusudi!!

Dar siyo salama tena!!

PM hana habari yuko dodoma anakomaa na serikali mbili mambo ya maafa mtajiju
 
Wamekufa baada ya basi la UDA kujaribu kupita kwenye mkondo wa maji ya mvua yaliyokuwa yakipita juu ya barabara na basi hilo kusukumwa na maji hadi pembezoni mwa barabara, ndipo raia hao waliruka na kuchukuliwa na maji hayo yaliyokuwa na kasi kubwa yakitokea milima ya Kisarawe.

Usichanganye mambo, mwenzio Anasema Buyuni wewe unazungumzia UDA, kama anamaanisha UDA basi hapo sio Buyuni
 
mfanyakazi mwenzetu nyumba imemeguka hapo nyuma ya ubungo plaza chumba kimoja kimedondoka jioni hii maafa mazito
 
ni maeneo ya buyuni-chanika,
wamesombwa na maji ya mvua.
Hali ni mbaya,

sijui jinsi ya ku-upload picha wa dau mtanisamehe!

poleni sana eheenyi wananchi wa chanika buyuni.....pia pole kwa wakazi wa jiji la dsm kwa ujumla kwa wale waliopatwa na maafa sehemu mbalimbali kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
 
Nipo buyuni. Nimepita kwashida sana jirani kwa pinda na kipawa mpya. Hali ni mbaya
 
According to mkuu wa mkoa wa dsm waliothibitika kufariki ni 10.
 
Back
Top Bottom