Tahadhari-wizi wa ajabu Dar!

Tahadhari-wizi wa ajabu Dar!

kerubi afunikaye

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2013
Posts
1,183
Reaction score
1,061
Ninayeongea nanyi ni shuhuda mara mbili wa wizi husika.Kumetokea aina mpya ya wizi hapa jijini Dar ambapo mwizi hutumia aina fulani ya maji ambayo ukinyunyiziwa unabaki umeduwaa au unazimia.

Wiki tatu zilizopita jirani yangu mwenye biashara ya tigo pesa aliibiwa sh milioni 9 baada ya wezi hao kufika eneo lake la biashara na baada ya kumshika usoni mfanyakazi wake aliduwaa na wezi hao kubeba pesa zote.Hata hivyo wiki iliyopita wezi hao walikamatwa baada ya uchunguzi wa askari na kesi inaendelea.

Leo hii muda wa jioni nilipigiwa simu na staff mwenzangu akilia kwamba amerudi nyumbani na kukuta housegirl wake akiwa hoi huku tv,music system pamoja na fedha vikiwa vimeibiwa.

Nilikwenda huko na tukafuatilia na kugundua kuwa msichana huyo alikuwa akisumbuliwa kwa kutongozwa mara kwa mara na mtu asiyejuana naye vizuri kiasi cha kuzoeana hadi kumwelekeza nyumbani na alikuwa akija kumtembelea jamaa anapokuwa kenda kazini yeye na mkewe na watoto wakiwa shule.

Baada ya kupata nafuu,msichana huyu ametueleza hayo na kusema kuwa leo hii jamaa alikuja na wenzie wawili akiwa na kichupa kidogo chenye maji mkononi na kumwagia usoni,akaanguka na kupoteza fahamu hadi alipostuka mbele yetu jioni hii.

Tumekuta nyumba imepekuliwa sana kama watu waliokuwa na muda wa kutosha kutafuta vitu na nadhani walikuwa wakitafuta pesa nyingi ingawa walikuta tu laki 8 kabatini.

Kilichonifanya niandike hapa ni taarifa tulizozikuta polisi kuwa matukio ya aina hii yameanza kushamiri sana hivi sasa na wamepokea malalamiko mengi ya aina hii na baadhi ya watu kukamatwa wakiwamo akina mama wawili wa kiarabu wanaodaiwa kumuuzia maji hayo mmojawapo wa watuhumiwa.Nawatahadharisha wakazi wenzangu wa Dar kuwa waangalifu.

Inasemekana wezi hummwagia mtu maji usoni au hujipaka mikononi ambapo wakimshika tu kwa mikono hiyo anapoteza fahamu.Sijafahamu kwamba maji haya ni kemikali zenye athari hiyo au ni ushirikina.

Naomba vyombo vya dola vifuatilie kwa undani na kukomesha wizi huu kama ilivyokuwa ule wa kuspray vioo vya magari.Mwenyezi Mungu mwenye haki atawakomesha wale wote wenye kuwaza uovu juu ya wenzao.Tafakari,chunguza,chukua hatua.
 
Kama ni kweli basi hii ni balaa. Vyombo vya dola onyesheni utaalamu wote. Taifa linawategemea.
 
Hapa Tanzania aina yetu ya usalama hutegemea sana upelelezi badala ya ukachero...

Aina hizi za matukio ni ngumu kidogo kwa wana usalama kuzisambaratisha kwa muda mfupi...
 
hatari!!Mungu mwenye huruma atuhurumie,maana...
 
Kweli bongo, bongo kweli yaaani mnamkuta mtu kazimia nyumba imepekuliwa mnakaa kusubiri housegirl aamuke ?????? Hayo maji mnajua yana nini??? Mnafahamu athari za hayo maji ??????? kweli tukio la namna hiyo mnaendelea kuishi kwenye nyumba tuuuu??????
Plsease iteni crime scene wafunge hiyo nyumba wataalamu wachunguze ni kitu gani hasa???/
 
Kweli bongo, bongo kweli yaaani mnamkuta mtu kazimia nyumba imepekuliwa mnakaa kusubiri housegirl aamuke ?????? Hayo maji mnajua yana nini??? Mnafahamu athari za hayo maji ??????? kweli tukio la namna hiyo mnaendelea kuishi kwenye nyumba tuuuu??????
Plsease iteni crime scene wafunge hiyo nyumba wataalamu wachunguze ni kitu gani hasa???/

Mkuu wakifunga nyumba wataishi wapi? Hayo mambo ulaya sio huku kwetu,huku sisi huku hatuishi bali tunadumu.
 
Ni bora hao wanazimisha tu kuliko wanaotumia risasi, visu,mapanga n.k kutoa uhai wa watu.
Hao unaweza kuepukana nao kwa kutoji'involve na strange people. Be smart sio kila mtu m'shake hands na issue za demu kuingiza ndani mwangu nshapga marufuku.
 
Nisha anza kuhisi harufu flan.
Kuna siku katika pitapita zangu nilikutana na mkusanyiko wa watu wengi nikaona itakuwa vyema na mimi nisogee nishuhudie kinachoendelea,Nilipofika nilmkuta kijana mmoja wa kiislam akiwa na wasaidizi wake watatu.Katika eneo hilo kulikuwa na Meza na vipaza sauti,Na wingi wa umati ule walikuwa ni Waislamu katika kufika kwangu yule Bwana alikuwa anaendelea kutoa maelekezo amabpo tayari kuna vijana na wakiume walikuwa kama nane wamejipanga Mstari mmoja mbele ya yule kijna wa kiislam,

Yule Kijana wa kiislam(ni mwite kiongozi)alitoa mafuta kwenye chupa akajipaka mkononi(kulia)huku mkono wa kushoto akiwa kashika mic,kiongozi huyu akamwendea mtoto moja baada ya mwingine akawa anamgusa kwenye paji la uso pamoja na maeneo ya puani huku akisema kwa sauti"majini hamna nafasi tena katika mwili wa mtoto huyu" mtoto akiguswa maeneo ya kwenye paji la uso na puani alikuwa akidodondoka kama mzigo huku wasaidizi wa yule kiongozi wakisaidia wale watoto kudondoka vizuri,alifanya hivyo kwa watoto woote nane,6 walidondoka ispokuwa wawili tuu hawakudondoka,

Kiongozi akawa anawauliza mtoto mmoja baada ya mwingne "nimekusukuma" watoto karibia woote walisema hapana akasema ila walihisi nini wakajibu "kizunguzungu" sikuendelea kukaka sana pale nilianza kuondoka huku akiwataka wanaume wengine nane wajongee mbele,nikiwa naendelea kupiga hatua kwa mbali nilmsikia kiongozi huyo akitamka ni mafuta yaliyotoka mbali,yamechanganywa na maj ka sio maji basi ya mafuta ya zAmzAm,Huku akihimiza ndugu zake waislam wanunue mafuta ya hayo ili kuchangia Gharama kidogo manake mafuta hayo yame panda ndege kuletwa huku,Yametoka Arabuni na Maji yametoka kwenye kisima Cha Mtume nani sijui(manake nilikuwa nisha fika mbali)

Kwaio maaskari Uchunguzi unaweza ukaanzia Kwenye Mafuta hayo,Kwa kuwauliza waathirika wa wizi huwo hayo maji harufu yake ilikuwaje, huku wakifananisha na hayo wanayotembezaga kwenye mi hadhara.Nna wasiwasi maji au mafuta hayo yakawa na uhusiano ispokuwa wezi washa anza kuyatumia kwa manufaa mabaya.

Ni maoni yangu uki Complain sio mbaya na wewe utakuwa ni Mtizamo wako Tuu.
 
Nisha anza kuhisi harufu flan.
Kuna siku katika pitapita zangu nilikutana na mkusanyiko wa watu wengi nikaona itakuwa vyema na mimi nisogee nishuhudie kinachoendelea,Nilipofika nilmkuta kijana mmoja wa kiislam akiwa na wasaidizi wake watatu.Katika eneo hilo kulikuwa na Meza na vipaza sauti,Na wingi wa umati ule walikuwa ni Waislamu katika kufika kwangu yule Bwana alikuwa anaendelea kutoa maelekezo amabpo tayari kuna vijana na wakiume walikuwa kama nane wamejipanga Mstari mmoja mbele ya yule kijna wa kiislam,Yule Kijana wa kiislam(ni mwite kiongozi)alitoa mafuta kwenye chupa akajipaka mkononi(kulia)huku mkono wa kushoto akiwa kashika mic,kiongozi huyu akamwendea mtoto moja baada ya mwingine akawa anamgusa kwenye paji la uso pamoja na maeneo ya puani huku akisema kwa sauti"majini hamna nafasi tena katika mwili wa mtoto huyu" mtoto akiguswa maeneo ya kwenye paji la uso na puani alikuwa akidodondoka kama mzigo huku wasaidizi wa yule kiongozi wakisaidia wale watoto kudondoka vizuri,alifanya hivyo kwa watoto woote nane,6 walidondoka ispokuwa wawili tuu hawakudondoka,Kiongozi akawa anawauliza mtoto mmoja baada ya mwingne "nimekusukuma" watoto karibia woote walisema hapana akasema ila walihisi nini wakajibu "kizunguzungu" sikuendelea kukaka sana pale nilianza kuondoka huku akiwataka wanaume wengine nane wajongee mbele,nikiwa naendelea kupiga hatua kwa mbali nilmsikia kiongozi huyo akitamka ni mafuta yaliyotoka mbali,yamechanganywa na maj ka sio maji basi ya mafuta ya zAmzAm,Huku akihimiza ndugu zake waislam wanunue mafuta ya hayo ili kuchangia Gharama kidogo manake mafuta hayo yame panda ndege kuletwa huku,Yametoka Arabuni na Maji yametoka kwenye kisima Cha Mtume nani sijui(manake nilikuwa nisha fika mbali)
Kwaio maaskari Uchunguzi unaweza ukaanzia Kwenye Mafuta hayo,Kwa kuwauliza waathirika wa wizi huwo hayo maji harufu yake ilikuwaje, huku wakifananisha na hayo wanayotembezaga kwenye mi hadhara.Nna wasiwasi maji au mafuta hayo yakawa na uhusiano ispokuwa wezi washa anza kuyatumia kwa manufaa mabaya.
Ni maoni yangu uki Complain sio mbaya na wewe utakuwa ni Mtizamo wako Tuu.

kweli upumbavu hauna ujazo

sasa na akina kakobe utasema wanatumia nini??
 
Back
Top Bottom