Tahadhari: Tabia za madereva kuingia na abiria kwenye vituo vya mafuta

shaks001

JF-Expert Member
Feb 6, 2014
1,246
1,070
Nchi yoyote duniani huongozwa na sheria na taratibu zake,hata hapa kwetu Tanzania naamini sheria hizo na taratibu zipo.Lakini kuwa na taratibu na sheria ni jambo moja,ila kutekeleza ni jambo linngine.

Kuna huu uvunjaji wa sheria tena wa wazi kabisa unaofanywa na baadhi ya madereva hasa wa magari ya abiria kuingia na abiria kwenye vituo vya kuweka mafuta(petrol station).Hivi tushawahi kujiuliza endapo inatokea ajali ya moto na abiria wapo hapo kwenye gari,nini kitatokea?Au tumezoea maafa yanapotokea ndipo tuanze kuunda tume ya uchunguzi?

Kuna mambo ya kuchezea lakini si usalama na maisha ya watu.Haitasaidia vifo vimetokea halafu Rais aanze kutoa salamu za pole kwa "familia zilizopoteza ndugu zao".Tuna nafasi ya kuzuia majanga mengine kwa kuzisimamia sheria na taratibu zilizowekwa.Na hata sisi abiria tuwe na kauli moja tunapoona madereva wanatuingiza kwenye vituo vya mafuta kwani kwa kufanya hivyo tutaweza kuepusha madhara makubwa.

Pamoja tunaijenga nchi yetu!
 
Nchi yoyote duniani huongozwa na sheria na taratibu zake,hata hapa kwetu Tanzania naamini sheria hizo na taratibu zipo.Lakini kuwa na taratibu na sheria ni jambo moja,ila kutekeleza ni jambo linngine.

Kuna huu uvunjaji wa sheria tena wa wazi kabisa unaofanywa na baadhi ya madereva hasa wa magari ya abiria kuingia na abiria kwenye vituo vya kuweka mafuta(petrol station).Hivi tushawahi kujiuliza endapo inatokea ajali ya moto na abiria wapo hapo kwenye gari,nini kitatokea?Au tumezoea maafa yanapotokea ndipo tuanze kuunda tume ya uchunguzi?

Kuna mambo ya kuchezea lakini si usalama na maisha ya watu.Haitasaidia vifo vimetokea halafu Rais aanze kutoa salamu za pole kwa "familia zilizopoteza ndugu zao".Tuna nafasi ya kuzuia majanga mengine kwa kuzisimamia sheria na taratibu zilizowekwa.Na hata sisi abiria tuwe na kauli moja tunapoona madereva wanatuingiza kwenye vituo vya mafuta kwani kwa kufanya hivyo tutaweza kuepusha madhara makubwa.

Pamoja tunaijenga nchi yetu!
hilo wameshalifanya wimbo wa taifa wa madereva wanajaribu kupingana na sheria,. yaan hata baada ya ile ajali ya city boys, still utawakuta njia salamu zao kama kawaida, mwenyezi atuepusho na majanga ya hvi
 
Mimi nimeshagombana na abiria wenzangu na madereva wengi kwa kesi kama hizo.....mara nyingi mimi huwa nashuka na kwenda kupandia mbele......
Kama ilivyo desturi ya waTanzania kukosa umakini na kutokujali hata katika mambo yanayogusa maisha yao.......

Usipo uthamini wewe uhai wako unadhani ni nani atauthamini.....!!!

Siku kukitokea ajali ya moto kwenye vituo vya kujazia mafuta..(Mungu epushia mbali) nadhani yatakuwa ni maafa ya kihistoria.......lakini yote haya yanaepukika kwa kuthamini uhai.....

Nimewahi kushuhudia dala dala linatuingiza kwenye vituo vya mafuta mchana wa jua kali......dah!!! Aisee Mungu aepushie mbali......
 
Ni hatari sana lakini cha ajabu madereva baadhi yao wanaona kawaida tu.

Likitokea lolote hapo watu wanaanza kulaumu
 
Kwenye hili sisi abiria ndio wenye matatizo aghalabu tumekua tukiruhusu hii hali.dereva ataingiza gari na tutakua kimya na ikitokea kukemea tutakemea wakati bado tuko humo humo
 
Kwenye hili sisi abiria ndio wenye matatizo aghalabu tumekua tukiruhusu hii hali.dereva ataingiza gari na tutakua kimya na ikitokea kukemea tutakemea wakati bado tuko humo humo

Kweli kabisa mkuu....mimi silaumu madereva wa madala dala......sisi abiria ni tatizo kubwa katika hili.....
Nimeshawahi kutukanwa mara nyingi kwa ajili kulikemea hili.....
Mimi hukemea na nikiona wenzangu wapo dhidi yangu mimi huchukua hatua zangu za kiusalama......
 
Kweli kabisa mkuu....mimi silaumu madereva wa madala dala......sisi abiria ni tatizo kubwa katika hili.....
Nimeshawahi kutukanwa mara nyingi kwa ajili kulikemea hili.....
Mimi hukemea na nikiona wenzangu wapo dhidi yangu mimi huchukua hatua zangu za kiusalama......
Pamoja na matatizo mengi yakiuzembe yanayosababishwa na madereva,bado sisi tumekua na mchango wetu kupelekea uzembe mwingi wa madereva tukubali tukatae sisi abiria hatuna umoja! !!
 
Mafuta yenyewe yamechakachuliwa mpaka utokee mlipuko ni asilimia chache....

Kuna kipindi hili abiria wenzangu walinikemea vibaya nilipomhoji dereva na konda wake safari yangu ilikuwa ngumu sana kilomita 55 niliziona kama elfu 5
 
Mm binafsi nilikuwa sijui kama ni kosa.
Hata juzi nilikuwa naenda mbagala dereva aliingia pamoja na sisi katika petrol station ya mbele ya taifa, na hakuna abiria aliyeshuka wala kukemea.
Hili nalo linahitaji elimu au mkazo wa sheria kwamba abiria atakayeonekana ndani ya usafiri wa uma wakati ukijaza mafuta, faini laki sita au miezi mitatu jela au vyote kwa pamoja.
 
  • Thanks
Reactions: ora
Naona ajali zote huko za magari ya abiria, wanaosababisha ni abiria wenyewe,nadhani itumgwe sheria, ajali inapotokea na abiria nao washtakie kwa kuzembea na kushindwa kukemea uzembe wa dereva.
 
Ase elimu ndiyo inaitajika coz hata mimi nilikuwa celewi.Asante sana mkuu kwa elimu hii na mimi ntakuwa mstari wa mbele kupinga jambo huli
 
Nimewahi kusimangwa na abiria wenzangu wa mbagala pale kipati kwa sababu ya kupinga jambo hili. Inatakiwa elimu kwa abiria..wanausalama nao wawe makini juu ya hili hasa pale kipati mida ya jioni
 
Kitu kikisha jadiliwa hapa jf ni lazma kilete madhara kwa watakao puuzia ni suala la mda tuwawapoteza ndugu zetu tu!!
 
Naona ajali zote huko za magari ya abiria, wanaosababisha ni abiria wenyewe,nadhani itumgwe sheria, ajali inapotokea na abiria nao washtakie kwa kuzembea na kushindwa kukemea uzembe wa dereva.
Pengine sheria ipo ila hamna wa kuzifuatilia
 
Ni makosa makubwa sana.. Mimi binafsi ajali zote zinazotokana na uzembe milele daima ntaendelea kulaumua abiria... Sisi ndo tupo ndan ya gar na uzembe tunauona ila tunakaa kimya alaf tunalaumu serikali , cjui sumatra mara trafiki.. Upuuz mtupu
 
Simu,sigara,milipuko nk.haviruhusiwi bank.Si mara moja wala mbili,kuona watu wanatumia simu bank na hakuna anayejali.Lakini unaweza kupata picha kama mtu atoa sigara na kuivuta?
 
Pengine sheria ipo ila hamna wa kuzifuatilia
Ni kweli nakumbuka kama sikosei makamba sr akiwa rc dsm alikataza magari kujaza mafuta yakiwa na abiria,baada ya muda ikapotea hiyo amri,lakini huko hii tabia imezoeleka kitu kitakatazwa baadae kinasahaulika,chukua mfano suala la kusimamisha abiria ndani ya daladala.
 
Back
Top Bottom