Tahadhari mtanzania

Nov 11, 2007
10
74
TAHADHARI MTANZANIA
1.1 Tafakari ni muhimu, kwa mja mwenye busara,
1.2 Kuwaza ya kuhukumu, hoja na mawazo bora,
1.3 Hadi zijiri takwimu, kuziepuka hasara,
1.4 Tumwombe sana Karimu, atwepushe na idhara.

2.1 Umoja si jambo gumu, si kikiri na kakara,
2.2 Kuwaza kwa kinidhamu, itikadi na fikira,
2.3 Yawe mema ya kudumu, tuinadi takibira,
2.4 Na kuchapa kazi ngumu, ibakiayo subira.

3.1 Tekeleza majukumu, wenye shida wana hera!
3.2 Tenda mambo kwa awamu, usifanye kwa papara,
3.3 Anza na ya kujikwimu, ufahari sio sera,
3.4 Hata wakikulaumu, usijitoe kafara.

4.1 Matendo mema hudumu, duniani na akhera.
4.2 Watendee binadamu, usingoje mshahara,
4.3 Kila mja na msimu, dunia ni mduara,
4.4 Chungu leo kesho tamu, wala haya si nadra.

5.1 Waja wema wana hamu, 'upae kama tiara',
5.2 Kila jema uhitimu, sifazo ziwe toara,
5.3 Lisiwepo jambo gumu, la kukutia harara,
5.4 Usiwe wa kukahimu, bali uwe barabara,

6.1 Siku hizi kuna simu, piga ukigaragara,
6.2 Huitaji baragumu, kuisambaza dhamira,
6.3 Kila mji na sehemu, imeenea minara,
6.4 Si ruhusu mahasimu, uwezo wakakupora,

7.1 Wapelekee salamu, wanasiasa chokora,
7.2 Kila wakimwaga sumu, iwageuke kafara,
7.3 Wakome kukuhujumu, hata bila ya bakora,
7.4 Katu usijilaumu, watapogeuzwa sura.

8.1 Wategemea mizimu, hawaijuwi kudra?
8.2 Hata waliosilimu, hawafanzi mas'hara,
8.3 Sembuse wao walimu, vilemba vilivyofura,
8.4 Hawaswabih ismu, Rabbika wao ni kura?

9.1 Natowa hii elimu, siambe nawacharura,
9.2 Kukosa kwao nidhamu, hakunitii hasira,
9.3 Bali ijuwe kaumu, weusi na machotara,
9.4 Kwamba hawa madhalimu, SI HAKI YAO KUPORA!!

Eur Ing. Omari Rashid Nundu
Iringa, Tanzania
28 Oktoba 2014
 
Vizuri sana. Hii ni fani inayopotea kwani binadamu wa sasa hawawezi hata kuandika Kiswahili fasaha. Makosa kidogo: hapo . 1.4 Waswahili husema 'izara' na siyo 'idhara' ndio neno 'kuazirika' ingawa kimakosa watu husema 'kuadhirika'
Kuadhirika inamaanisha kuwa na 'udhuru' wakati kuazirika ni kufedheheka.
 
Huyu ndio yule aliyekuwa waziri ama naona vibaya? Kweli tuliingizwa chaka kama ni yeye. Naomba kuuliza tu, mawaziri wote ni wabunge, hivi huwa wanakumbwa na nini pindi wanapovuliwa uwaziri kushindwa kutetea wananchi wao bungeni? Ama huwa hawakubaliani na usemi wa mpanda ngazi hushuka?
 
TAHADHARI MTANZANIA
1.1 Tafakari ni muhimu, kwa mja mwenye busara,
1.2 Kuwaza ya kuhukumu, hoja na mawazo bora,
1.3 Hadi zijiri takwimu, kuziepuka hasara,
1.4 Tumwombe sana Karimu, atwepushe na idhara.

2.1 Umoja si jambo gumu, si kikiri na kakara,
2.2 Kuwaza kwa kinidhamu, itikadi na fikira,
2.3 Yawe mema ya kudumu, tuinadi takibira,
2.4 Na kuchapa kazi ngumu, ibakiayo subira.

3.1 Tekeleza majukumu, wenye shida wana hera!
3.2 Tenda mambo kwa awamu, usifanye kwa papara,
3.3 Anza na ya kujikwimu, ufahari sio sera,
3.4 Hata wakikulaumu, usijitoe kafara.

4.1 Matendo mema hudumu, duniani na akhera.
4.2 Watendee binadamu, usingoje mshahara,
4.3 Kila mja na msimu, dunia ni mduara,
4.4 Chungu leo kesho tamu, wala haya si nadra.

5.1 Waja wema wana hamu, 'upae kama tiara',
5.2 Kila jema uhitimu, sifazo ziwe toara,
5.3 Lisiwepo jambo gumu, la kukutia harara,
5.4 Usiwe wa kukahimu, bali uwe barabara,

6.1 Siku hizi kuna simu, piga ukigaragara,
6.2 Huitaji baragumu, kuisambaza dhamira,
6.3 Kila mji na sehemu, imeenea minara,
6.4 Si ruhusu mahasimu, uwezo wakakupora,

7.1 Wapelekee salamu, wanasiasa chokora,
7.2 Kila wakimwaga sumu, iwageuke kafara,
7.3 Wakome kukuhujumu, hata bila ya bakora,
7.4 Katu usijilaumu, watapogeuzwa sura.

8.1 Wategemea mizimu, hawaijuwi kudra?
8.2 Hata waliosilimu, hawafanzi mas'hara,
8.3 Sembuse wao walimu, vilemba vilivyofura,
8.4 Hawaswabih ismu, Rabbika wao ni kura?

9.1 Natowa hii elimu, siambe nawacharura,
9.2 Kukosa kwao nidhamu, hakunitii hasira,
9.3 Bali ijuwe kaumu, weusi na machotara,
9.4 Kwamba hawa madhalimu, SI HAKI YAO KUPORA!!

Eur Ing. Omari Rashid Nundu
Iringa, Tanzania
28 Oktoba 2014

huyu mzee tangu apigwe chini na jk kapotea vibayA sana.ila hongera kwa ushairi mzuri.
 
TAHADHARI MTANZANIA
1.1 Tafakari ni muhimu, kwa mja mwenye busara,
1.2 Kuwaza ya kuhukumu, hoja na mawazo bora,
1.3 Hadi zijiri takwimu, kuziepuka hasara,
1.4 Tumwombe sana Karimu, atwepushe na idhara.

2.1 Umoja si jambo gumu, si kikiri na kakara,
2.2 Kuwaza kwa kinidhamu, itikadi na fikira,
2.3 Yawe mema ya kudumu, tuinadi takibira,
2.4 Na kuchapa kazi ngumu, ibakiayo subira.

3.1 Tekeleza majukumu, wenye shida wana hera!
3.2 Tenda mambo kwa awamu, usifanye kwa papara,
3.3 Anza na ya kujikwimu, ufahari sio sera,
3.4 Hata wakikulaumu, usijitoe kafara.

4.1 Matendo mema hudumu, duniani na akhera.
4.2 Watendee binadamu, usingoje mshahara,
4.3 Kila mja na msimu, dunia ni mduara,
4.4 Chungu leo kesho tamu, wala haya si nadra.

5.1 Waja wema wana hamu, 'upae kama tiara',
5.2 Kila jema uhitimu, sifazo ziwe toara,
5.3 Lisiwepo jambo gumu, la kukutia harara,
5.4 Usiwe wa kukahimu, bali uwe barabara,

6.1 Siku hizi kuna simu, piga ukigaragara,
6.2 Huitaji baragumu, kuisambaza dhamira,
6.3 Kila mji na sehemu, imeenea minara,
6.4 Si ruhusu mahasimu, uwezo wakakupora,

7.1 Wapelekee salamu, wanasiasa chokora,
7.2 Kila wakimwaga sumu, iwageuke kafara,
7.3 Wakome kukuhujumu, hata bila ya bakora,
7.4 Katu usijilaumu, watapogeuzwa sura.

8.1 Wategemea mizimu, hawaijuwi kudra?
8.2 Hata waliosilimu, hawafanzi mas'hara,
8.3 Sembuse wao walimu, vilemba vilivyofura,
8.4 Hawaswabih ismu, Rabbika wao ni kura?

9.1 Natowa hii elimu, siambe nawacharura,
9.2 Kukosa kwao nidhamu, hakunitii hasira,
9.3 Bali ijuwe kaumu, weusi na machotara,
9.4 Kwamba hawa madhalimu, SI HAKI YAO KUPORA!!

Eur Ing. Omari Rashid Nundu
Iringa, Tanzania
28 Oktoba 2014

Utenzi mzuri hongera
 
Great thinkers tunajadili somo sio mtu. Mimi nimeipenda hii ya kudumisha lugha na kutoa nasaha. Lakini nikusahihishe tu Chinga, huyu Mzee anaongea sana tena kwa busara kubwa, hajiropokei tu bungeni. Labda Chinga uangalii BUNGE na usikilizi radio wala kuangalia tv. Huyu ndiye chanzo cha bodaboda kusamehewa kodi. Ndie aliyeibuwa swala la posho kubwa za safari na bajeti kubwa ya matumizi. Ndie aliyeanzisha na kukoza majadiliano ya asilimia 10 za vijana na wanawake kwenye halimashauri. Ndiye anayesisitiza kuwa wafanya biashara wazalendo walioanzisha biashara mpya wapate 'tax holiday' ya miaka mitano badala ya kuwapa wawekezaji wanaotudanganya kwa kubadilisha majina kila miaka mitano. Huyu jamaa hayuko kimya na anavyoendelea hivi sijuwi analenga nini. Nimeeleza machache niyajuwayo lakini kuna wanaofuatilia zaidi. Ninaupenda ushairi wake na nasaha zake. Mimi ninaye mgombea wangu urais tayari kwa sababu zangu na nisingependa naye huyu aingie kwenye mbio hizo kwani kwa maswala ya rushwa na uwajibikaji anaweza akachukuwa uamuzi utakaomfanya aiage dunia mapema!
huyu mzee tangu apigwe chini na jk kapotea vibayA sana.ila hongera kwa ushairi mzuri.
 
Great thinkers tunajadili somo sio mtu. Mimi nimeipenda hii ya kudumisha lugha na kutoa nasaha. Lakini nikusahihishe tu Chinga, huyu Mzee anaongea sana tena kwa busara kubwa, hajiropokei tu bungeni. Labda Chinga uangalii BUNGE na usikilizi radio wala kuangalia tv. Huyu ndiye chanzo cha bodaboda kusamehewa kodi. Ndie aliyeibuwa swala la posho kubwa za safari na bajeti kubwa ya matumizi. Ndie aliyeanzisha na kukoza majadiliano ya asilimia 10 za vijana na wanawake kwenye halimashauri. Ndiye anayesisitiza kuwa wafanya biashara wazalendo walioanzisha biashara mpya wapate 'tax holiday' ya miaka mitano badala ya kuwapa wawekezaji wanaotudanganya kwa kubadilisha majina kila miaka mitano. Huyu jamaa hayuko kimya na anavyoendelea hivi sijuwi analenga nini. Nimeeleza machache niyajuwayo lakini kuna wanaofuatilia zaidi. Ninaupenda ushairi wake na nasaha zake. Mimi ninaye mgombea wangu urais tayari kwa sababu zangu na nisingependa naye huyu aingie kwenye mbio hizo kwani kwa maswala ya rushwa na uwajibikaji anaweza akachukuwa uamuzi utakaomfanya aiage dunia mapema!

ccm wote ni baba mmoja mam mmoja.thanks kwa maelezo yako mazuri.
 
Back
Top Bottom