Tahadhari kwa Timu ya CHADEMA?

Ninachoogopa ni kwamba JK anaweza akaigeuza ikawa hoja yake na kupata kisingizio cha kusafiri kwenda kutangaza kuwa Tanzania kuna demokrasia
 
tutumie fursa hii adimu ambayo Rais katoa kwa chadema kujenga hoja lakini pia kuwaongezea hoja chadema ambazo wakiwakilisha kwa Rais zitakuwa na manufaa kwa taifa letu.
 
chadema wana fursa nyingi ama kuacha kula chochote watakapofika Ikulu au kususa kwenda Ikulu kwa hofu ya kupewa sumu
 
Siku mtakapokutana na JK nawaomba muwe makini sana na vyakula na vinywaji vitakavyokuwepo kwa sababu hamuwezi kujua kwa nini kakubali haraka kukutana na nyie, ni mawazo yangu tu.
Ni kweli ndugu yangu, maana Viongozi wa Chadema ni binaadam kama walivyo watu wengine kama Mwakyembe.
 
Fikiria mara mbili hivi unafikiri kama Jk angeamua kutumia dola yake kuwadhuru chadema angeshindwa? mimi naamini anajua kuwa madhara ya kuwadhuru viongozi wa chadema chama kikuu cha upinzani kwa sasa ni makubwa kuliko kuwaacha na uhai wao. hawezi kutumia nafasi ya Ikulu kufanya usemayo
Hawezi chochote make CDM ndo inawafuasi wengi, na isingekuwa kuchakachua, asinge kuwa Rais, hiyo tu inampa hofu
 
Hili nalo neno, maswala ya polonium si mchezo. Hii nafasi si hadimu kama PIPIJOJO alivyo sema Jk ni kichaka tu ukisema wakati wowote umwone unamwona nothing special, anakutana na hata machangudoa then can not be special in that way.
 
kabidhi mchawi akutunzie mtoto, chadema mikononi mwa JK hawawezi kupata madhara kuliko nje ya JK. Watanzania wamekabidhi chadema kwa JK, Taifa limetoa baraka zake hakuna haja ya kurusha shutuma dhidi ya JK
 
tutumie fursa hii adimu ambayo Rais katoa kwa chadema kujenga hoja lakini pia kuwaongezea hoja chadema ambazo wakiwakilisha kwa Rais zitakuwa na manufaa kwa taifa letu.

Hivi unadhani kuna kitu ? Si ulimsikia akiongea na wazee wenye mawazo kama yake?
 
Kila kukicha hali ya kutokuaminiana hapa nchini imekuwa ikiongezeka kupelekea wanachi kutokuamini kama baadhi ya vifo na hata magonjwa yanayowapata watanzania wenzetu hayana mkono wa mtu. Katika wakati huu ambapo timu ya CHADEMA inajiandaa kukutana na Rais ni vyema ikazingatia pia swala la usalama mara itakapokuwa ugenini.

Kwanza: Wajumbe wasisalimiane/pongezana kwa kushikana mkono na mtu aliye vaa gloves
Pili: Siku hiyo wote wafunge.

Possibly, CHADEMA leadership might have considered and analysed security options otherwise this post is just an alert.

Hivi kwa mtizamo wako unadhani CHADEMA ni tishio kiasi hicho kwa CCM hadi wawahujumu? Umepotoka kwa hilo.
 
Hili nalo neno, maswala ya polonium si mchezo. Hii nafasi si hadimu kama PIPIJOJO alivyo sema Jk ni kichaka tu ukisema wakati wowote umwone unamwona nothing special, anakutana na hata machangudoa then can not be special in that way.

sasa kama sio fursa adimu kwa nini chadema wameomba kwa barua kwenda kumuona JK si wangeendelea na maandamano? nani kawazuia kuamndamana nchi nzima. Jk alishatoa msimamo wake alipoongea na Wazee nani hakusikia.
 
Siku mtakapokutana na JK nawaomba muwe makini sana na vyakula na vinywaji vitakavyokuwepo kwa sababu hamuwezi kujua kwa nini kakubali haraka kukutana na nyie, ni mawazo yangu tu.

Mawazo ya kijinga!
 
Hivi unadhani kuna kitu ? Si ulimsikia akiongea na wazee wenye mawazo kama yake?

ni fursa adimu kwenda kumshawishi na kumjuza kwamba ama alishauriwa vema au vibaya. kama chadema wataacha kujenga hoja fursa hiyo haina maana
 
chadema wametegwa walipoandika barua kwa Jk walifikiri atakaa kutokana na msimamo alioonyesha ndani ya hotuba yake kwa wazee.
 
Barua ya chadema kwa Jk ingeongeza aya ya wasiwasi wa kupewa sumu mbona mnakuja kusema hapa JF
 
Anne Makinda kawashindwa chadema bungeni akawaacha wakatoka bungeni sio vema na Jk akawashindwa wakatoka Ikulu bila kuaga. Ni muda muafaka kwetu kutengeneza mazingira ya kufanikisha mazungumzo ya Jk na chadema.
 
Back
Top Bottom