Tafsiri ya neno "kibamia" kisheria ni ipi?

Tafsiri ya neno "kibamia" kisheria ni ipi?

My Son drink water

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2016
Posts
4,930
Reaction score
13,335
Nchi ni lazima iongozwe kisheria ili kutoa haki kwa watu wake wote.
Taifa likiongozwa kwa mihemko ya chuki binafsi na chuki za kisiasa, hilo taifa huitwa " Maandazi Republic ".

Maana yake ni kwamba, ni taifa lisilo jitambua lilipotoka na linapokwenda.
Niliwahi kuhudhuria kesi ya rafiki yangu nchini Uingereza enzi zile nikibeba Box, rafiki yangu ambaye ni raia wa UK, alifikishwa mahakamani kwa kutuhumiwa kutoa lugha ya matusi kwa mtalaka wake.

Alimwambia ni mpumbavu na mjinga.
Siku ya hukumu, hakimu alimsafisha mtuhumiwa na kusema hana kosa lolote lile kisheria linalopaswa kumtia hatiani.

Hakimu alitoa hukumu na kusema.
"A fool is any person that lacks or completely suffers no prudence,hence having no prudence doesn't imply an insult, and a stupid is a person whose deeds show that he/she is absolutely uneducated,hence being a stupid doesn't mean that you have been insulted ".
"Mpumbavu ni mtu aliyepungukiwa au hana hekima kabisa, kuwa mpumbavu siyo tusi, na mjinga ni mtu ambaye matendo yake yanaonyesha kuwa hana Elimu, kuwa mjinga siyo kwamba umetukanwa".

Sehemu ya hukumu hiyo ilisema hivyo, hakimu alidai hivyo ndivyo alivyoitafsiri sheria.

Serikali inapoamua kumpiga marufuku msanii na kumfungia kazi zake kwa sababu tu ameimba kibamia, neno ambalo ni la mitaani ni kichekesho kweli.
Ni tafsiri ipi ya kisheria ambayo inatambua kuwa kibamia ni tusi?

Kibamia ni bamia ndogo kuliko zote, na bamia ni mboga, iweje leo Jamhuri,("The entire government is regarded as Republic and any decisions made by any top official therein are mentioned as decisions carried out by the Republic of the particular country ".)

Itambue kuwa kibamia ni tusi bila chombo cha kutafsiri sheria ambacho ni mahakama kuridhia?

Tanzania ni taifa linaloheshimika kimataifa kwa miaka mingi mno, hatutakubali kuwa "Maandazi Republic "kwa sababu ya watendaji wachache wa serikali kutunga sheria kandamizi kwa sababu zisizojulikana.

Serikali imejigeuza kuwa mahakama, shame on you!
 
Kaka Mimi nakubaliana na ww asilimia zote. Tatzo wanashindwa kujua Fasihi inakazi gani
 
Sasa huyo mtoa hukum alipatiwa nafasi kwa kupewa bamia sindio tatizo!

MTU anapopewa madaraka kwa kupitia mirindimo ya vibamia, bamia na mabamia.....hata kichwani amejaa utelezi wa mabamia

Usitegemee maamuzi ya wala mihogo.
 
Nchi ni lazima iongozwe kisheria ili kutoa haki kwa watu wake wote.
Taifa likiongozwa kwa mihemko ya chuki binafsi na chuki za kisiasa, hilo taifa huitwa " Maandazi Republic ".
Maana yake ni kwamba, ni taifa lisilo jitambua lilipotoka na linapokwenda.
Niliwahi kuhudhuria kesi ya rafiki yangu nchini Uingereza enzi zile nikibeba Box, rafiki yangu ambaye ni raia wa UK, alifikishwa mahakamani kwa kutuhumiwa kutoa lugha ya matusi kwa mtalaka wake.
Alimwambia ni mpumbavu na mjinga.
Siku ya hukumu, hakimu alimsafisha mtuhumiwa na kusema hana kosa lolote lile kisheria linalopaswa kumtia hatiani.
Hakimu alitoa hukumu na kusema.
"A fool is any person that lacks or completely suffers no prudence,hence having no prudence doesn't imply an insult, and a stupid is a person whose deeds show that he/she is absolutely uneducated,hence being a stupid doesn't mean that you have been insulted ".
"Mpumbavu ni mtu aliyepungukiwa au hana hekima kabisa, kuwa mpumbavu siyo tusi, na mjinga ni mtu ambaye matendo yake yanaonyesha kuwa hana Elimu, kuwa mjinga siyo kwamba umetukanwa".
Sehemu ya hukumu hiyo ilisema hivyo, hakimu alidai hivyo ndivyo alivyoitafsiri sheria.
Serikali inapoamua kumpiga marufuku msanii na kumfungia kazi zake kwa sababu tu ameimba kibamia, neno ambalo ni la mitaani ni kichekesho kweli.
Ni tafsiri ipi ya kisheria ambayo inatambua kuwa kibamia ni tusi?
Kibamia ni bamia ndogo kuliko zote, na bamia ni mboga, iweje leo Jamhuri,("The entire government is regarded as Republic and any decisions made by any top official therein are mentioned as decisions carried out by the Republic of the particular country ".)
Itambue kuwa kibamia ni tusi bila chombo cha kutafsiri sheria ambacho ni mahakama kuridhia?
Tanzania ni taifa linaloheshimika kimataifa kwa miaka mingi mno, hatutakubali kuwa "Maandazi Republic "kwa sababu ya watendaji wachache wa serikali kutunga sheria kandamizi kwa sababu zisizojulikana.
Serikali imejigeuza kuwa mahakama, shame on you!
Usishangae na wewe kupigwa marufuku usiandike JF mwaka mzima, chezea Fisiemu wewe.
 
Binti anautafuta uwaziri.
Ndio tatizo la rais kuwa nabteuzi nyingi na teuzi za kiki.
 
Sasa huyo mtoa hukum alipatiwa nafasi kwa kupewa bamia sindio tatizo!

MTU anapopewa madaraka kwa kupitia mirindimo ya vibamia, bamia na mabamia.....hata kichwani amejaa utelezi wa mabamia

Usitegemee maamuzi ya wala mihogo.
Tutakupendekeza uwe mtafsiri wa sheria[emoji122] [emoji122] [emoji122] [emoji122] [emoji122] [emoji122]
 
hata ukiweka sheria mahakama haziko huru........udikteta na maagizo kutoka juu...

"USAWA HAUPATIKANI KWA MZANI KUWA SAWA BALI HUTEGEMEA MPIMAJI MWENYEWE"
 
ni sheria ire ire iliyoipa haki neno "Mandazi Republic " ( in Njoroge voice)

ni kweli kabisa hapo sheia imekaa kushotoz na kama ni sanaa msanaa amefanikiwa sana kupeleka ujembe na kupnguza ukali wa maneno.

imgine angesemaa @@$%%oo ndogo nadhani angekuwa condemn now.

kuna nyimbo moja nimewahi kuisikiliza sijui aliimba nani lakini

kuna mistari kama wali nazi..matango nakulaga..maboga sijui nini by the angeuimba kavu kavu hata kama angetoa billion hakuna studio ingekubali kuurecord

LAW AND REGULATIONS HAVE BEEN SUSPENDED FOR A WHILE
 
Back
Top Bottom