Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,408
- 4,987
Mahakama ya Wilaya ya Makete mkoani Njombe imechukua hatua kali dhidi ya vitendo vya rushwa baada ya kuwahukumu maofisa wawili wa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS), Thadeus Mtui na Florian Kilango, kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya shilingi laki tano kila mmoja. Hukumu hiyo ilitolewa baada ya mahakama kuridhika kuwa watumishi hao waliomba na kupokea rushwa ya jumla ya shilingi milioni nane kutoka kwa mfugaji Yuda Male.
Mahakamani ilielezwa na mwendesha mashtaka wa TAKUKURU, Daniel Mono, kuwa washtakiwa hao walichukua fedha hizo kwa awamu mbili, ambapo Novemba 2025 walipokea shilingi milioni mbili na Januari 2026 wakachukua milioni sita nyingine. Fedha hizo zilitolewa na mfugaji Yuda Male ili aepuke kuchukuliwa hatua za kisheria baada ya kukutwa akiingiza mifugo ndani ya Hifadhi ya Msitu wa Chimala.
Hata hivyo, baada ya kuona anaendelea kusumbuliwa licha ya kutoa kiasi hicho kikubwa cha fedha, mfugaji huyo aliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya dola. Hakimu Mkazi Mfawidhi Irvan Msacky, mbali na kutoa adhabu hiyo, pia aliamuru fedha zote zilizochukuliwa zirudishwe, akisisitiza kuwa mahakama haitavumilia vitendo vya rushwa vinavyohatarisha uhifadhi wa rasilimali za taifa.
Mahakamani ilielezwa na mwendesha mashtaka wa TAKUKURU, Daniel Mono, kuwa washtakiwa hao walichukua fedha hizo kwa awamu mbili, ambapo Novemba 2025 walipokea shilingi milioni mbili na Januari 2026 wakachukua milioni sita nyingine. Fedha hizo zilitolewa na mfugaji Yuda Male ili aepuke kuchukuliwa hatua za kisheria baada ya kukutwa akiingiza mifugo ndani ya Hifadhi ya Msitu wa Chimala.
Hata hivyo, baada ya kuona anaendelea kusumbuliwa licha ya kutoa kiasi hicho kikubwa cha fedha, mfugaji huyo aliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya dola. Hakimu Mkazi Mfawidhi Irvan Msacky, mbali na kutoa adhabu hiyo, pia aliamuru fedha zote zilizochukuliwa zirudishwe, akisisitiza kuwa mahakama haitavumilia vitendo vya rushwa vinavyohatarisha uhifadhi wa rasilimali za taifa.