Tafakuri

Tafakuri

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
1,065
Reaction score
1,412
Tafakuri

❝Je, kama ningezaliwa katika dini nyingine kabisa, nikakulia humo na nikafa nikiwa bado kwenye dini hiyo — je, kwa mujibu wa dini nyingine nitahesabika nimepotea au kwenda motoni?

Na kama Mungu ndiye aliyeniumba, kwa nini tena aje kuniadhibu kwa kitu ambacho mazingira yangu ndiyo yamenilea kukiamini?

Je, haki ya Mungu ipo wapi kati ya kuzaliwa, mazingira, ukweli, na uchaguzi wa mwanadamu?❞

Je, binadamu ana uhuru kamili wa kuchagua anachoamini?

Au mazingira ya kuzaliwa ndiyo yanaamua mengi?

Mungu anamhukumu mtu kwa alichojua au kwa alichokikuta?

Mungu ni mwenye rehema na haki, je, atawezaje kumuadhibu mtu ambaye tangu utoto wake alifundishwa “huu ndio ukweli”?

Wewe mwenye Elimu unajibu vipi haya maswali

Abuuabdillah ✍️
0744 883 353
 
Tafakuri

❝Je, kama ningezaliwa katika dini nyingine kabisa, nikakulia humo na nikafa nikiwa bado kwenye dini hiyo — je, kwa mujibu wa dini nyingine nitahesabika nimepotea au kwenda motoni?

Na kama Mungu ndiye aliyeniumba, kwa nini tena aje kuniadhibu kwa kitu ambacho mazingira yangu ndiyo yamenilea kukiamini?

Je, haki ya Mungu ipo wapi kati ya kuzaliwa, mazingira, ukweli, na uchaguzi wa mwanadamu?❞

Je, binadamu ana uhuru kamili wa kuchagua anachoamini?

Au mazingira ya kuzaliwa ndiyo yanaamua mengi?

Mungu anamhukumu mtu kwa alichojua au kwa alichokikuta?

Mungu ni mwenye rehema na haki, je, atawezaje kumuadhibu mtu ambaye tangu utoto wake alifundishwa “huu ndio ukweli”?

Wewe mwenye Elimu unajibu vipi haya maswali

Abuuabdillah ✍️
0744 883 353


Kwa mujibu wa Uislamu, Qur'an inasisitiza kwamba Mwenyezi Mungu ni mwenye haki kamili na hamdhulumu mtu hata chembe.

Mwenyezi Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya iwezavyo..............” — Qur’an 2:286


Na pia:


Anayeongoka basi anaongoka kwa ajili ya nafsi yake. Na anayepotea basi anapotea kwa khasara yake mwenyewe. Wala habebi mbebaji mzigo wa mwengine. Wala Sisi hatukuwa wenye kuadhibu mpaka tupeleke Mtume.” — Qur’an 17:15


Maana yake ni kwamba Mungu humhukumu mtu kwa:

kiwango cha ukweli kilichomfikia,
uwezo wake wa kutambua,
nia yake,
na juhudi yake ya kutafuta haki.

Ndiyo, mazingira yana athari kubwa sana kwa binadamu. Mtoto huzaliwa kwenye dini, lugha na tamaduni bila kuchagua. Ndiyo maana katika Uislamu kuna dhana ya fitrah — kwamba kila mtu huzaliwa na maumbile ya kumtambua Mungu, lakini mazingira humwelekeza upande fulani.


Binadamu ana uhuru wa kuchagua, lakini si uhuru usioathiriwa na mazingira. Kwa hiyo hukumu ya Mungu si ya kipofu; ni ya haki, elimu kamili na rehema.


Ndiyo maana Muislamu hawezi kusema kwa uhakika kwamba kila asiye Muislamu ataingia motoni moja kwa moja, kwa sababu hukumu ya mwisho ni ya Mwenyezi Mungu ambaye anajua kilichomfikia kila mtu na kilichokuwa moyoni mwake.
 
Kwa mujibu wa Uislamu, Qur'an inasisitiza kwamba Mwenyezi Mungu ni mwenye haki kamili na hamdhulumu mtu hata chembe.

Mwenyezi Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya iwezavyo..............” — Qur’an 2:286


Na pia:


Anayeongoka basi anaongoka kwa ajili ya nafsi yake. Na anayepotea basi anapotea kwa khasara yake mwenyewe. Wala habebi mbebaji mzigo wa mwengine. Wala Sisi hatukuwa wenye kuadhibu mpaka tupeleke Mtume.” — Qur’an 17:15


Maana yake ni kwamba Mungu humhukumu mtu kwa:

kiwango cha ukweli kilichomfikia,
uwezo wake wa kutambua,
nia yake,
na juhudi yake ya kutafuta haki.

Ndiyo, mazingira yana athari kubwa sana kwa binadamu. Mtoto huzaliwa kwenye dini, lugha na tamaduni bila kuchagua. Ndiyo maana katika Uislamu kuna dhana ya fitrah — kwamba kila mtu huzaliwa na maumbile ya kumtambua Mungu, lakini mazingira humwelekeza upande fulani.


Binadamu ana uhuru wa kuchagua, lakini si uhuru usioathiriwa na mazingira. Kwa hiyo hukumu ya Mungu si ya kipofu; ni ya haki, elimu kamili na rehema.


Ndiyo maana Muislamu hawezi kusema kwa uhakika kwamba kila asiye Muislamu ataingia motoni moja kwa moja, kwa sababu hukumu ya mwisho ni ya Mwenyezi Mungu ambaye anajua kilichomfikia kila mtu na kilichokuwa moyoni mwake.
Umejibu vyema kabisa
 
Kwa mujibu wa Uislamu, Qur'an inasisitiza kwamba Mwenyezi Mungu ni mwenye haki kamili na hamdhulumu mtu hata chembe.

Mwenyezi Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya iwezavyo..............” — Qur’an 2:286


Na pia:


Anayeongoka basi anaongoka kwa ajili ya nafsi yake. Na anayepotea basi anapotea kwa khasara yake mwenyewe. Wala habebi mbebaji mzigo wa mwengine. Wala Sisi hatukuwa wenye kuadhibu mpaka tupeleke Mtume.” — Qur’an 17:15


Maana yake ni kwamba Mungu humhukumu mtu kwa:

kiwango cha ukweli kilichomfikia,
uwezo wake wa kutambua,
nia yake,
na juhudi yake ya kutafuta haki.

Ndiyo, mazingira yana athari kubwa sana kwa binadamu. Mtoto huzaliwa kwenye dini, lugha na tamaduni bila kuchagua. Ndiyo maana katika Uislamu kuna dhana ya fitrah — kwamba kila mtu huzaliwa na maumbile ya kumtambua Mungu, lakini mazingira humwelekeza upande fulani.


Binadamu ana uhuru wa kuchagua, lakini si uhuru usioathiriwa na mazingira. Kwa hiyo hukumu ya Mungu si ya kipofu; ni ya haki, elimu kamili na rehema.


Ndiyo maana Muislamu hawezi kusema kwa uhakika kwamba kila asiye Muislamu ataingia motoni moja kwa moja, kwa sababu hukumu ya mwisho ni ya Mwenyezi Mungu ambaye anajua kilichomfikia kila mtu na kilichokuwa moyoni mwake.
Sahihi
 
Ushasema Mungu ni mwingi wa Rehema na mwenye Haki, so tuna uhakika hukumu yake itakuwa ya haki kabisa, hatuhitaji kuwa na wasiwasi kuwa kuna mtu ataonewa.

Kwanza wote tumetenda dhambi, hakuna mwenye haki hata mmoja! ! Tunategemea rehema tu za Mungu kuishi milele maana tayari tushakosa vigezo vya kuishi.

Haki tunahesabiwa kwa kutetewa na YESU. Ndiyo njia pekee MUNGU anatuhesabu kuwa wenye haki:

"Haki hii inayotoka kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wanaomwamini. Kwa maana hapo hakuna tofauti,

kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu"

Waroma.3.22-23.NENO2025


Kwa ambao hawajamsikia Yesu?


1) Kwanza je anamtambua Muumba wake moyoni mwake?

"Kwa maana yote yanayoweza kujulikana kumhusu Mungu ni dhahiri kwao, kwa sababu Mungu mwenyewe ameyadhihirisha kwao.

Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, uwezo wake wa milele na uungu wake, ingawa havionekani kwa macho, vinafahamika wazi. Watu wanaweza kuyajua mambo hayo kutokana na vitu hivyo alivyoumba Mungu. Kwa hiyo hawana njia yoyote ya kujitetea!"

Waroma.1.19-20.BHND


2) Pili anajitahidi kufanya yaliyo haki / mema kwa kadri ya ufahamu wake kama yule Jemedari wa kiroma Kornelio? Hadi Mungu akamtuma Petro kwake amuambie habari za Yesu. Mpaka hapo tunaona kufanya mema hakutoshi, Kornelio alipaswa kukiri imani juu ya YESU.

"Kulikuwa na mtu mmoja huko Kaisarea aitwaye Kornelio, jemadari wa kikosi kimoja kiitwacho “Kikosi cha Italia.”

Alikuwa mtu mwema; naye pamoja na jamaa yake yote walimcha Mungu; alikuwa anafanya mengi kusaidia maskini wa Kiyahudi na alikuwa anasali daima."


Matendo.10.1-2.BHND


"Mathalani: Watu wa mataifa mengine hawana sheria; lakini kila wanapotimiza matakwa ya sheria wakiongozwa na dhamiri zao, wao wenyewe wanakuwa kipimo cha sheria ingawa hawaijui sheria.

Mwenendo wao unaonesha kwamba matakwa ya sheria yameandikwa mioyoni mwao. Dhamiri zao zinashuhudia pia jambo hilo, maana fikira zao mara nyingine huwashtaki, na mara nyingine huwatetea."


Waroma.2.14-15.BHND


3) Mwisho wa siku Mungu anawajua wateule wake tangu hata hajaumba. Yani alikaa akafikiri akawaona watu wake hawa ni wangu, kabla hata hajaumba

"Kwa maana alituchagua katika yeye kabla ya kuumbwa kwa ulimwengu ili tuwe watakatifu na bila lawama mbele zake. Kwa upendo"
Waefeso.1.4.NENO2025


4) Na Mungu halazimishi anataka watu wanaomchagua kwa hiari. Kwahiyo wateule sio kama kawalazimisha.

"Mtu yeyote akipenda kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu au ninasema kwa ajili yangu mwenyewe."
Yohana.7.17.NENO2025


"Ndipo akawaita umati ule wa watu pamoja na wanafunzi wake, akasema, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate."
Marko.8.34.NENO2025


5) Neema ya Mungu itawafikia wateule wake ambao huku tunaweza kuona hawafai / hawastahili, hata ambao hawakumsikia Yesu.

Na wengine Neema itawapita ingawa tunawaona ni watu "wazuri", hasa waliosikia kuhusu Yesu na wakamkataa.  Ndiposa Rehema na Utukufu wa Mungu itakapodhihirishwa waziwazi kwa watakaookolewa

"Tuseme nini basi? Je, Mungu ni dhalimu? La, hasha!

Kwa maana Mungu alimwambia Musa, “Nitamrehemu yeye nimrehemuye, na pia nitamhurumia yeye nimhurumiaye.”

Kwa hiyo haitegemei kutaka kwa mwanadamu au jitihada, bali hutegemea huruma ya Mungu.

Iweje basi, kama Mungu kwa kutaka kuonesha ghadhabu yake na kufanya uweza wake ujulikane, amevumilia kwa uvumilivu mwingi vile vyombo vya ghadhabu vilivyoandaliwa kwa uharibifu?

Iweje basi, kama yeye alitenda hivi ili kufanya wingi wa utukufu wake ujulikane kwa vyombo vya rehema yake, alivyotangulia kuvitengeneza kwa ajili ya utukufu wake?

Hivi vyombo ni sisi, ambao pia alituita, sio kutoka kwa Wayahudi peke yao, bali pia kutoka kwa watu wa Mataifa."

Waroma.9.14-24.NENO
 
Tafakuri

❝Je, kama ningezaliwa katika dini nyingine kabisa, nikakulia humo na nikafa nikiwa bado kwenye dini hiyo — je, kwa mujibu wa dini nyingine nitahesabika nimepotea au kwenda motoni?

Na kama Mungu ndiye aliyeniumba, kwa nini tena aje kuniadhibu kwa kitu ambacho mazingira yangu ndiyo yamenilea kukiamini?

Je, haki ya Mungu ipo wapi kati ya kuzaliwa, mazingira, ukweli, na uchaguzi wa mwanadamu?❞

Je, binadamu ana uhuru kamili wa kuchagua anachoamini?

Au mazingira ya kuzaliwa ndiyo yanaamua mengi?

Mungu anamhukumu mtu kwa alichojua au kwa alichokikuta?

Mungu ni mwenye rehema na haki, je, atawezaje kumuadhibu mtu ambaye tangu utoto wake alifundishwa “huu ndio ukweli”?

Wewe mwenye Elimu unajibu vipi haya maswali

Abuuabdillah ✍️
0744 883 353
Kinachokupeleka mbinguni siyo dini.

Kinachokupeleka Mbinguni ni Moyo wako Thabiti pamoja na matendo yako.
 
Umepewa hekima ya kuchanganua mambo, kwa mfano nimekuta wazazi wangu Kuna mila na desturi walikua nazo ila nimezitupilia mbali baada ya kuona hazina tija.
Dini uliyozaliwa humo, una uwezo wa kutafakari kama ni sahihi kuendelea kubaki humo.
 
Na hayo matendo tunayashape vipi na kwa utaratibu gani kama sio kupitia miongozo ya hizohizo dini? Au yameandikwa wapi hayo tunayopaswa kuyaenendaNa hayo matendo tunayashape vipi na kwa utaratibu gani kama sio kupitia miongozo ya hizohizo dini? Au yameandikwa wapi hayo tunayopaswa kuyaenenda
Ndiyo mana nasema dini ni muongozo tu, lakini siyo kigezo cha kumfikisha mtu Mbinguni.
 
Dini ni utapeli.

Hakuna Mungu.

Live your life to the fullest.

Habari za dini na Mungu ni hadithi za danganya toto!


Wewe kusema “dini ni utapeli” hakufanyi uwe na akili zaidi ya wengine ni kauli rahisi isiyo na ushahidi mzito. Ulimwengu huu wenye mpangilio, sheria zake na uhai wake haujitokezi tu bila chanzo. Kukataa Mungu hakumaanishi Mungu hayupo, ina maana tu wewe hutaki kukubali uwepo wake.

Kusema dini ni hadithi za “danganya toto” ni kupuuza historia, falsafa, na mabilioni ya watu waliopata maana, maadili, na mwelekeo wa maisha kupitia imani. Kama dini ni ujinga, basi eleza kwa hoja madhubuti chanzo cha maadili, kusudi la maisha, na uhai wenyewe, si kelele za mitandaoni.

“Live your life to the fullest” bila msingi wa maadili ni kauli tupu. Bila mwongozo, “fullest” yako inaweza kuwa uharibifu kwa wengine. Dini haijawahi kuwa tatizo, tatizo ni watu wanaokosa kuelewa au kuitumia vibaya.

Kwa kifupi: kukataa si hoja, ni msimamo. Leta ushahidi na mantiki, si maneno makali yasiyo na mizizi.


Mjibu kiislamu


Sawa, ukitaka jibu la kiislamu lenye msimamo mkali lakini hoja, unaweza kumjibu hivi:

Kauli yako ya kusema “hakuna Mungu” ni madai makubwa sana, na katika Uislamu, madai yanahitaji dalili. Qur'an inasema wazi kwamba:

“Au wameumbwa pasipo na kitu, au wao ndio waumbaji?” (52:35)

Hii ni hoja ya msingi kabisa: huwezi kuwepo bila chanzo. Wewe, ulimwengu, na kila kitu kilicho na mpangilio haviwezi kujitokeza tu bila Muumba. Kukataa hilo si akili, ni kukwepa ukweli.

Unaposema dini ni “hadithi za danganya toto”, unapuuzia ukweli kwamba Uislamu umesimama juu ya wahyi (ufunuo), mantiki, na historia iliyo wazi ya Muhammad—mtu ambaye hakuwa mwongo, wala hakufundisha ujinga bali tauhidi, haki, na maadili yaliyoinua jamii.

Uislamu haujawahi kusema uishi kiholela. “Live your life to the fullest” bila mipaka ya halali na haramu ni kufuata matamanio tu. Qur'an inaonya:

“Je, umemwona aliyefanya matamanio yake kuwa mungu wake?” (45:23)

Hapo ndipo tatizo lilipo, sio dini, bali mtu anayejifanya yeye ndiye kipimo cha kila kitu.
 
Ndiyo mana nasema dini ni muongozo tu, lakini siyo kigezo cha kumfikisha mtu Mbinguni.

Katika Uislamu, dini siyo muongozo tu, bali ndiyo njia aliyoweka Mwenyezi Mungu ya kumfikisha mtu Peponi. Qur'an inasema: ‘Hakika dini mbele ya Allah ni Uislamu’ (3:19).
Matendo mema ni muhimu, lakini lazima yaambatane na imani sahihi na kumtii Mwenyezi Mungu.
 
Ushasema Mungu ni mwingi wa Rehema na mwenye Haki, so tuna uhakika hukumu yake itakuwa ya haki kabisa, hatuhitaji kuwa na wasiwasi kuwa kuna mtu ataonewa.

Kwanza wote tumetenda dhambi, hakuna mwenye haki hata mmoja! ! Tunategemea rehema tu za Mungu kuishi milele maana tayari tushakosa vigezo vya kuishi.

Haki tunahesabiwa kwa kutetewa na YESU. Ndiyo njia pekee MUNGU anatuhesabu kuwa wenye haki:

"Haki hii inayotoka kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wanaomwamini. Kwa maana hapo hakuna tofauti,

kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu"

Waroma.3.22-23.NENO2025


Kwa ambao hawajamsikia Yesu?


1) Kwanza je anamtambua Muumba wake moyoni mwake?

"Kwa maana yote yanayoweza kujulikana kumhusu Mungu ni dhahiri kwao, kwa sababu Mungu mwenyewe ameyadhihirisha kwao.

Tangu Mungu alipoumba ulimwengu, uwezo wake wa milele na uungu wake, ingawa havionekani kwa macho, vinafahamika wazi. Watu wanaweza kuyajua mambo hayo kutokana na vitu hivyo alivyoumba Mungu. Kwa hiyo hawana njia yoyote ya kujitetea!"

Waroma.1.19-20.BHND


2) Pili anajitahidi kufanya yaliyo haki / mema kwa kadri ya ufahamu wake kama yule Jemedari wa kiroma Kornelio? Hadi Mungu akamtuma Petro kwake amuambie habari za Yesu. Mpaka hapo tunaona kufanya mema hakutoshi, Kornelio alipaswa kukiri imani juu ya YESU.

"Kulikuwa na mtu mmoja huko Kaisarea aitwaye Kornelio, jemadari wa kikosi kimoja kiitwacho “Kikosi cha Italia.”

Alikuwa mtu mwema; naye pamoja na jamaa yake yote walimcha Mungu; alikuwa anafanya mengi kusaidia maskini wa Kiyahudi na alikuwa anasali daima."


Matendo.10.1-2.BHND


"Mathalani: Watu wa mataifa mengine hawana sheria; lakini kila wanapotimiza matakwa ya sheria wakiongozwa na dhamiri zao, wao wenyewe wanakuwa kipimo cha sheria ingawa hawaijui sheria.

Mwenendo wao unaonesha kwamba matakwa ya sheria yameandikwa mioyoni mwao. Dhamiri zao zinashuhudia pia jambo hilo, maana fikira zao mara nyingine huwashtaki, na mara nyingine huwatetea."


Waroma.2.14-15.BHND


3) Mwisho wa siku Mungu anawajua wateule wake tangu hata hajaumba. Yani alikaa akafikiri akawaona watu wake hawa ni wangu, kabla hata hajaumba

"Kwa maana alituchagua katika yeye kabla ya kuumbwa kwa ulimwengu ili tuwe watakatifu na bila lawama mbele zake. Kwa upendo"
Waefeso.1.4.NENO2025


4) Na Mungu halazimishi anataka watu wanaomchagua kwa hiari. Kwahiyo wateule sio kama kawalazimisha.

"Mtu yeyote akipenda kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu au ninasema kwa ajili yangu mwenyewe."
Yohana.7.17.NENO2025


"Ndipo akawaita umati ule wa watu pamoja na wanafunzi wake, akasema, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate."
Marko.8.34.NENO2025


5) Neema ya Mungu itawafikia wateule wake ambao huku tunaweza kuona hawafai / hawastahili, hata ambao hawakumsikia Yesu.

Na wengine Neema itawapita ingawa tunawaona ni watu "wazuri", hasa waliosikia kuhusu Yesu na wakamkataa.  Ndiposa Rehema na Utukufu wa Mungu itakapodhihirishwa waziwazi kwa watakaookolewa

"Tuseme nini basi? Je, Mungu ni dhalimu? La, hasha!

Kwa maana Mungu alimwambia Musa, “Nitamrehemu yeye nimrehemuye, na pia nitamhurumia yeye nimhurumiaye.”

Kwa hiyo haitegemei kutaka kwa mwanadamu au jitihada, bali hutegemea huruma ya Mungu.

Iweje basi, kama Mungu kwa kutaka kuonesha ghadhabu yake na kufanya uweza wake ujulikane, amevumilia kwa uvumilivu mwingi vile vyombo vya ghadhabu vilivyoandaliwa kwa uharibifu?

Iweje basi, kama yeye alitenda hivi ili kufanya wingi wa utukufu wake ujulikane kwa vyombo vya rehema yake, alivyotangulia kuvitengeneza kwa ajili ya utukufu wake?

Hivi vyombo ni sisi, ambao pia alituita, sio kutoka kwa Wayahudi peke yao, bali pia kutoka kwa watu wa Mataifa."

Waroma.9.14-24.NENO


Katika Uislamu, kila mtu anawajibika kwa matendo yake mwenyewe mbele ya Mwenyezi Mungu, si kubebewa dhambi na mtu mwingine.

Qur'an inasema: ‘Na mbebaji habebi mzigo wa mwingine’ (6:164).

Pia Allah ni Mwingi wa rehema na anasamehe anayemrudia kwa toba ya kweli bila kupitia kwa mtu yeyote. Jesus katika Uislamu ni Nabii mtukufu, si mwenye kubeba dhambi za watu.”
 
Tafakuri

❝Je, kama ningezaliwa katika dini nyingine kabisa, nikakulia humo na nikafa nikiwa bado kwenye dini hiyo — je, kwa mujibu wa dini nyingine nitahesabika nimepotea au kwenda motoni?

Na kama Mungu ndiye aliyeniumba, kwa nini tena aje kuniadhibu kwa kitu ambacho mazingira yangu ndiyo yamenilea kukiamini?

Je, haki ya Mungu ipo wapi kati ya kuzaliwa, mazingira, ukweli, na uchaguzi wa mwanadamu?❞

Je, binadamu ana uhuru kamili wa kuchagua anachoamini?

Au mazingira ya kuzaliwa ndiyo yanaamua mengi?

Mungu anamhukumu mtu kwa alichojua au kwa alichokikuta?

Mungu ni mwenye rehema na haki, je, atawezaje kumuadhibu mtu ambaye tangu utoto wake alifundishwa “huu ndio ukweli”?

Wewe mwenye Elimu unajibu vipi haya maswali

Abuuabdillah ✍️
0744 883 353
Tatizo lako ni kufikiri kuwa mtu anapozaliwa ndio mwanzo wake. Hizi roho zilikuwepo kabla ya huu ulimwengu mzee na hicho ulicho ndio sehemu ya ule wema au ubaya wako na ikitokea umevuka mpaka ukaenda kwingine au kuzaliwa kwingine lazima utaonyeshwa ukweli na utarud vivyo hivyo kwa ile roho iliyopotea ikijikuta sehem kwema itarud yenyewe sehem chafu. Isome biblia ujue ukweli mwingi uliojificha chief. Unavyoambiwa nalikujua kabla ya kuumbwa kwa ulimwengu jiongeze
 
Katika Uislamu, dini siyo muongozo tu, bali ndiyo njia aliyoweka Mwenyezi Mungu ya kumfikisha mtu Peponi. Qur'an inasema: ‘Hakika dini mbele ya Allah ni Uislamu’ (3:19).
Matendo mema ni muhimu, lakini lazima yaambatane na imani sahihi na kumtii Mwenyezi Mungu.
Ukishatenda matendo mema obvious unakuwa unamtii Mungu, vinabaki vipengele vingine vichache vya kufuatisha kwenye dini lakini hivyo binafsi naona kama ni ziada, ila msingi mkuu ni kuishi katika mema.
 
Back
Top Bottom