TAFAKARI: Ni wanyonge gani hawa?

Samiaagain2025

JF-Expert Member
Dec 2, 2020
2,926
3,054
Wanajamvi heshima kwenu,

Tangu mwanzo na hata sasa, serikali ya awamu ya tano inajipambanua kama "serikali ya wanyonge". Wananchi wengi sasa wanazidi kuuliza kuwa hawa ni wanyonge wa aina gani?:
  • Wakulima ambao bei za mazao yao hazieleweki, mfano: bei ya pamba na korosho.
  • Wanufaika wa HESLB wanaodaiwa mamilioni ya pesa huku wakiongezewa na "retention fee'?
  • Wahitimu wa vyuo wasio na ajira na wamesota kwa takribani miaka 5?
  • Watumishi wa umma wanaolia kuongezewa mishahara na kupandishwa madaraja?
  • Wastaafu wanaodai mafao yao NSSF na PSSSF kwa tabu na usumbufu mkubwa?
  • Kwani wananchi wanaosomesha watoto wao bure sekondari wanafaidika na nini kama vijana hao hawapati ajira kwa wingi?
  • Wanaochapwa viboko na baadhi ya maofisa wa serikali?
  • Walipakodi na TRA?
Haya ni baadhi tu ya maswali ili kubainisha wanyonge wanaoongelewa na serikali hii ni akina nani hasa.

Tutafakari.
 
Naipenda nchi yangu ila siipendi mufumo yake ya kiongozi au kiutawala. Kweli number tunaisoma😭
Mitano tenaaaa au nasema uongo jamani?
 
Yqani jamaa anatuita wanyonge tunekaa tunamchekea tu. Maisha yanakwenda mrama tunamwagalia tu'!.

Hivi nchi hii tuna wanajeshi kweli? Ama tunawapiganaji tu?

Nchi hii tuna vyombo vya dola? Ama tuna vyombo vya jikoni tu?
 
Yqani jamaa anatuita wanyonge tunekaa tunamchekea tu. Maisha yanakwenda mrama tunamwagalia tu'!...
Hivyo vyombo vimeshakuwa penetrated na wana siasa.

Maybe hapo nyuma walikuwa na uwezo huo.. lakin kwa sasa hawana ujanja
 
Yapo majinga huswa haya mataga yanajiproud kabsa kuitwa wanyonge huku yakishangilia kwa uzuzu wao
 
Yqani jamaa anatuita wanyonge tunekaa tunamchekea tu. Maisha yanakwenda mrama tunamwagalia tu'!.

Hivi nchi hii tuna wanajeshi kweli? Ama tunawapiganaji tu?

Nchi hii tuna vyombo vya dola? Ama tuna vyombo vya jikoni tu?
Wanyonge wameamua kuishi kinyonge
 
Back
Top Bottom