payuka
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 829
- 127
Kama mtaikumbuka vizuri historia katika chaguzi mbalimbali zilizoihusisha CCM, ndani na nje ya chama chao hawa jamaa hawajawahi kufanya uchaguzi wowote ulioisha salama bila tuhuma zozote.
Walianza Kwa Kuchakachua ndani ya chama chao kwenye Kura za maoni, waliwanyima haki wale walioshinda kwa Kuchaguliwa kihalali na wananchi. Matumizi mabaya ya fedha ili kufanikisha Rushwa zao yalishika nafasi kubwa sana katika mchakato ule.
Ni taswira hii hii ambayo imejirudia kwenye uchaguzi mkuu, matumizi ya pesa na ubabe ndo yamechukua nafasi. Wameshindwa kuheshimu maamuzi ya wananchi kwa tamaa na uchu wa madaraka. Wasidhani Wananchi ni wapumbavu walivokaa kimya.
Nahitimisha kwa kusema hakuna jambo lisilo na mwisho, Ipo siku!!
Walianza Kwa Kuchakachua ndani ya chama chao kwenye Kura za maoni, waliwanyima haki wale walioshinda kwa Kuchaguliwa kihalali na wananchi. Matumizi mabaya ya fedha ili kufanikisha Rushwa zao yalishika nafasi kubwa sana katika mchakato ule.
Ni taswira hii hii ambayo imejirudia kwenye uchaguzi mkuu, matumizi ya pesa na ubabe ndo yamechukua nafasi. Wameshindwa kuheshimu maamuzi ya wananchi kwa tamaa na uchu wa madaraka. Wasidhani Wananchi ni wapumbavu walivokaa kimya.
Nahitimisha kwa kusema hakuna jambo lisilo na mwisho, Ipo siku!!